FT: Simba SC 1-0 Ihefu FC | Ligi Kuu Bara | Stade de Benjamin Mkapa 12/11/2022

Kama kweli unatazama mechi za Simba vizuri kabisa na unaujua mpira sidhani kama utamlaumu kocha, kazi yake anaifanya vizuri kwa 100%. Changamoto pale ni eneo la mwisho kwenye ufungaji hakuna utulivu na wote wanaopewa nafasi ya kucheza pale mbele hawajafit kabisa. Ukitaka kumlaumu Mgunda jiulize kwanza timu aliikuta katika hali gani na je wale wachezaji yeye ndio alipendekeza wasajiliwe?!!
 
Nilikuwa napiga stori na shabiki mmoja wa Simba anasema hii timu Mungda imemshinda

Hapo ni baada ya kupata sare na Singida

Nikamuambia nipe sababu, akasema kwanza jinsi anavyomuona tu ni kama hana Quality ya kuhudumu kwenye timu kubwa kama ile

Nikamuuliza kwa hiyo hadhi ya Mgunda ndio sababu ya kupata sare ya leo?

Nikamuambia ile mechi dakika za mwanzoni Simba ilicheza hovyo na mimi sikupendezewa kuona namna jinsi wachezaji hawajitumi kwa asilimia zote

Na kosa lililofanyika mpaka kupelekea Singida wapate bao la kuongoza, lilitokana na Enonga kufanya uzembe wa kucheza na mpira

Sasa hapo Mgunda anahusika vipi?

Haya kipindi cha pili Simba ilipiga mpira mwingi tukatengeneza nafasi nyingi lakini mwisho wa siku Kibu alikosa magoli zaidi ya matatu, hapo utamlaumu Mgunda kwa lipi?
 
Hata ukirejea kutazama baadh ya mechi mfano vs Yanga, Azam, hao Singida na hata Mtibwa pamoja na kuwa walifungwa goli 5 lakini nafasi nyingi za kufunga magoli zilitengenezwa kwenye mechi zote hizo lakini washambulizi wanakosa umakini kabisa.. hii sio shida ya Mgunda amemuamini na kumpa nafasi kila mchezaji pale.. Wakati wake wa kulaumiwa apewe timu asajili silaha zake za maangamizi ashindwe ndio tuje kumlaumu hapa..
 
Hili niliwahi kulizungumza hadi kwa mashabiki wa Yanga ambao walikuwa wanaona ule mfululizo wa kutoa sare kwenye mechi za kimataifa shida ni kocha

Niliwakumbusha kuwa katika mechi yao na Zalan, Mayele alikosa magoli mengi ya wazi katika kipindi cha kwanza.

Lakini mechi ilivyomalizika kwa kufunga hattrick hakuna yeyote aliyeongelea zile nafasi alizokuwa anakosa kwasababu matokeo ya mwisho ni Yanga kashinda

Mechi waliotoa sare na Al Hilal bado Mayele alikuwa anakosa mabao ya wazi lakini, walipopata sare mashabiki walihamishia hasira zao kwa kocha

Wakati kilichokuwa kinaonekana uwanjani ni spirit ya wachezaji kwenye kujituma na kuipambania timu ilikuwa very low

Ukiwa na uongozi wenye watu wa mawazo kama haya ya mashabiki basi hatuwezi kufika mbali kwasbabu kila mechi tutayopoteza basi tutakuwa tunakazi ya kubadilisha makocha
 
Na bahati mbaya viongozi wengi wa hizi timu wana mawazo ya kishabiki kama hayo na ndio mana mpira wetu unapata tabu sana kusonga mbele. Leo huko duniani Man City kapigwa na kumuacha Arsenal kubaki kileleni na watu wenye weledi na taaluma zao huwaoni wakitapatapa tazama hapa sasa Simba imeshinda leo kwenye mechi ngumu sana anatoka mtu anamlaumu kocha mara ooh timu inashika mkia tunashindaje goli moja sijui mara wametusumbua wanashindwa kuelewa hii ndio football.
 
japo simba imeshinda lakini bado inaitaji marekebisho mengi sana
 
japo simba imeshinda lakini bado inaitaji marekebisho mengi sana
Viongozi wapo hadhiri (wanakusikia). Sehemu gani kwa mtazamo wako ambayo unaona pafanyiwe marekebisho..! Nguvu Moja [emoji881]
 
Viongozi wapo hadhiri (wanakusikia). Sehemu gani kwa mtazamo wako ambayo unaona pafanyiwe marekebisho..! Nguvu Moja [emoji881]
Sasa hivi tuna majeruhi wengi karibu I kila mechi tuna majeruhi hatuna kocha wa mazoezi hii inaweza kuwa sababu inayochangia
 
Mnapoint zetu tatu mzunguko ujao msipo sajiri January
 
Sasa hivi tuna majeruhi wengi karibu I kila mechi tuna majeruhi hatuna kocha wa mazoezi hii inaweza kuwa sababu inayochangia
Kuna mambo Simba SC wanatakiwa kupambana kwa haraka na si kuchelewa kufanya hasa kuhusu haya ya Kocha wa mazoezi na Kocha wa makipa.

Okrah amerudi game ya Jana baada ya kutoka kwenye majeraha. Mchezo uliopita Peter Banda licha ya kufunga bao ameliumia. Jana Sakho ameumia na wapo wengine akina Okwa, Jimmy, Israel.

Na bado tunasisitiza kwa Viongozi Usajili unaofuata dirishani dogo uwe wa kiwango.
 
Tusisingizie kuwa tatizo ni kocha wa viungo

Simba haina kocha atayetusaidia.
Hawa waliopo wanabahatisha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…