Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Miye nashindwa kuwaelewa mnaohusisha watu kama Lowasa, Mengi n.k juu ya suala hili eti wana malengo yao ya urais na vitalu vya respectively. Hivi ina maana Lowasa na Mengi waliwashauri watu hawa wapige hili deal????
Wizi umefanywa na wezi hawa kwa manufaa yao, kamati imefanya uchunguzi na repoti imesomwa bungeni na imedhihirika bila mashaka yoyote kuwa wezi hawa wamehusika katika wizi huu, Je Lowasa na Mengi wanaingiaje hapa???
Habari za jioni watanzania wenzangu!
Poleni na siku nzima ya leo ambayo kama taifa tumepitia wakati mgumu sanaaa!
Napenda kuwapongeza wale wote walioiibua hii kashfa ya escrow,pia pongezi ziende kwa kafulila kwan alisimama kkidete pale bungeni ili kudai pesa hizi zirudishwe! Kamati ya PAC pongezi nyingi sana mmefanya kazi nzito mbarikiwe na tumetambua mchango wenu! Kulinda ripoti kwa usiku mzima pale bungeni si kazi ndogo,kizazi cha wazalendo kitawakumbuka daima!
Mm binafsi nimesikitishwa sanaa na yote niliyoyasikia kutoka kwenye kamati ya PAC! Hivi kweli nchi hii ina uongozi wa kidemokrasia?kweli watu wanagawana pesa kama wanagawana peremende?hivi kweli watu wamekosa uzalendo kiasi hiki?nimetokwa na machozi kweli kabisa! Lkn mm najiuliza hivi kweli hakuna alielijua hili na kuchukua hatua mpaka lipigiwe kelele bungeni?nina maswali mengi mnoo lkn labda majibu yatapatikana kesho ripoti hii itakapojadiliwa bungeni!
Mm naomba kama taifa kuna haja ya kujua wajibu wetu! Na ni wakati muafaka wa viongozi woote kujitathmin kama kweli wanastahili kuendelea kushikilia nyadhifa zao!
Nataman kusema mengi lkn nina uchungu mnoo naona nitaandika hata yasiyofaa! Mm kama mwananchi mzalendo kabisa na ambae nataka kuhakikisha kuwa mafisadi hawaendelei kuitesa nchi yetu,basi naanza kuchukua hatua kwanza kwa kujiandikisha ili nichague kiongozi wangu wa serikali ya mtaa anaefaa,pia panapo majaliwa hapo mwakani nitaonyesha uzalendo wangu kwa kupiga kura kuwachagua viongozi wasio na chembe ya ufisadi! Tutaonana kwenye karatasi ya kupigia kura! Lkn pia nitakuwa mjumbe mwema wa kuwakataa wazi wazi mafisadi na wanyonyaji wa nchi yetu!
CHADEMA kaeni chini na Zitto mzungumze yaishe!!Makosa yake yanazungumzika mbona?
Kuivua nguo serikali kiasi hiki na kulinda ripoti yao isiibiwe usiku kucha sio jambo rahisi!!Zitto ni MWANAMAPINDUZI
Kauri zake ndo zimemponza. Viongozi wetu wanafanya kazi zao bora liende tu. Hawako makini. Unapokuwa umepewa ofisi kubwa hivyo inabidi kufanya kazi kwa weledi mkubwa.
Ripoti haijamtaja kuhusika kwa wizi huu moja kwa moja ila to be honest wizi wa namna hii unapotokea na mawaziri kugawana hela kwa kiwango hiki bila waziri mkuu na rais kujua ina maana hawastahili kuongoza nchi. Hawafai kabisa.
Tuwe wakweli ndugu zanguni.
Hawa viongozi wakubwa wa nchi hii WAMEHUSIKA KWA KIWANGO KIKUBWA. Nchi hii tunajua deal zinavyopigwa.
Hata rais alistahili kuwajibika tu ktk hili, ataendelea kuwepo ktk kiti chake kwa kuwa hakuna namna ya kumwajibisha. Ila ataongoza nchi hii kwa aibu kubwa.
Mnyika aliwahi kusema rais ni dhaifu na hili linathibitika kwa matukio kama haya. Serikali yake inaanguka kwa mara ya pili.Huu ni UDHAIFU na AIBU kubwa kwake na kwa familia yake lakini na kwa Watanzania kwa ujumla.
Mwl Nyerere akifufuka leo atatuadhibu Watanzania kwa kutokumsikiliza pale alipomkataa JK kuwa hawezi majukumu makubwa ya kitaifa.
Na tunataka kufanya kosa jingine kubwa maana watu wanaanza kumpigia chapuo Lowasa awe rais ajaye. Hili litakuwa kosa jingine la kitaifa.
WATANZANIA TUWE WASIKIVU.
hata ukitetea wameshajulikana hiyo tu inatosha, aliyekutwa na ngozi ndiye aliyekula nyama!una miaka mingapi na una uzoefu gani na siasa za nchini au nchi yeyote ile duniani?
Hivi kweli unafikiri hizo billioni 200 au 300 ndio hela kubwa zaidi kuibwa hapa nchini? Do you really think so?
Juzi tu hapa, tulizikia bodi ya gas ya serikali ilikula 30billion kwa masaa mawili tu kama matumizi ya mkutano wao mkuu, je click hapa unalikumbuka hilo? Umeliskia tena zaidi ya ile siku 1 tu? Unafahamu ni mabillion mangapi kwa siku yanaliwa bandari katika upitishaji wa mafuta haya tunayoweka kwenye magari yetu? Unafikir hili swala la hivyo vibillion vichache walivyopewa kiongozi ndio hela kubwa zenye walakini walishozo wahi pokea wakiwa madarakani?
Ndugu ni dhahiri uelewa wako wa the political syndicates and webs that run a country bado mdogo. Hii ishu haina utofauti na na sio kubwa in terms of amount ukiringanisha na ufisadi mwingine nchini. Swala ni kwamba hii ni vita ya mapapa wakubwa! Wazee wameingiliana maslahi ndio maana unaona hili. Hehehehe usidanganyike kirahisi kijana, japokua ni swala zuri lakini kwa asilimia 100 limesukumwa kisiasa!
Hivyo vilivyotolewa ni vijisenti tuuu? Mtu anapewa million 40 hadi bungeni anatajwa? Unakumbuka ile issue ya mkuu wa jeshi mwenye account yenye trillion 3 hapo south africa? Kama hujui google. Haya iliishia wapi?
Hii ni vita/boxing match ya heavy weights dogo. Wewe shangilia tu the show sababu tumelipia kiingilio kwa kodi zetu!
Ha ha ha utetezi WA kijinga kabisa kuwahi kutokea hapa jamiiforum hata hao maaskofu wakisoma watakucheka.Hivi kwanini Watanzania tunaangalia kila jambo kihasihasi? Maaskofu ni watu kama Sisi..kuna ushahidi gani kuwa walijua kuwa Fedha hizo sio Mali halali ya Rugemalila? Hivi kama Fedha hizo walizipokea kama mchango wake katika ujenzi wa shule au kabisa..kuna dhambi gani kwa maaskofu hao. I think tunayo moments bila kufikiri kwa akili.
Halafu tunasema Tanzania tuna rais kweli?
Kaingiziwa bila kujua
Pengo awawajibishe na kanisa liambiwe.....
Miaskofu nayo mijizi? Au zilikua za kuimarisha makanisa