Fursa ya safari ya kibiashara China (kwa wajasiriamali wenye mitaji midogo)

Fursa ya safari ya kibiashara China (kwa wajasiriamali wenye mitaji midogo)

Kutakuwa na safari ya kibiashara kwa wajasiriamali wenye mitaji kidogo nchini China mji wa YI WU mwezi wa tatu mwaka huu wa 2024 tarehe kumi hivi
Safari itakuwa ya pamoja kwa watu wasiopungua 10 na wasiozidi 20.. Faida ya safari hii ya pamoja
.Kupata barua ya mwaliko kwa bei nafuu
. Kupata tickets kwa bei nafuu
. Malazi ya pamoja ya bei nafuu uwapo huko
. Usafiri wa bei nafuu
. Ukalimani
. Mtandao wa maduka ya jumla makubwa na madogo
.Kupata connection mbalimbali za wafanyabiashara na wazalishaji wa China
. Gharama nafuu za chakula, vinywaji matembezi nknk
. Gharama nafuu na za uhakika za kusafirisha mizigo kurudi nchini..

Hii ni fursa mpya na wale watakaoweza kwenda ndio watafungua pazia kwa wengine huko mbeleni
Yale mambo ya kuagiza online ama kumuagiza mtu na kuishia kutapeliwa sasa yanafika mwisho.. Lakini vilevile kununua kitu kwa picha nayo yamafikia ukomo wake
Nitaweka mawasiliano rasmi kwa wale wote walio tayari.. Dirisha la waendaji litafungwa wiki ya pili ya mwezi February siku ya wapendanao

Nyongeza:
Kwa vijana wasio na mishe naweza kuwapa mizigo ya mali kauli kama wakitimiza vigezo na masharti

Sent using Jamii Forums mobile app
Kimepanda kimeshuka ntantarira nyingi. Unataka kuwapiga watu vihela vyao huna lolote
20231224_095052.jpg
 
Huu unaofanya ni ubatili, nitasema kwa nn na yoyote aliyekua excited na hii fursa awe makini sana

Umeiweka fursa kwa namna nzuri ya kuvutia, haya hufanywa na wote wanaiona fursa ndani ya fursa kama ilivyokua kwa Ontario, mr kuku, jatu, mr vanilla, kalyinda and the likes

Ukweli mchungu fursa yoyote nzur inayolipa haishirikishi watu public hivi. Kikawaida binadamu sisi ni wabinafsi, hiki niliwahi kumueleza Ontario kuwa Kama kweli forex inalipa hivyo unapata wapi muda wa siku nzima kufundisha watu? Huo muda si ungekua unatumia kuingiza hizo pesa za forex ili uwe bilionea zaidi? Kwamba pesa umezichoka?

Sasa mshana, ww unatafuta watu uwape semina na uwaeleze kuhusu kwenda china kuchukua bidhaa na utawasaidia kuanzia process za visa kusafiri watapofikia hadi masokoni wataponunua bidhaa. Muda wote huu utaoutumia ww malipo yako ni nn?umejitolea? Ukisema umejitolea hapa ndio umeandaa ubatili niliosema mwanzo
Kama kuna malipo basi ilipaswa kuyaweka wazi mapema kabisa.

Nimeona umesema utawapa pia watu bidhaa za mali kauli, hii ni namna ya kuvutia fursa uliyotangaza. Hii ni ubatili, labda ulikua unatania. Mali kauli haiwi rahisi hivi kama ulivyoiweka. Wapo wataoona nipo negative sababu tu ya kuvutiwa na maneno yako. Wabongo wengi ni rahisi kuwatapeli mtandaoni ukiweza tu kuwaaminisha watapata utajiri au fursa nzuri bure au kwa gharama ndogo

Msaada mkubwa na mzuri ulipaswa uweke post ueleze kuanzia mwanzo wa anavyotakiwa kufanya kukata ticket na gharama average zipo vipi, kuproces visa na njia ipoje na gharama zipo vipi, kusafiri, hotel huko average gharama zipo vipi, wapi pa kufikia, masoko yalipo na masoko yalipo contacts zao, watumie kampuni ipi kwa shipping
Kutokea hapo anayetaka angejipima, na kwa msaada zaidi angekutafuta pale alipokwama. Lakini hii yako haina tofauti na kina Ontario, mr kuku, jatu n.k
Halafu mkuu imagine mtu anaaminishwa 6m itamtosha kwenda na kurudi China huku akiwa kanunua mzigo. Nimesema hiyo hela si bora apewe yeye Mshana awaagizie watu ila baadae mitaji ikikua waende wenyewe? Bado wanabisha.
 
Halafu mkuu imagine mtu anaaminishwa 6m itamtosha kwenda na kurudi China huku akiwa kanunua mzigo. Nimesema hiyo hela si bora apewe yeye Mshana awaagizie watu ila baadae mitaji ikikua waende wenyewe? Bado wanabisha.
Nadhani tumpe muda mtoa fursa kwani amesisitiza information nyingi na ufafanuzi atautoa next week ambayo inaanza kesho.
 
BTW watanzania na hususani wajasiriamali walio wengi wamekuwa makini sana na taarifa za mitandaoni hivyo siyo mburura/ignorant kama mnavyowachukulia baadhi yenu. Utapeli wa biashara za china kwa wafanyabiashara hapo kariakoo umewafundisha wengi sana. Si rahisi mtu awe na zaidi ya 5M kwa Sasa ukamtapeli kirahisi. Waliotoa maoni kuhusu tahadhali za kuchukua kutokana na fursa iliyotolewa na Mshana Jr wamefanya vizuri tena kizalendo lakini hawapaswi kubeza idea yake. Watanzania tumekuwa tukitishana juu ya fursa ndo maana unakuta mtu ana kamtaji kake lakini kutokana na vitisho vya wengi anaambulia ama kughairi au kutochukua uamuzi na kutapanya mtaji wake. Tunachohitaji watu wawe wazalendo kwa nchi na watz wenzao, hata kama coordinator atapata chochote nae siyo mbaya ili mradi amewapa watu exposure nao wakapata pa kuanzia. Kwenda China siyo kama kwenda Kizimkazi, unahitaji watu wenye connection na exposure. Naomba tusimkatishe tamaa mleta idea na wale walionza kuhamasika japo tahadhari ni mhimu kwa Kila fursa.
 
Sasa Mshana Jr Mchina karibu atazindua kituo cha biashara hapo Ubungo ambacho kitakuwa kinatoa huduma za exhibition trading platform, cros-border E-commerce platform, commodity procurement platform kwa Made in China goods only

Hata huyo mfanyabiashara wa K/koo badala ya kwenda China anaweza kwenda Ubungo akajionea bidhaa anazopenda then akaenda kwa watu wa procure watakaokuwa na ofisi zao hapo hapo akafanya malipo akaagiza mzigo kutoka China. Ubungo itakuwa ni one stop wholesale center

Hii imekaaje?
 
Sasa Mshana Jr Mchina karibu atazindua kituo cha biashara hapo Ubungo ambacho kitakuwa kinatoa huduma za exhibition trading platform, cros-border E-commerce platform, commodity procurement platform kwa Made in China goods only

Hata huyo mfanyabiashara wa K/koo badala ya kwenda China anaweza kwenda Ubungo akajionea bidhaa anazopenda then akaenda kwa watu wa procure watakaokuwa na ofisi zao hapo hapo akafanya malipo akaagiza mzigo kutoka China. Ubungo itakuwa ni one stop wholesale center

Hii imekaaje?
Sina hakika kama bei ya mchina kukuagizia na kukuletea mzigo itakuwa cheap kiasi hicho au same as umenunulia china. Ikiwa kama unavyodhania basi flow ya watu kwenda China itapungua sana kibiashara na hii ni itakuwa na economic impact kwa both Tz na China. Ngoja tusubiri ikishafunguliwa but kwa mtazamo wangu pale watafacilitate mambo ya transport, logistics, shipping, marketing and procurement facilities.
 
Sina hakika kama bei ya mchina kukuagizia na kukuletea mzigo itakuwa cheap kiasi hicho au same as umenunulia china. Ikiwa kama unavyodhania basi flow ya watu kwenda China itapungua sana kibiashara na hii ni itakuwa na economic impact kwa both Tz na China. Ngoja tusubiri ikishafunguliwa but kwa mtazamo wangu pale watafacilitate mambo ya transport, logistics, shipping, marketing and procurement facilities.
Kama watafacilitate transport, logistics, shipping ipi itakuwa nafuu kufanya mfanyabishara mwenyewe au Mchina afacilitate?
 
Bora kama una mill 5 kushuka chini study vizuri alibaba kuna kila kitu mle na verified supplier...mambo ya Matapeli yapo lakini mimi sijawahi tapeliwa hata siku moja nina zaidi ya mwaka naagiza na vitu navoagiza vinafika salama kama nilivoagiza hata nikitaka niuze bei za kariakoo naweza uza...ukipata mtaji mkubwa kama 10 mill na zaidi nenda china...
 
Back
Top Bottom