FT: Ihefu SC 2-1 Young Africans SC | NBC Premier League | Highland Estates | 04/10/2023

...binafsi nilipoona ile rotation ya wachezaji 8 nikajua tu ushindi leo droo,kocha kapata kitu cha kujifunza
Tumekuwa tukimpongeza kocha kwa kufanya rotation katika kikosi na kujisifu kuwa tuna vikosi vitatu. Iweje leo utilie shaka? Tusiwe wanafiki, soka ni magoli, na magoli ndio yanayoamua ushindi, sare au kupoteza
 
Nimesikitika Sana...... Lawama kupewa Diarra eti Magoli Yote asingefungwa..Ufupi Umeigharimu timu...!

Watu wanasahau Mapema ,Kimo hiki hiki ndo kilituvusha mechi Dhidi ya Marumo na Zalani....!

Tuwe Watu wa shukurani na fadhila jama..!
Shabiki hajawahi kuwa mtu wa shukurani na fadhila, sikuzote yeye anataka mchezaji ampe matokeo chanya ambayo hayatamuumiza kihisia.

Shinda mechi 50 kwa kiwango kikubwa ila ukiharibu moja ni lazima walalamike tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…