Fundisho la Utatu haliingii akilini kabisa, mnaoamini mmetoa wapi mbona Biblia iko wazi kabisa?

Fundisho la Utatu haliingii akilini kabisa, mnaoamini mmetoa wapi mbona Biblia iko wazi kabisa?

Kwani nani kaleta hoja ya vitabu vitakatifu hapa? Mimi au wewe?

Unaleta hoja ya vitabu vitakatifu, nikikubana unasema hoja yetu si ya vitabu vitakatifu?

Unavikana vitabu vitakatifu na kusema si hoja kwako?

Unasema msingi wa imani yako si vitabu vitakatifu?
Rudi kwenye hoja yetu tafadhali. "Mungu yupo na hana chanzo".
 
Kwa hivyo umekubali vitabu vitakatifu havina hoja?
Rudi kwenye hoja, usijitoe ufahamu tafadhali.

Utakatifu wa vitabu ni uzi mwingine, ukipenda anzisha tujadili.

Mungu yupo na hana chanzo.
 
Biblia inamwita Roho Mtakatifu wewe unaita Roho Takatifu! Unatumia Biblia ya wapi? Dah; Shetani is so powerful.
Una mengi sana ya kujifunza ili uelewe kuwa kilichowachanganya wengi ni Lugha iliyotumika kuandika Agano Jipya na tafsiri kutoka Lugha hiyo kwenda lugha zingine.

Lugha iliyotumiwa kuandika original manuscript za Agano Jipya ni Kiyunani (Kigiriki). Lugha ya Kigiriki inatumia gender pronouns na nouns hata kwenye vitu. Ndiyo maana waliotafsiri waliandika Roho Mtakatifu badala ya Roho Takatifu.
 
Una mengi sana ya kujifunza ili uelewe kuwa kilichowachanganya wengi ni Lugha iliyotumika kuandika Agano Jipya na tafsiri kutoka Lugha hiyo kwenda lugha zingine.

Lugha iliyotumiwa kuandika original manuscript za Agano Jipya ni Kiyunani (Kigiriki). Lugha ya Kigiriki inatumia gender pronouns na nouns hata kwenye vitu. Ndiyo maana waliotafsiri waliandika Roho Mtakatifu badala ya Roho Takatifu.
... kwamba wewe ni mtaalamu wa tafsiri kuliko waliotafsiri Biblia? Kwamba nina mengi ya kujifunza kwamba sio Roho Mtakatifu bali Roho Takatifu? Ha ha ha! Be serious Mkuu.

Hakika nimeamini Shetani ni baba wa uongo na upotoshaji. Biblia nzima Roho Mtakatifu anawakilishwa kwa kiwakilishi nafsi kiambata "a" badala ya "i" sijui unatuletea stori za wapi Chief?
 
Rudi kwenye hoja, usijitoe ufahamu tafadhali.

Utakatifu wa vitabu ni uzi mwingine, ukipenda anzisha tujadili.

Mungu yupo na hana chanzo.
Kama utakatifu wa vitabu ni hoja ya uzi mwingine, kwa nini umeileta hoja hiyo katika uzi huu?

Mimi sijaileta hoja hiyo hapa, wewe umeileta.

Hoja umeleta wewe mwenyewe, unaona nakubana, unaikana kuwa si ya uzi huu sasa?

Unakana na kusema vitabu vitakatifu havina hoja?

Siondoki hapo mpaka nipate jibu.
 
... kwamba wewe ni mtaalamu wa tafsiri kuliko waliotafsiri Biblia? Kwamba nina mengi ya kujifunza kwamba sio Roho Mtakatifu bali Roho Takatifu? Ha ha ha! Be serious Mkuu.

Hakika nimeamini Shetani ni baba wa uongo na upotoshaji. Biblia nzima Roho Mtakatifu anawakilishwa kwa kiwakilishi nafsi kiambata "a" badala ya "i" sijui unatuletea stori za wapi Chief?
Kwa ufahamu wako unafikiri waliotafsiri Biblia walikuwa sahihi kwa asilimia 100%?
Mimi ni MKRISTO tena ni MKRISTO kweli kweli (sijisifu la hasha), lakini nimeutafuta UKWELI na nimejua kuna makosa mengi tu ya "tafsiri" ndani ya Biblia.
Fanya utafiti wako mdogo utaona hilo. Hata hao wanaojiita "theologians" wanalifahamu hilo kwa hakika.

ROHO TAKATIFU au ROHO MTAKATIFU siyo nafsi ya tatu ya MUNGU BABA, bali ni uwezo wa MUNGU BABA au nyenzo ya MUNGU BABA anayowapatia "wateule wake" ili waweze kutenda kazi alizowakusudia kuzitenda. Tena, uwezo huo au nyenzo hiyo ya MUNGU BABA ndiyo inayowafanya wateule hao kufanyika "watoto wa MUNGU". Hakuna mwanadamu atakayeingia kwenye UFALME WA MUNGU bila ya kuwa na ROHO TAKATIFU ndani yake.

ROHO TAKATIFU ndiyo ROHO YA MUNGU na pia ndiyo ROHO YA KRISTO.

Ikiwa MUNGU BABA ni "ROHO", iweje basi awe na nafsi nyingine ya tatu ambayo ni ROHO MTAKATIFU???

BWANA YESU KRISTO alisema hivi :
"mimi na BABA yangu tu wamoja" (YOHANA 10:30).
Kama Roho Mtakatifu angekuwa nafsi ya tatu ya MUNGU basi YESU KRISTO angesema, mimi, roho mtakatifu, na BABA yangu tu wamoja.

Tena YESU KRISTO akasema;

Yohana 14:10​

"Je, huamini ya kuwa mimi niko ndani ya Baba, naye Baba yuko ndani yangu? Maneno ninayowaambia siyasemi kwa ajili yangu mwenyewe, bali Baba akaaye ndani yangu ndiye atendaye hizi kazi".

Hapa napo tunaona BWANA YESU KRISTO hamtaji ROHO TAKATIFU, bali anaonesha dhahiri kuwa kuna wawili tu, yaani MUNGU BABA na MUNGU MWANA.

Pia soma YOHANA 1:1-14.
 
YOHANA 1

Neno akawa mwili

1 Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. 2 Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu. 3 Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika chochote kilichofanyika. 4 Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. 5 Nayo nuru yang'aa gizani, wala giza halikuiweza.

6 Palitokea mtu, ametumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana. 7 Huyo alikuja kwa ushuhuda, ili aishuhudie ile nuru, wote wapate kuamini kwa yeye. 8 Huyo hakuwa ile nuru, bali alikuja ili aishuhudie ile nuru. 9Kulikuwako Nuru halisi, amtiaye nuru kila mtu, akija katika ulimwengu. 10 Alikuwako ulimwenguni, hata kwa yeye ulimwengu ulipata kuwako, wala ulimwengu haukumtambua. 11Alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea. 12 Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake; 13 waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu. 14 Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.
 
Kama utakatifu wa vitabu ni hoja ya uzi mwingine, kwa nini umeileta hoja hiyo katika uzi huu?

Mimi sijaileta hoja hiyo hapa, wewe umeileta.

Hoja umeleta wewe mwenyewe, unaona nakubana, unaikana kuwa si ya uzi huu sasa?

Unakana na kusema vitabu vitakatifu havina hoja?

Siondoki hapo mpaka nipate jibu.
Umebanwa mpaka Unatafuta pa kutorokea.
Utakatifu wa vitabu haukuwa mkondo wa mjadala wetu kuhusu uwepo wa Mungu. Ni sawa na wewe ulipoleta hadithi za James Bond 007, lakini hatukubadili mkondo wa hoja yetu ya uwepo wa Mungu au la. Umejitoa ufahamu kabisa kwa kujaribu kunitia gizani katika mwanga. Sio rahisi katika hili.

Hata hivyo kama unataka tujadili hoja juu ya vitabu vitakatifu, niko tayari. Karibu.

Mungu yupo na hana chanzo.
 
Umebanwa mpaka Unatafuta pa kutorokea.
Utakatifu wa vitabu haukuwa mkondo wa mjadala wetu kuhusu uwepo wa Mungu. Ni sawa na wewe ulipoleta hadithi za James Bond 007, lakini hatukubadili mkondo wa hoja yetu ya uwepo wa Mungu au la. Umejitoa ufahamu kabisa kwa kujaribu kunitia gizani katika mwanga. Sio rahisi katika hili.

Hata hivyo kama unataka tujadili hoja juu ya vitabu vitakatifu, niko tayari. Karibu.

Mungu yupo na hana chanzo.
Kuna swali la James Bond 007 umeniuliza nikashindwa kujibu?

Hoja ya vitabu vitakatifu umeileta mwenyewe, jibu maswali yanayoihusu.

Hoja ya vitabu kuwa vitakatifu umeikataa? Huamini katika vitabu vitakatifu tena?
 
Kwa ufahamu wako unafikiri waliotafsiri Biblia walikuwa sahihi kwa asilimia 100%?
Mimi ni MKRISTO tena ni MKRISTO kweli kweli (sijisifu la hasha), lakini nimeutafuta UKWELI na nimejua kuna makosa mengi tu ya "tafsiri" ndani ya Biblia.
Fanya utafiti wako mdogo utaona hilo. Hata hao wanaojiita "theologians" wanalifahamu hilo kwa hakika.

ROHO TAKATIFU au ROHO MTAKATIFU siyo nafsi ya tatu ya MUNGU BABA, bali ni uwezo wa MUNGU BABA au nyenzo ya MUNGU BABA anayowapatia "wateule wake" ili waweze kutenda kazi alizowakusudia kuzitenda. Tena, uwezo huo au nyenzo hiyo ya MUNGU BABA ndiyo inayowafanya wateule hao kufanyika "watoto wa MUNGU". Hakuna mwanadamu atakayeingia kwenye UFALME WA MUNGU bila ya kuwa na ROHO TAKATIFU ndani yake.

ROHO TAKATIFU ndiyo ROHO YA MUNGU na pia ndiyo ROHO YA KRISTO.

Ikiwa MUNGU BABA ni "ROHO", iweje basi awe na nafsi nyingine ya tatu ambayo ni ROHO MTAKATIFU???

BWANA YESU KRISTO alisema hivi :
"mimi na BABA yangu tu wamoja" (YOHANA 10:30).
Kama Roho Mtakatifu angekuwa nafsi ya tatu ya MUNGU basi YESU KRISTO angesema, mimi, roho mtakatifu, na BABA yangu tu wamoja.

Tena YESU KRISTO akasema;

Yohana 14:10​

"Je, huamini ya kuwa mimi niko ndani ya Baba, naye Baba yuko ndani yangu? Maneno ninayowaambia siyasemi kwa ajili yangu mwenyewe, bali Baba akaaye ndani yangu ndiye atendaye hizi kazi".

Hapa napo tunaona BWANA YESU KRISTO hamtaji ROHO TAKATIFU, bali anaonesha dhahiri kuwa kuna wawili tu, yaani MUNGU BABA na MUNGU MWANA.

Pia soma YOHANA 1:1-14.
... asante kwa ufafanuzi japo umezingatia zaidi itikadi za kimadhehebu kuliko Biblia yenyewe kuhusu Roho Mtakatifu vs Roho Takatifu. Kama imefahamika kwamba waliotafsiri Biblia wamekosea kuhusiana na hilo, kwanini marekebisho yasifanywe ili iendane na tafsiri sahihi; at least dhehebu lenu mtoke na toleo sahihi?

1. Yohana 14:16-17; "Nami nitamwomba Baba naye atawapa msaidizi mwingine ili akae nanyi hata milele ndiye roho wa kweli ...."; ==> Nami (mimi/Yesu), Baba, msaidizi mwingine. Wanatajwa wangapi hapo? (Yesu, Baba, na Roho Mtakatifu).

3. Matendo ya Mitume 5:3, 4 "Petro akasema, Anania kwa nini shetani amekujaza moyo wako kumwambia uongo Roho mtakatifu na kuzuia kwa siri sehemu ya dhamani ya kiwanja kilipokuwa kwako hakikuwa mali yako na kilipokuwa kimekwisha kuuzwa, dhamani yake haikuwa katika uwezo wako? ili kuwaje hata ukaweka neno hilo mwonyoni mwako? hukumwambia uongo mwanadamu bali Mungu.";

Kama kumwambia uongo Roho Mtakatifu ni kumwambia uongo Mungu utasemaje Roho Mtakatifu sio Mungu?
 
Kuna swali la James Bond 007 umeniuliza nikashindwa kujibu?

Hoja ya vitabu vitakatifu umeileta mwenyewe, jibu maswali yanayoihusu.

Hoja ya vitabu kuwa vitakatifu umeikataa? Huamini katika vitabu vitakatifu tena?
Sikuuliza swali kwani ningekuwa nimekengeuka mkondo wa hoja yetu. Siulizi maswali kizembe.

Vitabu vitakatifu haikuwa hoja, ila unalazimisha iwe hoja. Niko tayari kujibu hoja zako kama utauliza tena ukiona bodo zinatija kijamii.

Sivikatai vitabu vitakatifu kwani hivyo ndiyo msingi wa imani yetu.
 
Sikuuliza swali kwani ningekuwa nimekengeuka mkondo wa hoja yetu. Siulizi maswali kizembe.

Vitabu vitakatifu haikuwa hoja, ila unalazimisha iwe hoja. Niko tayari kujibu hoja zako kama utauliza tena ukiona bodo zinatija kijamii.

Sivikatai vitabu vitakatifu kwani hivyo ndiyo msingi wa imani yetu.
Vitabu gani hivyo, vitaje tuviangalie tuone kama msingi wa imani yako ni sahihi au si sahihi.
 
Vitabu gani hivyo, vitaje tuviangalie tuone kama msingi wa imani yako ni sahihi au si sahihi.
Biblia Takatifu na Kuran Takatifu ndiyo vitabu ninavyovifahamu kwa majina. Kati ya hivyo, nafahamu mengi ktk Biblia Takatifu.
 
Biblia Takatifu na Kuran Takatifu ndiyo vitabu ninavyovifahamu kwa majina. Kati ya hivyo, nafahamu mengi ktk Biblia Takatifu.
Biblia na Quran vyote vimejaa contradictions.

Hivyo si vitakatifu.

Unaelewa hilo?
 
Hujathibitisha Mungu yupo.

Kiukweli watu wanaisema Mungu yupo ndio wana kiburi.

Wamejiwekea kiburi cha kusema wanajua chanzo cha ulimwengu, na chanzo hicho ni huyo Mungu wao.

Sisi tunaobisha ni watu wanyenyekevu sana.

Tunajua ulimwengu ni mgumu sana kuuelewa, tumejishusha kwa unyenyekevu tukisema kwamba ulimwengu huu maswali yake ni makubwa sana, na hili jibu jepesi la Mungu ni kiburi, tena cha kijinga.

Unyenyekevu wetu unatutaka tukubali hatujui majibu, tufanye uchunguzi kujua majubu zaidi kuhusu chanzi cha ulimwengu, maisha na kika kitu.

Kwa hivyo, you have it backwards.

Watu wanaosema wao wanamjua Mungu ndiyo wenye kiburi.

Sisi tunaohoji hii imani na kutafuta majibu ya kina ni wanyenyekevu sana, tunajua ulimwengu una maswali magumu yasiyotaka kukurupuka kwa kutoa majibu ya kiimani ambayo hayapi kwenye research.
Huo unyenyekevu unamfanyia nani?
 
BIBLIA INAFUNDISHA NINI JUU YA UTATU?
JIBU.

Mungu ni mkubwa kuliko sisi na tusitarajie kumuelewa katika kila jambo. Utatu ni jambo gumu kulieleza kwa kina. Hakuna mwanadamu anayeweza kulielewa kwa undani zaidi. Biblia inafundisha kuwa Baba ni Mungu, ya kuwa Yesu ni Mungu na pia Roho mtakatifu ni Mungu. Biblia pia inafundisha kuna Mungu mmoja tu. Ijapokuwa tunaweza kufahamu uhusiano tofauti tofauti wa sehemu za utatu huu ni vigumu kuelewa kwa akili ya kibinadamu. Hii haimaanishi kuwa si kweli au si maagizo ya Biblia.

Utatu ni Mungu mmoja katika nafsi tatu. Aya za biblia zifuatazo zitatumika kufafanua neno hili.

1) Kuna Mungu mmoja: kumbukumbu la torati 6:4; wakorintho wa kwanza 8:4; wagalatia 3:20; Timotheo wa kwanza 2:5.

2) utatu una nafsi tatu: mwanzo 1:1; 1:26; 3:22; 11:7 Isaya 6:8; 48:16; 61:1; Mathayo 3:16-17; Mathayo 28:19; wakorintho wa pili 13;14. Katika mwanzo 1:1 neno la wingi “Elohim” linatumika. Katika mwanzo 1:26; 3:22; 11:7 na Isaya 6:8, neno la wingi “sisi” limetumika. Kwa hivyo neno “Elohim’ na “sisi” kumaanisha zaidi ya mmoja halina pingamizi.

Katika Isaya 48:16 na 61:1, Mwana azungumza huku akihusisha Baba na Roho Mtakatifu. Fananisha Isaya 61:1na Luka 4:14-19 kuona Mwana akizungumza. Mathayo 3:16-17 inaelezea ubatizo wa Yesu. Anayeonekana hapa ni Mungu Roho mtakatifu akimshukia Mungu Mwanahuku Mungu Baba akitangaza furaha yake katika Mwana. Mathayo 28:19 na wakorintho wa pili 13:14 ni mifano ya nafsi tatu katika Mungu mmoja.

3) Nafsi hizi tatu zinatambulika katika maandiko. Katika agano la kale “ BWANA” linatofautishwa na “Bwana” (mwanzo 19:24; Hosea 1:4). “BWANA” ana “Mwana” (zaburi 2:7, 12; Methali 30:2-4). Roho anatofautishwa na “BWANA” (hesabu 27:18) na pia kutoka “Mungu” (zaburi 51:10-12). Mungu mwana atofautishwa na Mungu Baba (zaburi 45:6-7; waebrania1:8-9). Katika agano jipya, Yohana 14:16-17 ndipo Yesu anazungumza na Baba juu ya kuleta Msaidizi, Roho mtakatifu. Hii ina maana ya kuwa Yesu hakujichukulia yeye mwenyewe kuwa Baba wala Roho Mtakatifu. Katika kila mahali ndani ya agano jipya Yesu alipozungumza na Mungu Baba alikuwa akizungumza na nafsi moja wapo ya Utatu – Baba.

4) kila nafsi katika utatu huu ni Mungu: Baba ni Mungu: Yohana 6:27; warumi 1:7; petro wa kwanza 1:2. Mwana ni Mungu: Yohana 1:1, 14; warumi 9:5; wakolosai 2:9; waebrania 1:8; Yohana wa kwanza 5:20. Roho mtakatifu ni Mungu: Matendo ya mitume 5:3-4; wakorintho wa kwanza 3:16 (anayedumu ndani ni Roho mtakatifu –warumi 8:9; Yohana 14:16 –17; Matendo ya mitume 2:1—4).

5) Katika mpangilio ndani ya utatu huu: maandiko yanaonyesha kuwa Roho Mtakatifu humtumikia Baba na Mwana na Mwana humtumikia Baba. Huu ni uhusiano wa ushirika wao wala hupunguzi uungu wa nafsi yoyote ile. Kuhusu Mwana tazama: luka 22:42; Yohana 5:36; Yohana 20:21; Yohana wa kwanza 4:14. kuhusu Roho Mtakatifu tazama Yohana 14:16; 14:26; 15:26; 16:7 na hasa Yohana 16:13-14.

6) Majukumu ya kila nafsi katika utatu: Baba ndiye aliyesababisha kuwako kwa 1) ulimwengu (wakorintho wa kwanza 8:6; Ufunuo wa Yohana 4:11), 2) ufunuo wa kimungu (Ufunuo wa Yohana 1:1) 3)wokovu (Yohana 3:16-17); Matendo ya kibinadamu ya Yesu ( Yohana 5:17; 14:10). Baba anaonekana kwanza katika haya yote.

Mwana ni wakala ambaye Baba humtumia kufanyia haya: 1) Kuumba na kustawisha ulimwengu (wakorintho wa kwanza 8:6; Yohana 1:3; wakolosai 1:16-17); 2) ufunuo wa kimungu (Yohana 1:1; Mathayo 11:27; Yohana 16:12-15; Ufunuo wa Yohana 1:1); na 3) wokovu ( wakorintho wa pili 5:19; Mathayo 1:21; Yohana 4:42). Baba alifanya mambo haya yote kupitia Mwana anayetenda kazi kama mwakilishi wake.

Roho Mtakatifu ndiye anayetumiwa na Baba kufanya haya: 1) uumbaji na ustawishaji wa ulimwengu (mwanzo 1:2; Ayubu 26:13; zaburi 104: 30); 2) ufunuo wa kimungu (Yohana 16:12-15; waefeso 3:5; petro wa pili 1:21); 3) wokovu (Yohana 3:6; Tito 3:5; petro wa kwanza 1;2); na 4) matendo ya Yesu ( Isaya 61:1; Matendo ya mitume 10;38). Haya yote Baba ayatenda kupitia Roho Mtakatifu.

Baba, Mwana na Roho si vipande vya Mungu bali kila nafsi ni Mungu. Mungu asiyeonekana na macho hawezi kuelezwa kwa usahihi na mwenye kuona na macho ya kibinadamu akaeleweka. Lakini katika hali zote tazama Mungu kama nafsi tatu zisizogawanyika kuwa Miungu mitatu bali Mungu mmoja tu. “jinsi zilivyo kuu utajiri wa hekima na maarifa ya Mungu! Hukumu zake hazichunguziki, wala njia zake hazitafutikani! Maana ni nani aliyeijua nia ya Bwana?” 9 warumi 11:33-34)
Umeandika vitu vinavyosomeka!
 
Mwanzo 1:26-28 BHN
Kisha Mungu akasema, “TUMFANYE mtu kwa mfano wake......" Mimi sio mtu wa kusali sana ila najaribu kuwaza, Mungu alikua na nani alivyokua akihusisha uwingi ktk uumbaji wake na hata mambo mengine?
 
Back
Top Bottom