Funzo: Rais Pierre Nkurunziza pesa ameziacha

Kama Nkurunzizah angeweka mfumo mzuri wa madaraka familia yake ingekuwa na uhakika wa kupata mafao yao kwa mujibu wa sheria.
 
Haya maazimio haya mmmmmmmhh
 
Ila wale watoto walionichangia humu jf Mungu awalinde, yaani mtu kukubali kutoa hela yake akupe mtazame mara mbili mbili.

Pia wapo wale wengine walinituhumu na kunitukana, hao namwachia Mungu ahangaike nao.

Nkurunzinza, na u handsome wako wote umeacha all.
 
Tatizo huwezi kimbia na mihela yote,hainei mfukoni,wale unaoamini wakutunzie ndo wanakupiga,,San Abacha nae alichota bilions ya madola wakampiga
sa hivi yule wa Sudan Al Bashiri naye wanarudisha ye hakutorosha kitu
 
Chadema siku mkichukua nchi mtanyonga watoto wa viongoz wa CCM Mpaka wasio kua na hatia na ikija Tena kuchukua CCM chadema watafungwa mpaka wale walevi kwa kunyanyasa watu nawaza japo najua chadema haito chukua nchi
 
Waafrika tuna akili ndogo sana eti unakuta wajinga fulani wanasema mtu fulani atawale maisha bila kujua kwa kiumbe chochote humu duniani hakuna cha maisha.

Kitu ambacho George Washington alikiona mwaka 1776 eti kuna waswahili bado kabisa hawawezi kuliona leo hii mwaka 2020....!!!!! Nafikiri hili ni tatizo la IQ zaidi kuliko kitu chochote kile.

Ndio maana sisi waafrika tunafeli sana kwani tuwapo madarakani tunakuwa gizani kabisa na hatujui kama kuna na kesho pia, yaani mtu analewa hadi anafikiri anaweza akafanya kikao akamualika na Mungu vile vile.

Angalia huu mswaada uliyopitishwa majuzi na bunge, yaani watu wanachukulia kama wao ndio wanaseti ajenda za dunia na wana-act kama vile hakuna Mungu ila wao ndio mbadala wake.

Madaraka ni kitu kibaya sana hasa kwetu waswahili.
 
Mkuu hakuna funzo lolote juu ya kifo cha mheshimiwa Nkurunzinza,maana kifo kipo tu na kifo ni kwaajili ya kiumbe chochote kilicho hai.

Kama binadamu hatuwezi kuacha harakati zetu za kupambana na maisha eti kisa tutakufa,huu ni upuuzi mkubwa

Kilichomkuta mheshimiwa ni sawa na asikari kufa vitani,kwa dhana yako unataka kutuambia kuwa tusifanye harakati za maisha kwa kuhofia kifo?

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
 
Kila nikitafakari kulikuwa na ulazima gani wa mswada ule kuletwa bungeni nacheka kwa uchungu

Hakuna Rais aliyestaafu aliyewahi kusumbuliwa

Hakuna Makamu Rais mstaafu aliyewahi kusumbuliwa

Hakuna waziri Mkuu aliyewahi kusumbuliwa

Hakuna Spika mstaafu aliyewahi kusumbuliwa

Hakuna Jaji mstaafu aliyewahi kusumbuliwa

Wote wanaheshima zao mtaani na wanakula pension zao kiroho safi na wengine hadi wanahama na vyama na kurudi tena bila wasiwasi

Kwanini uletwe sasa hivi? Wanajipanga kufanya nini miaka mitano ijayo?

Hakika yajayo yanafurahisha. Ukiona mtu anajihami mapema, ni dalili kwamba anayo yawaza anayajua mwenyewe
 

hata wewe unaelazimisha mada kesho yako iombee kwa Mungu! ametangulia tu wanaofuata nadhan unajua
 
Eeh corona endelea kufanya ziara za kustukiza kwa wale wasio na mapenzi mema.🙏🏾
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…