Furahia Uhuru ulionao sasa, ni zawadi kubwa sana maishani mwako

Furahia Uhuru ulionao sasa, ni zawadi kubwa sana maishani mwako

Afande makalo wa kirumba central mshe*Zi sana yule bwana,ikifika wakati wa kulala usiku anamuamrisha nyampala achote maji chooni amwage kwenye sakafu ili watu walale kwenye maji.nilikaa mule siku 3 ila nilitoka nimekonda nimebaki kichwa tu!![emoji16][emoji1]

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
KUANGALIA CHINI

ile tumetoka kukaguliwa pasport zetu palee bet bridge na kugongewa mihuri ya kuingiza SA ilikuwa kama saa 7 usiku tukarudi kwenye basi tulilokuwa tukisafiri nalo ilikuwa mwendo kama wa lisaa limoja na nusu nafikiri ilikuwa saa 8:30 au saa tisa kamili usiku

Ndipo kati ya abiria mwenzetu alipoomba kwenda kujisaidia alibanwa na haja dereva ilibidi amsaidie ashuke akajisaidie ndipo aliporudishwa kwa kasi ya ajabu na vipande kama vitatu vikiwa na bunduki tulianza kupukutishwa/kuibiwa sim na pesa huku wazee wa kazi wakipita city moja moja kutusachi huku akikuwekea bunduki kichwani; MUNGU UTULINDE WATOTO WAKO WATULIVI

HAPO ILIKUWA; don’t look at me, yaani usiniangalie huku anakwambia angalia chini:

Nilicheka sana baada ya kuibiwa na wale majambazi kuondoka bila ya kumdhuru yeyote kwenye basi lile,

Kwenye siti ya watu watatu tulikaa wanaume wawili na kidada kimoja sasa hapo nishakula kipondo cha kutosha na kujibana bana na kutoa nilivyotoa na nilivyoficha ALHAMDULLILLAH ndio kaka jambazi akaamia kwa huyo dada tuliyokaa nae city moja alikuwa akiambiwa DON’T LOOK AT ME- dada alikuwa haelewi chochote alizidi kumkodolea macho yule jambazi/kibaka daah ikabidi nimwambie huyo anakwambia usimuangalie angalia chini dada atakuua huyoo ndipo dada akashituka na kuanza kuangalia chini maana alikuwa akipigwa kwa kutoelewa daah kitambo sana - MR.FINISHI alikuja kufanya kazi yake ya kufinish daah hatari

Sister nimekumisi sana kama unaona ujumbe huu najua utakumbuka kitu em ni dm tupige stori miaka minne sasa imepita
DAAH MAISHA HAYAA MMMH

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kuna tukio niliwahi kulifanya mwaka 2004, nikapelekwa butimba na mzee wangu akakomaa nisichomoke kwa dhamana for 28 days.

Jesus Christ, hapo nilikua mahabusu tu, niliyo yaona shetani akasome wallah

[emoji15][emoji15][emoji15][emoji15]
 
Back
Top Bottom