From the book 'I am the State' (Mimi ni Dola)

From the book 'I am the State' (Mimi ni Dola)

Mnangoja nini kuandika hicho kitabu cha mema yake, au nyie sio wabunifu bali ni watu wa kuiga tu baada ya wabunifu kuanzisha jambo?

Mema huwa hayatajwi,maana huwa yanaonekana.
 

Yaliyojificha uwekezaji wa Hayati Dk Magufuli Chato yawekwa vitabuni​

Ijumaa, Aprili 14, 2023
magufuli-pic.jpg


Dar es Salaam. Ikiwa ni miaka miwili tangu aliyekuwa Rais wa Tanzania, Dk John Magufuli kupoteza maisha Machi 17, 2021 akiwa madarakani, waandishi wakongwe wanne wamezindua kitabu kinachoonyesha sura ya kiongozi huyo na uwekezaji mkubwa alioupeleka wilayani Chato.

Absalom Kibanda, Ansbert Ngurumo, Neville Meena na Jesse Kwayu ndio waandishi walioandika kitabu hicho chenye jina 'I am the State' ikiwa na maana Mimi ndio Dola.

Kitabu hicho linaonyesha hali ilivyo sasa wilayani Chato alipozaliwa kiongozi huyo mkuu wa nchi baada ya miradi mikubwa ya maendeleo
Miongoni mwa mambo yaliyoangaziwa katika kitabu hicho ni wanyama waliopelekwa Chato enzi ya utawala wa Rais Dk Magufuli, ujenzi wa kiwanja cha ndege, uboreshaji mkubwa wa miundombinu, wananchi kukimbilia kununua viwanja, ujenzi wa masoko na miradi mingineyo.

Pia kitabu hicho kimeangazia fedha zilizopelekwa wilayani huko zitarejeshwaje, mpango wa wilaya hiyo kuandaliwa kuwa mkoa uko uliishia wapi.

Kabla ya uzinduzi wa kitabu hicho Ansbert Ngurumo amesema jina la kitabu limetokana na hofu iliyoshuhudiwa baada ya utawala wa hayati Dk Magufuli tangu mwaka 2015-2021 kuelekeza miradi mingi eneo alikozaliwa bila kuwepo mtu aliyehoji.

Amesema kilichofanyika ndani ya utawala wa Dk Magufuli ilikuwa ni historia ya kipekee kwani awamu zote za viongozi waliopita hapa nchini hakukuwa na kiongozi aliyefanya uwekezaji mkubwa eneo alilotoka.

Mbali na uwekezaji walioutaja kuwa na dalili zote za ubinafsi alioufanya kiongozi huyo, amesema upo ukandamizaji mkubwa alioufanya kwenye jamii na kutoa kauli zenye vitisho kuonyesha hakuna aliye juu yake.

"Kama mnafikiri mpo huru kiasi hicho watch it,"Kauli hayati Dk Magufuli enzi ya uhai wake ambaye imeleta tafsiri kwenye kitabu hicho namna ambavyo uongozi wake haukutetereshwa na kitu chochote.

Akizindua kitabu hicho Askofu wa Jimbo la Karagwe mkoani Kagera, Dk Benson Bagonza amesema uandishi wa kitabu hicho uwe chachu kwa viongozi wastaafu na walio madarakani kuandikiwa vitabu kulingana na mazuri na mabaya yao.

Amesema kitabu cha I am the State kinaonyesha namna fedha za umma zilivyotumika nje ya bajeti ya bajeti ya serikali.

"Mambo yaliyotajwa katika kitabu hiki yalitendeka nchi ikiwa gizani na watu walinyamazishwa na haya yaliyoandikwa ni sehemu ndogo ya yaliyotendeka nchi ikiwa gizani"amesema.
Hawa ni wapumbavu.. kwanini hawajaenda kuuliza imekuaje sumbawanga mjini kuna barabara safi na taa za pembezoni.. ?

Simba akizeeka kukimbilia waliko fisi.

Kwanza serikali ipige marifuku hiki kitabu..
 
Hawa ni wapumbavu.. kwanini hawajaenda kuuliza imekuaje sumbawanga mjini kuna barabara safi na taa za pembezoni.. ?

Simba akizeeka kukimbilia waliko fisi.

Kwanza serikali ipige marifuku hiki kitabu..
Waambie serikali wakifute basi
 
Mema huwa hayatajwi,maana huwa yanaonekana.
Kwako ni mema, sisi tunaona ni wajibu wa serikali kupitia kodi za wananchi. Nenda Afrika kusini kama kuna mweusi yoyote anasema miundombinu iliyojengwa na makuburu ni wema. Usichanganye wema na wajibu. Angekuwa volunteer kisha afanye aliyofanya ungetamka neno wema.
 
Ukiuwa kwa upanga utakufa kwa upanga!! Kama alipewa sumu na wewe uliyempa sumu utakufa kwa sumu!!

Kitabu kimeandikwa na wapinzani sijaona Cha achabu hapo!

Hata kama angekuwa mwizi mwenye kupendelea kwao alikumbuka pia na kwengine.SGR ,Ndege, Mwalimu nyerere hydrolylic power ,Lami zilitandikwa kila Kona ya Nchi, hospitali zilijengwa kila Kona ya Nchi NK ,nK,nK.

Kwani chato siyo Tanzania au? Acheni upumbavu wa kiwango Cha upumbavu!!

Lakini pia afadhali mwizi mmoja kuliko Nchi inavyoliwa kama mchwa kila Kona ya Nchi kwa sasa.soma ripoti ya CAG ndiyo utaona sasa Nchi inavyoliwa kama mchwa! Maofisini hamna madili ya Kazi tena.

Na kwani kitabubkizindukiwe na askofu Bagonza ambaye tunajua alikuwa mpinzani wake.Ndiyo maana Mtu mmoja kasema bukoba ni maskini japo ni wasomi kwa sababu ya ujuaji na usomi wa kijinga.kitabu hicho kikae kanisani kwake wakasome na masisters zake.

Serikali ikipige marufuku likitabu hilo
 
Hawa ni wapumbavu.. kwanini hawajaenda kuuliza imekuaje sumbawanga mjini kuna barabara safi na taa za pembezoni.. ?

Simba akizeeka kukimbilia waliko fisi.

Kwanza serikali ipige marifuku hiki kitabu..
Tayari kitabu kiko sokoni kama vipi na nyie mifugo ya Magufuli andikeni kitabu cha kumpamba, simple!!!
 
Huo ni upambavu wa kiwango cha SGR na kuna mtu kawalipa.Waongee lingine, kwenye suala la miradi hapo wamechemka!
Reli ya SGR inaenda Chato?Mradi wa Umeme Rufiji upo Chato?Bandari kavu ya Kwala ipo Chato?Mradi Ujenzi wa mji Mkuu wa serikali upo Chato?Ujenzi wa vituo vya Afya zaidi ya 300 vipo Chato?Kijazi Flyover ipo Chato?Mfugale Flyover ipo Chato?Barabara ya njia nne Kimara mpaka Kibaha ipo Chato?
Kwa uchache,Waandishi wameongozwa na chuki zaidi ya uhalisia.
JK mwenyewe alipeleka umeme Kijiji cha Hoyoyo, Mkuranga ambapo hakuna mradi wowote bali Umeme alipata Mkwewe Baba yake na Salma na shambani kwa mkewe!
Ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo ambao alizindua mwaka 2014!
Inshort Kibanda na Ngurumo kama wamo humu jukwaani wajue wamejidharirisha akiwemo na Baba Askofu!.Ila Ngurumo nadhani stress za kukimbia nchi zinamsumbua!
Umekisoma kitabu? Umejua maudhui yake? Isije ikawa hujasoma kisha unabweka? Issue kubwa ni kwamba raisi alipendelea alikozaliwa siyo kwamba hakujenga miradi hapana. Alipendelea kwao bila idhini ya bunge. Soma I am the state
 
Imebidi nicheke sana, awe anakubalika sana huko mtaani, ila ikifika kwenye kipimo halisi cha kukubalika kwake ashindwe kuheshimu zoezi hilo! Hii ni kali ya mwaka.
Kwanza nani kasema kuwa hicho ndio kipimo halisi? Kwa hoja zipi? Yani usionekane kukubalika mtaani halafu utuambie et kipimo cha kukubalika ni kwenye uchaguzi?
 
Kumbe kweli alikuwa na mabaya, sasa kuna ubaya gani wa mtu kuandika mabaya yake tu? Nyie si mngejotikeza kuandika mazuri yake tu? Au ni hatua gani walichukuliwa waliokuwa wanaandika mazuri yake tu bila kuchanganya na hayo mabaya yake?
Ukiambiwa hao waliyokuwa wanaandika mazuri tu ni mashabiki zake au chawa waweke, je wewe unayeandika mabaya tu ni nani adui yake au unamchukia tu?
 
Wapumbavu badala ya ku deal na wizi wa sasa wa CAG wako Bize na marehemu tu ,naona group la ngurumo na meena hapo

USSR

Sent using Jamii Forums mobile app
Mpaka leo wapo watafiti wanamtafiti yesu je nao ni wapumbavu? Usije ukawa we ndo mpumbavu kiongozi? Ni mpumbavu sababu hutaki kusikia usiyopenda kusikia juu ya mpumbavu mwenzio jpm
 
Kwako ni mema, sisi tunaona ni wajibu wa serikali kupitia kodi za wananchi. Nenda Afrika kusini kama kuna mweusi yoyote anasema miundombinu iliyojengwa na makuburu ni wema. Usichanganye wema na wajibu. Angekuwa volunteer kisha afanye aliyofanya ungetamka neno wema.

Kama ni wajibu na mtu alitimiza wajibu kwanini uandikwe sasa!!!
Hao wazee mataahira wenye mashavu kama ngano za maandazi wametoa kitabu kinachokosoa wajibu uliotimizwa chato,as if chato hakuna watu wanaostahili kutimiziwa haki ya kuwa na miundombinu.

Jk huyo hapo kajenga kwao vizuri sana wamefunika makalio yao,ila jpm imekuwa nongwa,kwanini unafiki kiwango hiki kutokwa kwa watu wazima??

By the way sio tatizo,wacha wawauzie hicho kitabu mazezeta waliowalenga labda wameona fulsa ya kupigia vihela kadhaa kupitia jpm.
 
Bila ya Katiba Mpya yenye kujenga taasisi huru na kuziimarisha, vitabu vya namna hiyo hata viandikwe kila mwaka; ni bure kabisa
 
Aachwe apumzike! Kama serikali ya SSH itaendelea kuruhusu udhalilishaji huu dhidi ya kiongozi mkuu wa nchi mzalendo aliyetangulia mbele za haki basi wajue wanawakwaza watu wengi sana.
Nadhani tufike mahali tuwe objective. Tukisome kitabu kisha tukichambue na kuona ninkwa kiasi gani kinawasilisha ukweli au vinginevyo. Tutaju ni kwa kiasi gani "I am the State" kinauzugumzia uzalendo wa mwendazake.
 
  • Mswahili hajawahi kudhibitiwa kwa 'kunangwa', ingekuwa 'kumchamba' mswahili kunasaidia; ripoti za CAG zingetosha.
  • Kwa sasa vijiweni kuna malalamiko kuhusu Zenji kupendelewa kwenye mgao wa mikopo. Je tutarajie kitabu?
 
Back
Top Bottom