FT: Simba 1-0 De Agosto (Agg 4-1) | Simba yatinga hatua ya Makundi Ligi ya Mabingwa Afrika

FT: Simba 1-0 De Agosto (Agg 4-1) | Simba yatinga hatua ya Makundi Ligi ya Mabingwa Afrika

Execute

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2022
Posts
3,000
Reaction score
7,336
Ni siku iliyokuwa inasubiriwa kwa hamu sana na mashabiki hapa Tanzania, kule Angola na Afrika Mashariki kwa ujumla.

Mnyama mkali anashuka dimbani akiwa na kumbukumbu ya ushindi wa mabao matatu kwa moja ugenini.

Anaenda kumaliza ngwe na kuingia hatua ya makundi kwenye Ligi ya Mabingwa wa Afrika.

Tutakuwa hapa tukipeana taarifa mubashara. Mechi itaanza saa kumi kamili Alasiri.

Kikosi cha mnyama mkali

=======

01' Kipenga kinapulizwa kuashiria mwanzo wa mchezo dimba la Benjamin Mkapa.

03' Moses Phiri anafika lango la De Agosto lakini anadondoka mwenyewe.

07' Simba wanacheza pasi fupi nyingi ndani ya nusu yake.

12' Simba wapata kona ya kwanza ya mchezo, kichwa cha Inonga kinapaa juu ya goli.

13' 🟡Many Rashid wa De Agosto analamba kadi ya kwanza ya njano baada ya kumdondosha Okra akielekea langoni.

20' Mpira uko chini zikiwa ni pasi maridadi kutoka kwa timu zote mbili.

21' Simba wanapata kona ya pili ambayo inashindwa kuleta mabadiliko kwenye ubao.

25' Sakho anapunguza watu na kuingia mwenyewe, beki wa De Agusto anapangua mipango.

30' Phiri na Okrah wanajaribu langoni mwa De Agusto, gonga yao inazaa kona ya tatu kwa Simba bila ya matokeo.

32' 🟡 Kadi ya njano kwa Venancio baada ya kumvuta shati Chama.

33' ⚽Moses Phiri anaiandikia Simba bao la kwanza, pasi safi kutoka kwa Zimbwe Junior aliepokea mpira kutoka katikati ya uwanja.

43' Onyango anauza mpira, free kick kuelekea Simba. Free kick ya De Agosto inagonga ukuta.

45+2' Mpira mapumziko.

=====


50' Okra anajaribu kuwapita walinzi wa De Agosto lakini anapiga njeeeeee.

51' Venancio anapewa onyo kali baada ya kumzuia Kanoute kwenye njia, Venancio tayari ana kadi ya njano.

58' Simba wanamiliki mpira kwa kiasi kikubwa katikati ya dimba huku wakijaribu kufika kwenye lango la De Agosto mara chahce.

59' Faulo ya tisa kwa De Agosto, Mzamiru yuko chini.

63' Simba inapoteza mpira baada ya kujaribu kona fupi, mpira wa kurusha kuelekea Simba.

64' Chama anafanya udambwi na kumpita mlinda Mlango wa De Agosto, pasi inashindwa kimfikia Moses Phiri.

65' Phiri anapata nafasi nyingine na kuachia mkwaju mkali, kipa anapangua. Kona.

68' 🔁 Kibu Deniss anaingia kuchukua nafasi ya Sakho.

72' 🟡 Antonia Silva anapewa kadi ya njano kwa kumchezea ndivyo sivyo Okra.

77' 🔁Habib Kyombo anaingia kuchukua nafasi ya Okrah aliyeumia.

78' 🔁 Zimbwe JR nae anaenda bench na nafasi yake inachukuliwa na Gadiel Michael Mbaga.

87' Gadiel anapewa kadi ya njano baada ya kuvuta bukta ya mchezaji De Agusto.

89' Manula anaingia mwenyewe mpaka katikati ya uwanja.

90' Dakika tatu zinaongezwa kuhitimisha mpambano.

90+1' Nyoni na Mkude wanaingia, Israel Mwenda anaenda bench.

90+3' Mpira unatamatika dimba la Benjamin Mkapa na Simba wanasonga mbele kwenda hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika kwa jumla ya mabao 4-1 dhidi ya De Agosto.

Screenshot_20221016-154243.jpg
 
Ni siku iliyokuwa inasubiriwa kwa hamu sana na mashabiki hapa Tanzania, kule Angola na Afrika Mashariki kwa ujumla.

Mnyama mkali anashuka dimbani akiwa na kumbukumbu ya ushindi wa mabao matatu kwa moja ugenini.

Anaenda kumaliza ngwe na kuingia hatua ya makundi kwenye ligi ya mabingwa wa Afrika.

Tutakuwa hapa tukipeana taarifa mubashara. Mechi itaanza saa kumi kamili alasiri.
Shukran Sana mkuu
 
Leo hata kama ikitokea Simba amefungwa, lakini kwa kipindi tangua ashinde Angola nyoyo za waTanzania zilikuwa tuli tulia.

Hakuna msongo, huenda gramu chache za uzito ziliongezeka.

Sasa fikiria kinyume chake, mashaka tu na kuota ndoto za majinamizi.

Ni utani jamani, nchi nzuri sana hii.
 
Prediction yangu mapema sana.

1. Aishi Manura.
2.Islael Mwenda.
3. Mohamed Hussein.
4. Onyango Achieng.
5 Enok Enonga.
6. Jonas Mkude.
7. Osmane SACKO.
8. Sadio kanute.
9. Moses Philiph.
10. Clotus Chama.
11.Okra

Ila hiki kikosi hata robo fainali kufika ni kwa shida Sana.

Desember watafute majembe ma Tano tu 5.

1. Beki wa kati 1. Waachane na ottara futi 6
2. Beki mwenye uwezo wa 2/3.
3. Kiungo 6. Futi 6 CDM. Akpan ni 8.
4.Bado 8 Pana shida.
5. Washambuliaji 9.wawili futi 6

Pigs chini hao
Sako.
Banda.
Akpan.
Okwa.
Ottara.
Dejan.

Wakizingatia Huu ushauri Nusu fainali wanafika.
 
Leo hata kama ikitokea Simba amefungwa, lakini kwa kipindi tangua ashinde Angola nyoyo za waTanzania zilikuwa tuli tulia.

Hakuna msongo, huenda gramu chache za uzito ziliongezeka.

Sasa fikiria kinyume chake, mashaka tu na kuota ndoto za majinamizi.

Ni utani jamani, nchi nzuri sana hii.
Simba ni kama alishapita kwasababu agosto wanatakiwa kupata magoli matatu huku wakizuia mnyama asifunge hata moja. Hii ni impossible situation.
 
Prediction yangu mapema sana.

1. Aishi Manura.
2.Islael Mwenda.
3. Mohamed Hussein.
4. Onyango Achieng.
5 Enok Enonga.
6. Jonas Mkude.
7. Osmane SACKO.
8. Sadio kanute.
9. Moses Philiph.
10. Clotus Chama.
11.Okra

Ila hiki kikosi hata robo fainali kufika ni kwa shida Sana.

Desember watafute majembe ma Tano tu 5.

1. Beki wa kati 1. Waachane na ottara futi 6
2. Beki mwenye uwezo wa 2/3.
3. Kiungo 6. Futi 6 CDM. Akpan ni 8.
4.Bado 8 Pana shida.
5. Washambuliaji 9.wawili futi 6

Pigs chini hao
Sako.
Banda.
Akpan.
Okwa.
Ottara.
Dejan.

Wakizingatia Huu ushauri Nusu fainali wanafika.
Duuuuuuh Sasa mkuu mchezaji gani ambae utampata Africa hii Kati ya hao uliowataja wasiwe wamecheza champions league?? Au confederation???
 
Prediction yangu mapema sana.

1. Aishi Manura.
2.Islael Mwenda.
3. Mohamed Hussein.
4. Onyango Achieng.
5 Enok Enonga.
6. Jonas Mkude.
7. Osmane SACKO.
8. Sadio kanute.
9. Moses Philiph.
10. Clotus Chama.
11.Okra

Ila hiki kikosi hata robo fainali kufika ni kwa shida Sana.

Desember watafute majembe ma Tano tu 5.

1. Beki wa kati 1. Waachane na ottara futi 6
2. Beki mwenye uwezo wa 2/3.
3. Kiungo 6. Futi 6 CDM. Akpan ni 8.
4.Bado 8 Pana shida.
5. Washambuliaji 9.wawili futi 6

Pigs chini hao
Sako.
Banda.
Akpan.
Okwa.
Ottara.
Dejan.

Wakizingatia Huu ushauri Nusu fainali wanafika.
Kama huyo moses philip ni mchezaji wa Simba basi kweli hicho kikosi hakiwezi kufika mahali. Bora wamrudishe Moses Phiri waachane na huyo Philips
 
Prediction yangu mapema sana.

1. Aishi Manura.
2.Islael Mwenda.
3. Mohamed Hussein.
4. Onyango Achieng.
5 Enok Enonga.
6. Jonas Mkude.
7. Osmane SACKO.
8. Sadio kanute.
9. Moses Philiph.
10. Clotus Chama.
11.Okra

Ila hiki kikosi hata robo fainali kufika ni kwa shida Sana.

Desember watafute majembe ma Tano tu 5.

1. Beki wa kati 1. Waachane na ottara futi 6
2. Beki mwenye uwezo wa 2/3.
3. Kiungo 6. Futi 6 CDM. Akpan ni 8.
4.Bado 8 Pana shida.
5. Washambuliaji 9.wawili futi 6

Pigs chini hao
Sako.
Banda.
Akpan.
Okwa.
Ottara.
Dejan.

Wakizingatia Huu ushauri Nusu fainali wanafika.
Yaani acha tu ase, ngoja tuone
 
Kila la heri mnyama hao wengine lolote liwakute[emoji1787][emoji23][emoji23]
 
16 October 2022
Benjamin Mpaka Stadium
Dar es Salaam, Tanzania

CAFCL MATCH :
Simba SC vs Clube Desportivo 1º de Agosto



Historia ya Clube 1º de Agosto ambayo imejenga kijiji cha michezo (Complex) ikiongozwa na kiongozi mwenye visheni General Carlos Alberto Hendrick Vaal da Silva. Kwa hapa Tanzania kwa mbali timu ya Azam FC timu ya mpira wa miguu imewekeza Azam Chamazi Complex centre katika jiji la Dar es Salaam .

Imewekeza katika uwanja waliopa jina General França Ndalu football stadium, viwanja vidogo vya soka na mpira wa mikono, academy za bweni, Jumba la maonyesho lilikatiwa jina la mchezaji wa zamani Paulo Bunze nyota wa mpira wa mikono / handball.

Uwekezaji huo endelevu tayari umeanza kuonesha matunda yake . Klabu hiyo ya michezo ilianzishwa tarehe 1 Agosti 1977 ipo chini ya usimamizi wa jeshi la nchi ya Angola.

Mradi mkubwa wa 'kijiji' cha Clube Desportivo 1º de Agosto wazaa matunda ya kwanza ya uwekezaji wake

Source : Adão Faustino Augusto

Contrary to other national clubs, 1º de Agosto Led by General Carlos Hendrick, who is already in his second term as Chairman of the Board of Directors of Clube 1º de Agosto, as promised, investments in the construction of new infrastructures in the Sports City, namely the boarding school, the General França Ndalu football stadium and the multipurpose pavilion that will be named after the late handball player Paulo Bunze.
They have already begun to bear fruit
 
Back
Top Bottom