Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 9,189
- 16,128
saa ngapi mechi?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Pamoja ya kuwa umetumia font mbovu, kila la heri kwa Mnyama leo🦁🦁🦁Naaam, wasalam wakuu,
Ile siku maalumu iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu hatimaye imefika. Pambano lenye hadhi la watani wa jadi katika soka la bongo, Yanga na Simba.
Karibuni katika matukio mubashara (live updates) ya mtanange huu wa kukata na shoka baina ya mahasimu wa soka la Bongo #KariakooDerby Yanga na Simba, utakaochezwa saa 11 jioni Estadio De Benjamin Mkapa leo jumapili 23-10-2022.
Huu ni mchezo wa namba 64 wa Ligi Kuu ya NBC 2022/2023, Yanga akiwa ni mwenyeji wa mchezo wa leo dhidi ya mtani Simba.
Mchezo uliyopita wa Ligi Kuu msimu wa 2021/2022 uliochezwa April 30, 2022, timu hizi zilitoshana au kuchoshana nguvu kwa sare ya bila kufungana/suluhu ya 0-0. Kwa maana hiyo huu ni mchezo wa mzunguko wa kwanza kwenye msimu wa 2022/2023.
Timu hizo zinaingia uwanjani zikiwa na alama 13 kila moja, lakini Simba ipo kileleni kutokana na wingi wa mabao ya kufunga na kufungwa dhidi ya Yanga ambayo inashika nafasi ya pili, kila moja amecheza mechi tano.
Pia michezo mingine (Derby) ya hivi karibuni ni ule wa Mei 28, 2022 kwenye nusu fainali ya Azam Sports Federation Cup ambapo, Simba alifungwa goli moja bila majibu, ambapo shuti kali la Feisal Salum ‘Fei Toto’ liliwalaza na viatu mashabiki wa Simba siku hiyo.
Vilevile mnamo Agosti 13, 2022 kwenye mechi ya ngao ya Hisani, Simba alitepeta tena kwa Yanga kwa kufungwa goli 2 kwa moja. Fiston Mayele "Mzee wa kutetema" akiingia kambani mara mbili siku hiyo na mashabiki wa Simba wakitoka vichwa chini.
Kwa miaka ya karibuni Simba imekuwa ikishindwa kupata ushindi mbele ya Yanga katika michezo ya Ligi Kuu Bara kwani mara yao ya mwisho kushinda ilikuwa bao 1-0, Februari 16, 2019 lililofungwa na mshambuliaji, Meddie Kagere.
Kwenye mechi za kimataifa, tarehe 16/10/2022 Yanga imetolewa kwenye michuano ya CAF CL na Al Hilal baada ya kufungwa 1-0 na kushukia kwenye michuano ya CAF CC ambapo pia amepangiwa Club Africain kwenye mchezo wa Play off kuelekea makundi.
Pia Simba mechi ya mwisho kimataifa imetoka kupata ushindi wa 1-0 dhidi ya Primeiro De Agosto ya Angola na hivyo kufuzu hatua ya makundi ya CAF CL.
Je, leo itakuwaje baina ya miamba hii miwili? Nani ataibuka kidedea? kaa nami hapa mwanzo, kati na mwisho kupata kila kinachojiri kutoka katika dimba hili lenye kumbukumbu nzuri ya Hayati Benjamin Mkapa Dar es Salaam.
Azam Sports 1 HD wataurusha mpambano huu mubashara (live).
Je, "Watatetema" au "watapiga saluti?" Hahaha #𝑯𝒂𝒊𝒏𝒂𝑴𝒃𝒂𝑴𝒃𝒂𝑴𝒃𝒂
Unazeeka vibaya babu Watu8Mvua ikinyesha na jua linawaka (only old timers will understand this)
Sasa jiandae,kuiheshimu rekodi ya kutowafunga wananchi miaka 7 mfululizo huku ubingwa nao mkiukosa.😂WanaMsimbazi wenzetu OKW BOBAN SUNZU na Ghazwat Anzishe uzi live wa hii Mechi tunaenda kukumbushia KIPIGO CHA 2012, Utopolo afe Goli 5 bila.
Lazima wafukuzanee tuuuuuu
Kwani kuanzisha uzi pana zawadi wewe mnakufa hayo mambo ya kugombea uzi ni kama enzi za utoto wetu tulikua tunagombea Scania za Mwanamboka zikipita bara barani..113..Ukadhani kuashinza uzi ndio mtashinda? Utopolo subiri saa 1
Mkuu mbona kiherehere kama mtoto wa kike. Niliye mquote anaelewaKwani kuanzisha uzi pana zawadi wewe mnakufa hayo mambo ya kugombea uzi ni kama enzi za utoto wetu tulikua tunagombea Scania za Mwanamboka zikipita bara barani..113..
Vichwa vimeshachomolewa bado nyonga hahaaaChakula kitamu 3 -0View attachment 2395112
Kibongo bongo sidhani kama kuna App inayoonyesha game za hapaApp gani inaonesha hii mechi
Utopolo ni kumanuliwa tuMakolo Ni kichapo tuu