Fremu zinazojengwa hapa eneo la Jeshi Lugalo hadi njiapanda ya Kawe zitapangishwa raia au kwa askari tu?

wa stendi

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2016
Posts
25,190
Reaction score
27,434
Hizi fremu ni nyingi sana kama ziko chini ya JW wamefanya la maana sana kuliko kulivyokuwa na pori linatufugia viumbe hatarishi na misitu isiyokuwa na faida.

Yaani ukifika usawa wa Lugalo upande wa kushoto (kama unatoka Mwenge kwenda Tegeta mkono wa kulia) zimejengwa hadi kona ya kwenda kawe yaani ni nyingi sana!

Je, hizi zitapangishwa kwa familia za askari tu au hata mtu ambaye sio askari ataruhusiwa?
 
Niliposikia tu sababu ya kupelekea Ujenzi huo jinsi ilivyo ya Kipuuzi (kutokana na Unyeti wa hiyo Kambi) kwa Tanzania nzima ni kwamba nchi yetu sasa iko Uchi kabisa kwa Maadui na ipo Siku Tanzania itakuwa Mali ya Taifa lingine.
 
Kuzipata hizo itakua ni issue, nadhani watakodisha hadi kwa watu binafsi ila kipaombele watapeana wao wenyewe kwanza
Ni Mradi wa Kikosi #34KJ hapo Lugalo ambao Unajumuiisha Askari wa Vyeo mbalimbali (japo wale Commissioned ndiyo wengi ) ambapo walitakiwa kuzijenga Wenyewe na wakishaanza Biashara hawatodaiwa Kodi kwa (ndani) ya miaka Miwili.
 
Niliposikia tu sababu ya kupelekea Ujenzi huo jinsi ilivyo ya Kipuuzi ( kutokana na Unyeti wa hiyo Kambi ) kwa Tanzania nzima ni kwamba nchi yetu sasa iko Uchi kabisa kwa Maadui na ipo Siku Tanzania itakuwa Mali ya Taifa lingine.
Hiyo kambi ni ya makazi ya askari, na hospitali ya jeshi, haina siri za kuficha kihiivyo.

Maana raia wanaruhusiwa hapo 24/7 kama wakazi wa katika nyumba za ndugu zao wanajeshi na pia kama wagonjwa hospitali, halafu kuna shule pia pale, kwahiyo sio sensitive kihivyo.
 
Kuna nyama fulani ipo kule sikumbuki vizuri ni kitimoto au mbuzi tabu ukilewa na ukaanza vurugu sijui inakuwaje itakuwa kama unampapasa simba jike wakati ananjaa kwa kumbembeleza atulie chakula kinakuja.
 
Hauko 'Security Conscious' hivyo huna unachokijua na tafafhali acha Kunipotezea muda ila kuna Siku Tanzania ikivamiwa kirahisi na Watanzania kuwa Mali ya Nchi nyingine ndiyo mtatuelewa Wenye Akili Kubwa, Maono na Machale ya Kutukuka.
 
Askari sio raia kwani?.
 
Kuna bar na bwalo la sherehe pia mule ndani raia wanajichanganya tu
 
Vyovyote vile, kujenga fremu za biashara jeshini hawezi kuwa wazo zuri.
 
Ni Mradi wa Kikosi #34KJ hapo Lugalo ambao Unajumuiisha Askari wa Vyeo mbalimbali ( japo wale Commissioned ndiyo wengi ) ambapo walitakiwa Kuzijenga Wenyewe na wakishaanza Biashara hawatodaiwa Kodi kwa ( ndani ) ya miaka Miwili.
Huyu jamaa nahisi simzalendo kabisa hivi atakambi zamalekani huagawanafuga mapoli
 
Acha kutisha watu, nchi huru hii.
Hauko 'Security Conscious' hivyo huna unachokijua na tafafhali acha Kunipotezea muda ila kuna Siku Tanzania ikivamiwa kirahisi na Watanzania kuwa Mali ya Nchi nyingine ndiyo mtatuelewa Wenye Akili Kubwa, Maono na Machale ya Kutukuka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…