Kwenye makaratasi Yanga Bingwa itashinda 3, ila uwanjani, kwa Simba , wale pale jukwaani Dada zangu mmoja wa Mombasa na huyu akaa Upanga kwa nyuma itapata droo. Nani kaelewa? Haya nyoosha kidole juu!!
Swali fikirishi, hivi tukikaa saa 11 kucheki boli kwa Mkapa nani watakuwa na hofu ya makonzi, ni Yanga au Simba??
Yanga ina masifa sana, inakera mno, kazi kuonea tu wenzake hii si haki, makolo kila siku ni simanzi na kilio, na leo kilio kitaendelea mpaka kipara aachie mikoba, eti amesema kichapo kitalingana na mzuka wa mbumbumbu, mzuka mkubwa kujidai kupambana na kushambulia kwa nguvu, basi khamsa zitawahusu!! Gamondi noma sana, ni katili mno!!
Leo namuona Duke Abuya akishine, ni Duke Abuya day for me!!
Hii ni Maalum kwa wachezaji wa Yanga tu: Hakikisheni mnafunga mbumbumbu magoli mawili katika dakika 30 za kipindi cha kwanza, mpira ukianza tu shambulieni kama vichaa mpaka makolo wapoteane kwa kufungwa goli 2 safi, Yanga mkiruhusu kushambuliwa mwanzoni makolo watapata goli moja na moto utawawakia uto tutapigwa 3. Enyi wachezaji msijesema sikuwaambia, hatutaki lawama tunataka ushindi tu.