Fundisho la Utatu haliingii akilini kabisa, mnaoamini mmetoa wapi mbona Biblia iko wazi kabisa?

Fundisho la Utatu haliingii akilini kabisa, mnaoamini mmetoa wapi mbona Biblia iko wazi kabisa?

Wewe unajua kusoma kwanza?

Mistari yote hiyo anza kupangua hoja za kupingana zilizotolewa moja baada ya nyingine.

Dhana ya Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote kuumba ulimwengu unaowezekana kuwa na mabaya, wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao hauruhusu mabaya ni contradiction.

Na contradiction hiyo hujaitatua.
Mimi najua kusoma, na vilevile najua kuamdika.

Rejea post # 314. Nimeeleza wazi kuwa hakuna migonano kwenye mistari hiyo. Kwa hiyo sina cha kupangua. Migonano unayoiona ipo kwenye akili yako mwenyewe sio katika biblia.
Je unaweza kuielezea hiyo migongano uliyoitaja?
Kwa nini unasema ni migongano?

Nakunukuu:
Dhana ya Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote kuumba ulimwengu unaowezekana kuwa na mabaya, wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao hauruhusu mabaya ni contradiction.
Kutokana na nukuu hiyo, ni mabaya gani ambayo Mungu ameyaruhusu?
Ni kwa nini wewe unasema ni mabaya?
Je unaweza thibitisha huo ubaya kama kweli upo?
 
Mimi najua kusoma, na vilevile najua kuamdika.

Rejea post # 314. Nimeeleza wazi kuwa hakuna migonano kwenye mistari hiyo. Kwa hiyo sina cha kupangua. Migonano unayoiona ipo kwenye akili yako mwenyewe sio katika biblia.
Je unaweza kuielezea hiyo migongano uliyoitaja?
Kwa nini unasema ni migongano?

Nakunukuu:
Dhana ya Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote kuumba ulimwengu unaowezekana kuwa na mabaya, wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao hauruhusu mabaya ni contradiction.
Kutokana na nukuu hiyo, ni mabaya gani ambayo Mungu ameyaruhusu?
Ni kwa nini wewe unasema ni mabaya?
Je unaweza thibitisha huo ubaya kama kweli upo?
Ukisema "mistari hii haina mgongano, kwa sababu hii na hii" kwa kila mistari, nitakuelewa. Nitasoma sababu zako na kuzikataa au kuzikubali kulingana na mantiki yako.

Ukisema "hakuna migongano, migongano unaiona wewe kwa akili yako" bila kutoa uthibitisho kwa nini hakuna migongano, nitakuona mtu anayelazimisha hoja asiyoweza kuitetea.

Mpaka sasa unalazimisha hoja usizoweza kutetea.

Unasema Mungu yupo. Hoja hii hujaweza kuitetea.

Umesema roho ipo, hoja hii hujaweza kuitetea.

Umesema haya maandiko ni matakatifu hayana migongano, hoja hii hujaweza kuitetea.

Kwa sababu.

Mungu hayupo.

Roho hayupo.

Vitabu vina migongano.

Kama unabisha, thibitisha vinginevyo kwa hoja zenye mantiki, si kwa hoja za kulazimisha tu.
 
Ukisema "mistari hii haina mgongano, kwa sababu hii na hii" kwa kila mistari, nitakuelewa. Nitasoma sababu zako na kuzikataa au kuzikubali kulingana na mantiki yako.

Ukisema "hakuna migongano, migongano unaiona wewe kwa akili yako" bila kutoa uthibitisho kwa nini hakuna migongano, nitakuona mtu anayelazimisha hoja asiyoweza kuitetea.

Mpaka sasa unalazimisha hoja usizoweza kutetea.

Unasema Mungu yupo. Hoja hii hujaweza kuitetea.

Umesema roho ipo, hoja hii hujaweza kuitetea.

Umesema haya maandiko ni matakatifu hayana migongano, hoja hii hujaweza kuitetea.

Kwa sababu.

Mungu hayupo.

Roho hayupo.

Vitabu vina migongano.

Kama unabisha, thibitisha vinginevyo kwa hoja zenye mantiki, si kwa hoja za kulazimisha tu.
Jamani! Si nilikuliza kwa nini unasema mistari hiyo ina migongano? Unaona ugumu gani kuelezea migongano uliyoitaja halafu tukaendelea kujadili?
Ukitoa maelezo ya migongano, itakuwa rahisi kwangu kutoa sababu ya kwa nini nasema sio migongano.

Wewe umeona kuwa ni migongano kwa uelewa wako, mimi sijaona kuwa ni migongano kwa uelewa wangu. Funguka, kwa nini unasema ni migongano.

Hoja zako hazina uzito wa kushindwa kuzitetea. Jitahidi kujibu maswali yanayoendana na hoja zako ili twende sawa. Kuna wakati inabidi nikuulize kwanza kabla ya kutoa jawabu. Sijui kwa nini hupendi kujibu maswali! Katika post # 323 nimekuuliza maswali rafiki sana, lakini hujajibu hata moja.

Sio kweli kwamba nalazimisha hoja nisizoweza kutetea. Ni wewe unayelazimisha hoja ionekane kama ina mantiki. Najibu hoja kutokana na upeo wa akili zangu. Si vinginevyo.

Na vilevile silazimiki kujibu hoja zako kwa kutumia mtazamo wako. Nitajibu kutokana na ufahamu wangu ili upate jibu sahihi kutoka kwangu. Huu ni mjadala, kila mtu na mtazamo wake.

Hoja ya uwepo wa Mungu tumejadili sana lakini hatukumaliza baada ya wewe kung'ang'ania hoja nyingine. Ukakimbilia hoja ya utakatifu wa vitabu badala ya uwepo wa Mungu. Huenda hata hii utaipindua na kuanza hoja nyingine.

Hoja ya uwepo wa Roho, sikumbuki kama tumewahi jadili. Kama unataka, iweke kwenye mjadala.

Kutetea hoja ya migongano ndani ya biblia, sio kazi ngumu kwangu kama utaelezea migongano uliyoiona. Umetaja migongano bila kutoa maelezo ya migongano hiyo. Kutaja na kueleza ni vitu viwili tofauti.
 
Jamani! Si nilikuliza kwa nini unasema mistari hiyo ina migongano? Unaona ugumu gani kuelezea migongano uliyoitaja halafu tukaendelea kujadili?
Ukitoa maelezo ya migongano, itakuwa rahisi kwangu kutoa sababu ya kwa nini nasema sio migongano.

Wewe umeona kuwa ni migongano kwa uelewa wako, mimi sijaona kuwa ni migongano kwa uelewa wangu. Funguka, kwa nini unasema ni migongano.

Hoja zako hazina uzito wa kushindwa kuzitetea. Jitahidi kujibu maswali yanayoendana na hoja zako ili twende sawa. Kuna wakati inabidi nikuulize kwanza kabla ya kutoa jawabu. Sijui kwa nini hupendi kujibu maswali! Katika post # 323 nimekuuliza maswali rafiki sana, lakini hujajibu hata moja.

Sio kweli kwamba nalazimisha hoja nisizoweza kutetea. Ni wewe unayelazimisha hoja ionekane kama ina mantiki. Najibu hoja kutokana na upeo wa akili zangu. Si vinginevyo.

Na vilevile silazimiki kujibu hoja zako kwa kutumia mtazamo wako. Nitajibu kutokana na ufahamu wangu ili upate jibu sahihi kutoka kwangu. Huu ni mjadala, kila mtu na mtazamo wake.

Hoja ya uwepo wa Mungu tumejadili sana lakini hatukumaliza baada ya wewe kung'ang'ania hoja nyingine. Ukakimbilia hoja ya utakatifu wa vitabu badala ya uwepo wa Mungu. Huenda hata hii utaipindua na kuanza hoja nyingine.

Hoja ya uwepo wa Roho, sikumbuki kama tumewahi jadili. Kama unataka, iweke kwenye mjadala.

Kutetea hoja ya migongano ndani ya biblia, sio kazi ngumu kwangu kama utaelezea migongano uliyoiona. Umetaja migongano bila kutoa maelezo ya migongano hiyo. Kutaja na kueleza ni vitu viwili tofauti.
Ndiyo maana nilisema hujui kusoma.
 
Nasikitika sana kuona mtu anatetea fundisho la Utatu jambo ambalo ndani ya biblia halipo.

Upo ushahidi mwingi wa maandiko unaotofautisha Mungu, Yesu Kristo na Roho Takatifu ambayo waamini wa Utatu wanaita Roho Mtakatifu kama vile ni mtu. Je, Mungu anaonekana? Yesu alionekana, hakuna aliemuona Mungu hata Musa mwenyewe.

~ Andiko la Yoh 17:3 lina maana gani? Ikiwa Yesu ni Mungu?

~ Methali 8:30 ina maanisha nini?

~ Mwanzo 1:26 Mungu alikuwa akizungumza na nani?

Ningependa kupata majibu ya maandiko, jibu hoja kwa andiko ili tuamini unachosema. Maandiko yapo mengi sana yanayo tifautisha Mungu, Yesu na roho/nguvu ya Mungu ya utendaji.
Kwani Biblia Takatifu ni Neno Pekee la Mungu??
 
Kwa nini ulisema sijui kusoma?
Tovuti inaonesha mistari inavyogongana na migongano iko wapi, halafu wewe unaniambia nikuambie migongano iko wapi.

Hujui kusoma na sioni haja ya kuendelea kujibizana nawe.

Unaangusha viwango vya mjadala.
 
Tovuti inaonesha mistari inavyogongana na migongano iko wapi, halafu wewe unaniambia nikuambie migongano iko wapi.

Hujui kusoma na sioni haja ya kuendelea kujibizana nawe.

Unaangusha viwango vya mjadala.
Tovuti imetaja migongano, haitoi maelezo ya migongano hiyo. Mimi sijauliza migongano iko wapi, usipindishe maneno. Nahitaji kutoka kwako, maelezo ya migongano hiyo.

Kama najua kuandika, nitashindwaje kujua kusoma? Sidhani kama uko sahihi!

Mjadala ni pamoja na kulizana maswali. Lakini wewe hutaki kabisa ulizwe swali. Ukiulizwa swali, unaanzisha hoja nyingine juu yake!

Hata hivyo, mimi sioni shida kujibizana na mtu yeyote, hata kwa yule anayejitoa ufahamu wa kujibu maswali. Nachukulia kama changamoto tu, na sina kawaida ya kuikimbia kizembe changamoto yoyote ile.
 
Tovuti imetaja migongano, haitoi maelezo ya migongano hiyo. Mimi sijauliza migongano iko wapi, usipindishe maneno. Nahitaji kutoka kwako, maelezo ya migongano hiyo.

Kama najua kuandika, nitashindwaje kujua kusoma? Sidhani kama uko sahihi!

Mjadala ni pamoja na kulizana maswali. Lakini wewe hutaki kabisa ulizwe swali. Ukiulizwa swali, unaanzisha hoja nyingine juu yake!

Hata hivyo, mimi sioni shida kujibizana na mtu yeyote, hata kwa yule anayejitoa ufahamu wa kujibu maswali. Nachukulia kama changamoto tu, na sina kawaida ya kuikimbia kizembe changamoto yoyote ile.
Cognitive dissonance.
 
[emoji23][emoji23],Mambo ya imani hayalazimishwi, maana ni vitu za kubuni,, kuna wanaoabudu mtu kama wewe, kuna wanaoabudu ng'ombe, etc,,
Kila mtu yuko huru kuabudu chochote

ndio maana huwa hatuwaelewi ndugu zetu,wanavyokomaa na Yesu wetu wakati wao wana Issa wao[emoji38].
 
So mungu yesu pale msalabani alikua anamlilia nani!?..na aliyemtia mimba Maryam nani!?..na neno wa yohana ni nani,na aliyemtuma yesu nani!?
Unamlinganisha Mwenyezi Mungu na babu yako!
Hata mungu wako anasema yeye!
[emoji116][emoji116]
بَدِيعُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ وَإِذَا قَضَىٰ أَمْرًا فَإِنَّمَا يَقُولُ لَهُ كُن فَيَكُونُ

[ AL - BAQARA - 117 ]
Yeye ndiye Muumba wa mbingu na ardhi pasina ruwaza; na anapo taka jambo basi huliambia tu: Kuwa! Nalo huwa.
 
Unamlinganisha Mwenyezi Mungu na babu yako!
Hata mungu wako anasema yeye!
[emoji116][emoji116]
بَدِيعُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ وَإِذَا قَضَىٰ أَمْرًا فَإِنَّمَا يَقُولُ لَهُ كُن فَيَكُونُ

[ AL - BAQARA - 117 ]
Yeye ndiye Muumba wa mbingu na ardhi pasina ruwaza; na anapo taka jambo basi huliambia tu: Kuwa! Nalo huwa.
Mungu siyo seremala muisrael,hakukatwa govi Wala kusulubiwa
 
Kwa hiyo ww unaamini nini?
Kwa nini ninachoamini kiwe muhimu?

Imani haihitaji kuwa kwenye facts. Unaweza kuamini hata uongo.

Hivyo imani si kitu muhimu, kwa sababu naweza kuamini mimi ndiye Mungu, wakati si kweli.

Kitu cha msingi ni ukweli, ukweli ni nini?

Tunajuaje huu ni ukweli?

Ukweli ni kwamba Mungu hayupo, tunajua hilo kwa kuchambua mambo kwa logical consistency.

Watu wana wajibu wa kupambana na hali zao kutatua matatizo yao. Mungu hayupo.

Habari ya kuwapo kwa Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote kuwapo, ni hdithi iliyotungwa na watu tu.

Kupata jibu la maswali ambayo hawana majibu yake.

Kujifariji kwamba kuna anaye control kila kitu.

Kuwapumbaza wengine na kuwatawala.

Kupata imani ya kuendelea kuishi bila mafadhaiko.
 
Back
Top Bottom