Mtoto halali na hela
JF-Expert Member
- Aug 10, 2012
- 52,160
- 48,974
Eeh"DaimaMbeleNyumaMwiko"
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Eeh"DaimaMbeleNyumaMwiko"
Dodoma Jiji 2 yanga 1Ratiba ya Ligi Kuu ya NBC, leo Jumapili Mei 15, 2022, Yanga watakuwa ugenini kwenye Uwanja wa Jamhuri kucheza dhidi ya Dodoma Jiji FC Mkoani Dodoma.
Ikumbukwe kuwa Yanga haijapata bao hata moja katika mechi tatu zilizopita mfululizo katika Ligi Kuu Bara, presha kubwa ipo pia kwa mshambuliaji wao Fiston Mayele ambaye ameshafung mabao 12 hadi sasa akiwa mmoja wa vinara wa mabao msimu huu.
Kikosi cha Yanga kinachoanza katika mchezo wa leo Mei 15, 2022
KOCHA YANGA AFUNGUKA
Kocha Msaidizi wa Yanga, Cedric Kaze amesema kucheza mechi mfululizo ndani ya muda mfupi, kulifanya wachezaji wawe na uchovu, lakini suala la ubingwa lipo mikononi mwao, kilichobaki ni wao kukamilisha michezo licha ya kutoshinda mechi tatu mfululizo.
Kuhusu Mayele amesema kukosa penati ni bahati mbaya hata wachezaji wakubwa wanakosa, akizungumzia kikosi kuwa na mabadiliko katika mchezo wa leo amesema imetokana na uchovu wa baadhi ya wachezaji ili miili yao ikae vizuri, na wana imani kuwa wakiingia kutokea benchi inaweza kuwasaidia.
NENO LA DODOMA JIJI
Kocha Msaidizi wa Dodoma Jiji, Mohamed Muya amesema wanaiheshimu Yanga lakini wanaingia uwanjani kwa ajili ya kupambana.
Kuhusu kukabiliana na Mayele ambye amekuwa hatari msimu huu amesema Yanga wana wachezaji wazuri, hivyo mipango yao siyo kumdhibiti Mayele pekee bali wachezaji wote.
----------------
Timu zinaendelea kupasha misuli.
Timu zimeshaingia uwanjani, mashabiki ni wengi uwanjani, mchezo unaweza kuanza muda wowote kuanzia sasa.
Mchezo umeanza
1' Mchezo umeanza na Dodoma Jiji FC wanatoa mpira nje.
2' Yanga wanapata kona, inapigwa lakini walinzi wa Dodoma wanaokoa
4' Mchezo bado haujashika kasi, timu zote ni kama zinazomana.
6' Dodoma wanafanya shambulizi kali lakini walini na kipa wa Yanga wanakuwa makini kuondoa hatari
10' Kasi ya mchezo inaanza kuongezeka pande zote zinaongeza kasi
Hahaha haiwezekaniDodoma Jiji 2 yanga 1
Goli la wiki hiliWhat a goal!!
Marengo si mabaya sema hayakutimiaAmbundo kafanya kitu kizuri sana. Wengine wanapata nafasi, wanataka wamtafute Mayele
Naona mapema tu mmejiokotea dodo lenu.Hahahaaa. Lol.
Hii game yetu leo. Huo ubingwa kukufuata hilo sahau Mtani.
Kweli kabisa. Maana walishaanza kuchonga ngenga.Leo Tunataka Tuwakumbushe Watu Flani Hivi Jambo..
Wanachonga Sana MkuuKweli kabisa. Maana walishaanza kuchonga ngenga.
Kwa hili goli sina hata haja ya kuongezwa mshahara mwezi july kwa kweli. 😂😂😂😂What a goal!!
Kawaida saana. 😅Naona mapema tu mmejiokotea dodo lenu.
Ilikuwa mbaya sana sema mchezaji nae hakuwa makiniKibwana kampa assist mchezaji wa Dodoma