FT: Ligi Kuu: Yanga S.C 1-0 Ruvu Shooting: Uwanja wa Mkapa, 23/01/2023

FT: Ligi Kuu: Yanga S.C 1-0 Ruvu Shooting: Uwanja wa Mkapa, 23/01/2023

Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya Nbc na mabingwa wa muda wote nchini Tanzania[emoji1241] Young Africans S.C[emoji617] almaarufu Yanga leo tena wanashuka dimbani kukabiliana na maafande wa Ruvu shooting katika mwendelezo wa ligi kuu ya Nbc...

Mchezo huo utakuwa mgumu Kwa timu zote kwani Yanga[emoji617][emoji617] wanataka kushinda ili kuzidi kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi ya Nbc huku Ruvu shooting[emoji1949][emoji1949] nao wakiitaji alama zote tatu ili kujinasua kutoka mkiani mwa ligi.

Mchezo huu utapigwa kunako dimba [emoji2522] la Benjamini Mkapa mnamo saa1.00 usiku

Je ni Wananchi[emoji617][emoji617] au Mafande[emoji1949][emoji1949] ndio watakao ondoka na kicheko[emoji1][emoji1] baada ya dakika 90?? Kuwa nami mwanzo paka mwisho wa kipute

"" Wachezaji wa timu zote mbili wapo uwanjani[emoji2522] wakipasha misuli[emoji1732][emoji3571][emoji125]ili kujiweka sawa[emoji91][emoji91]

'''""""""""'''''"""""''""”"”""""""'"""""""""

00" Kipenga Cha mwamuzi kimepulizwa kuashiria Mpira[emoji460][emoji460] umeanza hapa kadika Dimba[emoji2522] la Benjamini Mkapa katika

02" Hatari langoni mwa Yanga [emoji617] ila mpira unaenda nje inakuwa ni goal kick

05" Ruvu shooting [emoji1949][emoji1949] wameanza vizuri mchezo wa leo huku utulivu ukiwa mkubwa

10" Kennedy Musonda yupo chini akipatiwa matibabu baada ya kugongana na goalkeeper wa Ruvu shooting

15" Mayele anaachia shuti kali lakini linapanguliwa na Mlinda mlango wa Ruvu shooting inakuwa Kona ambayo haikuzaa matunda

25" Bado milango ni migumu kwa timu zote

32" Gooooal[emoji460] Yanga [emoji617] wanatangulia Kwa bao Moja baada ya beki Mpoki Mwakinyuke kujifunga

40" Mayeleeeee....... Golikipa wa Ruvu anaokoa inakuwa ni kona. Hii ni Kona ya 5 Kwa Yanga wakati Ruvu hawajapa kona paka sasa

42" Moloko anapaisha akiwa kwenye nafasi nzuri ya kufunga. What a miss!

45" Shambulizi lingine langoni mwa Ruvu shooting lakini mpira unakwenda nje.

HT" Naaam ni mapumziko katika uwanja[emoji2522] wa Benjamin Mkapa Wananchi [emoji617] wakiongoza kwa bao 1-0 dhidi ya Ruvu shooting.
Tukutane kipindi cha pili

View attachment 2493095View attachment 2493096
Hodi hapa.........
 
Wale wasema kweli nipeni abc ya first half,maana sijaangalia kabisa ila sekandi hafu nipo...........Sina points za kutetea timu yangu first hafu,naomba wale wapinzani mnipe abcd Scars OKW BOBAN SUNZU kama mmeona game 😀😀
 
Japo Yanga wanaongoza ila Leo hawana mchezo mzuri kama tuliouzoea
Ni kweli walichelewa kuchanganya. Wameanza kuchanganya dakika 15 za mwisho. Mpira waliocheza dakika za mwishoni ndio wangeanza napo ingekuwa habari tofauti mpaka sasa
 
Back
Top Bottom