FT: Azam FC 1-0 Simba SC | NBC League, 28/10/2022

FT: Azam FC 1-0 Simba SC | NBC League, 28/10/2022

Nibandika bandua leo katika uwanja wa Benjamin Mkapa, pale miamba ya soka Afrika mnyama mkali mwituni wekundu wa msimbazi, watakapo karibishwa na matajiri wa Azam FC katika kuwania pointi 3 muhimu ili kujiweka vizuri kwenye msimamo wa ligi kuu!

Mara baada ya mnyama kutoshana nguvu na mtani wake wa jadi jumapili iliyopita na azam kukung'utwa 2-1 na KMc, leo watapata nafasi ya kujiuliza,
ngoma ni saa 1 kamili jioni hii!

Wanalunyasi karibuni, mwana kulitaka mwana kulipewa.

Nguvu moja.

=======

01' Mpira umeanza Benjamin Mkapa

08' Ayoub Lyanga anajaribu kutoka nje ya 18 lakini mpira unapaa juu ya lango la Simba

13' Kyombooooo, anakosa bao baada ya pasi nzuri kutoka kwa Okra

17' Azam wanafika kwenye lango la Simba, Kona. Simba wanasimama imara na kona haina madhara.

22' Simba wanacheza pasi nyingi kuelekea lango la azam, mikono ya Ahmada inawaokoa Azam.

23' Onyango anamdhibiti barabara mshambuliaji wa Azam, Prince Dube na kushindwa kufika kwenye lango la Simba akiwa na mpira.

31' Dube anapiga off target akiwa yeye na Manula

33' Azam wanapiga pasi za mipenyezo, Manula ana-slide na kuokoa jahazi

34' ⚽ Prince Dubeeeeee, bao safi na maridadi kutoka pembeni.. Manula anashindwa kufikia na kuzama nyavuni

39' Kipree, anajaribu mpira unatoka nje ya lango

42' Dube anapiga kichwa na mpira unapaa juu ya lango la Simba

44' Azam wanapoteza mpira, Kyombo anaunasa lakini anapiga fyongo

45+1' Half time
Huyo Habibu mmempromote weee... cha ajabu anacheza fyongo!
 
Nibandika bandua leo katika uwanja wa Benjamin Mkapa, pale miamba ya soka Afrika mnyama mkali mwituni wekundu wa msimbazi, watakapo karibishwa na matajiri wa Azam FC katika kuwania pointi 3 muhimu ili kujiweka vizuri kwenye msimamo wa ligi kuu!

Mara baada ya mnyama kutoshana nguvu na mtani wake wa jadi jumapili iliyopita na azam kukung'utwa 2-1 na KMc, leo watapata nafasi ya kujiuliza,
ngoma ni saa 1 kamili jioni hii!

Wanalunyasi karibuni, mwana kulitaka mwana kulipewa.

Nguvu moja.

=======

01' Mpira umeanza Benjamin Mkapa

08' Ayoub Lyanga anajaribu kutoka nje ya 18 lakini mpira unapaa juu ya lango la Simba

13' Kyombooooo, anakosa bao baada ya pasi nzuri kutoka kwa Okra

17' Azam wanafika kwenye lango la Simba, Kona. Simba wanasimama imara na kona haina madhara.

22' Simba wanacheza pasi nyingi kuelekea lango la azam, mikono ya Ahmada inawaokoa Azam.

23' Onyango anamdhibiti barabara mshambuliaji wa Azam, Prince Dube na kushindwa kufika kwenye lango la Simba akiwa na mpira.

31' Dube anapiga off target akiwa yeye na Manula

33' Azam wanapiga pasi za mipenyezo, Manula ana-slide na kuokoa jahazi

34' ⚽ Prince Dubeeeeee, bao safi na maridadi kutoka pembeni.. Manula anashindwa kufikia na kuzama nyavuni

39' Kipree, anajaribu mpira unatoka nje ya lango

42' Dube anapiga kichwa na mpira unapaa juu ya lango la Simba

44' Azam wanapoteza mpira, Kyombo anaunasa lakini anapiga fyongo

45+1' Half time
Ohoooo,Guardiola mnene amekalia kuti kavu. Kesho tu anarushiwa virago.
 
Banda, na sakho ni mauchafu unanua bech best warmer [emoji16]
 
All in all, kikosi cha Simba cha leo kina utani mwingi sana. Kumchezesha Mkude, Nyoni, Kapama kwa pamoja nu kutujaribu wana Simba. Azam ni very energetic club, wana kasi na uwezo wa kumiliki mpira. Wanaoweza kucheza mechi hizo ni akina Banda, Sakho, Okwa, Okrah. Kwa vyovyote vile Nyoni hawezi kumzuia prince dube hata kwa uchawi.
 
😅😅😅🤣 eti kyombo ndio mchezaji wa daraja la juu Tanzania.
 
All in all, kikosi cha Simba cha leo kina utani mwingi sana. Kumchezesha Mkude, Nyoni, Kapama kwa pamoja nu kutujaribu wana Simba. Azam ni very energetic club, wana kasi na uwezo wa kumiliki mpira. Wanaoweza kucheza mechi hizo ni akina Banda, Sakho, Okwa, Okrah. Kwa vyovyote vile Nyoni hawezi kumzuia prince dube hata kwa uchawi.
Wakati mnawanunua kwa mbwembwe na kuwatambulisha simba day hamkujua ni takataka?
 
Back
Top Bottom