Fuvu na Mifupa(Skull and Bones) Jamii ya Siri ya Kishetani inayoongoza Matukio ya Duniani

Fuvu na Mifupa(Skull and Bones) Jamii ya Siri ya Kishetani inayoongoza Matukio ya Duniani

Mkuu,ni kweli lakini nashindwa hata niandike kitu gani maana ni mengi sana.Nitajitahidi kufikiria cha kuandika siku moja mkuu ambacho kitakuwa na nyama za kutosha ili msomaji aweze kusoma na kuelewa mkuu....
Usisahau kunitag mkuu
 
hakika thamani ya mwafrika mbele za Mungu imehujumiwa kiasi kikubwa
Mkuu unaposema mwafrica ni mkazi na mzawa wa bara la Africa ambapo ndani ya bara la Africa wapo wazawa ambao ni Arabs,Indians na white mfano nchi za kusini wa Africa kuna wazungu kule ambao wanajitambulisha ni waafrica Kaskazini wa Bara ya Africa kuna waarabu nao wanajitambulisha kuwa ni waafrica

Thamani ya weusi(blacks) ndio wanahujumiwa na Race zingine (Black) hii ndio race ambayo inajumuisha watu weusi wote ambao wako ndani ya Africa na nje ya Africa
 
Mengine ni upuuzi, uzushi na kutisha tu watu, mtu akishasoma kwenye hayo mavitabu na mitandaoni basi mtu anabeba na kuyaamini, sasa mtu anakuambia kuna mji chini ya ardhi, viwanja vya ndege, na trni inayotembea kwa spidi ya light, duh... bado kuna watu wanakuambia mkuu lete nondo, tumieni ata akili ya kawaida kuhoji, mengine hayaingii akilini kabisa
Kuna watu wanavichekesho sana...
 
Madini gani hayo..??? Aliyesema madini yanahusika na rangi ya mtu nani..?

Acha kutudanganya
Hahahah mkuu bora na wewe umekuja, anakuambia mungu hakuumba binadamu aliepungukiwa na chochote, kwahiyo walemavu mungu hakuhusika na uumbaji wao
 
eiyer mimi nataka kuuliza jambo lililo nje ya mada..
maana nmeona umezungumzia mambo ya viumbe..

hivi hawa vampires/zombies
hivi viumbe vipo kweli au ni mpango unaokuja?
maana wamekazana kutuaminisha kupitia movie
 
Hahahah mkuu bora na wewe umekuja, anakuambia mungu hakuumba binadamu aliepungukiwa na chochote, kwahiyo walemavu mungu hakuhusika na uumbaji wao
Nina uhakika alimaanisha Mungu alimuumba binadamu akiwa mkamilifu lakini baada ya kupotea kwenye dhambi matokeo yake ndio kama hivyo kuna; ulemavu,chuki,vita,magonjwa nk.
 
Mkuu Eiyer mimi ni miongoni mwa wasomaji hasa hii post nmejifunza mengi na nmenufaika na mengi kwanza najivunia kuwa mweusi tena kutoka tanganyika leo hii Tanzania...nafurahia urithi wetu,natamani watu wafahamu ukweli na wajikubali kwa kile walichonacho...tukuze vya kwetu tuvithamini na kuvitetea popote pale...Heritage Of Tanzania.
 
Mkuu Eiyer asante kwa darasa..,Ivi sisi weusi tutajikomboa vipi mbele ya hawa wanaoendesha hii dunia
 
Kwangu mimi ninavyoelewa Malaika (wabaya au wema) hawaoi wala kuolewa, hata hivyo hawana jinsia mathayo 22:30 hivyo kauli ya wana wa Mungu kuoana na wana wanadamu Mwanzo 6..haimaanishi Malaika waovu kuoana na wanadamu badala yake humaanisha Wana wa Mungu Waliotokana na kizazi cha sethi watu ambao walishikilia maagizo ya Mungu na wana wa wanadamu wakiwa ni Uzao wa kaini ambao haukufata maagizo ya Mungu..kitendo hki huondoa tofauti kati ya Mungu na shetani 2Wakoritho 6:14...

Kwenye issue ya rangi Mungu hakuumba mtu Mweusi, Kwa sababu jamii ambapo ndo mtu wa kwanza aliumbwa (Middle East) ni weupe na hata Yesu mwenyewe alikuwa Mweupe....
Rangi tofauti ni controversial issue.. lakini bible inadokeza kitu ambacho wakristo wengi wanaamini...Mwanzo 9-10 inadokeza jambo hapo kuhusiana na Nuhu na wanawe, Makosa aliyoyafanya Hamu mtoto wa Nuhu na laana ambayo Nuhu aliitoa kwa mwanae huyo..laana iliyoishia kwa uzao wa Hamu kuwa mtumwa wa ndugu zake wawili (Shemu na Yafethi)...Watoto wa Hamu walikuwa Putu, Kushi na Misri...Wengi huamini kuwa uzao wa Hamu ndo bara la Afrika lilipotokea kwa sababu zifuatazo;

  • Misri ipo bara la Africa
  • Kushi pia anawaklisha Africa, alisambaa kupitia iraq, syria akafika mpaka afrika na inasemekana Sudani na Ethiopia zinawakilisha vizur kabisa ufalme wa kushi.
  • Ukisoma Hesabu 12..utakutana na kisa cha Miriamu na Haruni ndugu zake Musa, walianza kumsengenya Musa sababu kuu ikiwa ni wivu wa madaraka zidi ya ndugu yao, pia sababu nyingine ni kuhusu mke wa Musa inasemekana alikuwa Mweusi (Mkushi) ulikuwa ni ubaguzi wa rangi
  • Katiaka Yeremia 13:23..Mungu anamwambia Yeremia kuhusu mkushi kubadili ngozi yake...hii humaanisha kuwa baadhi ya wazao wa kushi walikuwa na ngozi tofauti na watu wengine, bila shaka walikuwa weusi
  • Katika Matendo 8:26...mtume filipo anaambiwa na malaika aende upande wa kusini (nadhani kusini tunajua kuna bara gani) na huko anakutana na mkushi akirejea nyumbani toka Yerusalemu kuabudu...
  • Bara la Africa ndo bara lilio nyuma kwa kila nyanja ya maendeleo ukilinganisha na mabara mengine...na kwa hakika Africa ni watumwa kabisa, zidi ya mabara mengine...na hii inaleta picha halisi ya laana ya Nuhu miaka melfu iliyopita.
Japo bado nipo kwenye investigation ila hzi sababu nachelea kukubaliana na uwepo wa watu weusi, na pia kama nembo ya laana kimaendeleo kulinganisha na rangi zingine....

Labda kama kuna incovinience sehemu waweza nirekebisha
Mkuu hongera kwa utafiti wako ila ninaomba nibishe nadhalia yako ya ulichosema kuhusu wana wa mungu kujitwalia wake kwa wanadam,anachosema mkuu eiyer ndicho nachokijua nakukiamini,baadhi ya biblia wamekazia hayo maneno mwanz:6 sasa ikawa kwamba hesabu ya wanadamu ilipoanza kuongezeka usoni pa nchi nao wakazaa mabinti, ndipo wana wa Mungu wa kweli wakaanza kuwaona mabinti wa wanadamu kwamba ni wenye sura ya kupendeza; nao wakajichukulia wake, yaani wote waliowachagua.so kimsingi namuunga mkono mkuu eiyer ila nae natofautiana nae aliposema malaika walioasi ndio walizaa na wanawake binadamu hapa nimeweka fungu lote sioni walioasi zaidi ni wana wa mungu wa kweli.
 
Suala au dhana ya kwamba wana wa Mungu ni watoto wa Seth ni assumption ambayo haina back up ya Biblia hata sehemu moja.Dhana hii naifahamu sana na kuna watu wengi wanadhaniahivyo lakini ukweli ni kinyume kabisa kwasababu zifuatazi...

1;Hakuna mahali Mungu aliwakataza wana wa Seth kuoana na wana wa Kaini
2;Hakuna anayeweza kueleza ni kwanini baada ya kuingiliana kwa wana wa Seth na Kaini kingono kukasababisha kuzaliwa viumbe wa ajabu kuliko binadamu
kwasababu Seth na Kaini wote walikuwa ni binadamu wa kawaida kabisa

Kwa upande wangu mimi madai yangu kuwa wana wa MUNGU ni malaika yana back up ya maandiko...

Ayubu 1:6
6 Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao
.

Hao hapo malaika wanaitwa wana wa Mungu.Dhana ya Seth na uzao wake kuwa ni wana wa Mungu ni ya kutunga tu....

Hakuna mahali ambapo biblia inasema kuwa malaika hawana jinsia,andiko uliloleta linasema "hakuna kuoa wala kuolewa kama malaika",kusema hakuna kuoa na kuolewa haimaanishi huna jinsia.Kwa upande mwingine inathibitisha kuwa wana jinsia maana kama wasingekuwa na jinsia wasingetaja kuu ya kutokuwepo kuoa na kuolewa.Mapadri hawaoi,je hawana jinsia kwasababu wamekatazwa kuoa na kuolewa?

Umenifanya nimecheka sana kwa maelezo yako haya.Unatakiwa ujifunze sana juu ya historia ya dunia hii,hapa sizungumzii hiztoria uliyosoma shuleni,nenda zaidi ya hapo...

Usichojua ni kwamba wakazi wa hilo eneo unaloliita wewe kuwa ni mashariki ya kati halikuwa na watu weupe bali weusi na halikuwahi kuitwa "mashariki ya kati" bali lilikuwa linaitwa "North east Africa".Weupe unaowaona eneo hilo walitokea Ulaya na Uturuki na hawakuwa wakazi wa eneo hilo tangu mwanzo na walipofika huko walikuwa wakiwaua sana watu weusi ambao ndiyo walikuwa wakazi halisi wa eneo hili.Historia ya eneo hilo inafanana na ya Misri.Misri haikuwa ya watu weupe bali hao ni watu wa kuja tu..

Kwanza ni kweli kabisa kuwa Hamu alitenda kosa ulilolisema hapo juu na alipewa laana na hao ni wana wake.Sasa jibu hoja zifuatazo...

1;Hao ambao umesoma historia unayoikubali wanakataa kuwa Misri haikuwahi kukaliwa na watu weusi,kama huyo mtoto wa Hamu ambaye ni Misri hakuwa mweusi? Kama alikuwa mweusi inakuwaje hao walioandaa hiyo historia yako wakataa jambo hilo?

2; Kama Misri ilikuwa na watu weusi kama unavyosema halafu Yesu alikuwa mtu mweupe kama unavyodai,inawezekanaje Yesu aje kujificha Misri wakati ule alipokuwa akitafutwa na Herode auwawe wakati akiwa mtoto mchanga ambapo alikimbilia huku yeye na wazazi wake?Inawezekanaje mtu mweupe aje kujificha katikati ya watu weusi na asifahamike?

3; Kama Misri ilikuwa na watu weusi kama ambavyo unadai,iweje mtoto Musa ambaye alikuwa mweupe kwa mtazamo wako aende akalelewe kwenye nyumba ya Farao na asijulikane kuwa ni Muisraeli?

4; Kama Misri ilikuwa inakaliwa na watu weusi ni kwanini ndugu zake Yusuph walishindwa kumtambua ndugu yao walipokwenda Misri kutafuta chakula wakati kwa unavyodai wewe walikuwa ni weupe? Yaani inakuwaje washindwe kumtambua mtu mweupe katikati ya weusi?

5;Kama unakataa kuwa Wamisri wa kale walikuwa siyo weusi maswali yote hapo yanajifia,lakini linazaliwa swali lingine kubwa zaidi ambalo linasambaratisha hoja yako yote ya laana na dhana ya kuwa watoto Hamu walikuwa ni weusi kwasababu kama utasema kuwa Misri hakuwa mweusi ni kwanini udai wengine ni weusi?

6; Kama unadai watoto wa Hamu walikuwa ni weusi,vipi kuhusu mtoto wa Hamu anayeitwa Kanaani ambaye ni baba wa Wakanaani?Waisraeli walipokuwa wanarudi nchi hiyo ya ahadi ambayo ilikuwa inakaliwa na watoto wa Hamu ambao ni Kanaani,walipambana nao,je walikuwa weusi kama watoto wengine wa Hamu? Kama walikuwa weusi ni kwanini unadai watu wa mashariki ya kati walikuwa weupe wakati hao walikuwa weusi? Kama hawakuwa weusi ni kwanini watoto wengine wa Hamu wawe weusi na wengine wasiwe weusi?

Mkuu maswali ni mengi sana na sidhani kama utaweza kuyajibu yote lakini ninachotaka kukueleza tu ni kwamba dhana ya watu weusi kuwa ndiyo watoto wa hamu tu inajifia yenyewe ukiangalia hoja zote nilizokuuliza na nyingine nyiingi sana ambazo sijakuuliza....

Na hoja hizo zinasambaratisha hizo hoja zako zoote ulizoandika hapo juu...

Hoja ya umaskini wa Africa ina majibu yake mengine lakini siyo hiyo dhana yako ambayo ililetwa na hawa hawa weupe ambao wamekufanya na wewe kudhani kuwa Yesu alikuwa mweupe....

Acha nikuchape na haya maneno ya Suleiman hapa kwanza...

Songs of songs 1:5
5 I am black, but comely, O ye daughters of Jerusalem, as the tents of Kedar, as the curtains of Solomon.


Nikutakie tafakari njema....
Mkuu nakuelewa nami nakwambia hao wana wa mungu sio malaika walioasi ndo walizaa na wanawake binadamu
 
Kosa kubwa tunal;olifanya Waafrika ni kufuata historia iliyoandikwa na wakoloni.Wakoloni wanataka tujione na tuonekane washenzi kabisa mbele ya macho yetu na dunia kwa ujumla wake.Wakoloni kama wa Afrika ya kusini walisema kwamba wakati wanafika Johanesbourg miaka 500 iliyopita wanasema walikuta ndege tu waliokuwa na viota vyao maeneo hayo.Wanataka kutufanya kuwa wao ndiyo walioleta "ustaarabu huku kwetu" kitu ambacho siyo kweli kabisa.....

Hivi hatujiulizi kwamba,mtu mweusi alikuwepo kabla ya ujio wa Wakoloni,kwanini historia yetu inaanzia kwenye ujio wa wakoloni na siyo kabla ya hapo?

Kwa mfano katika kitabu cha matendo ya mitume kuna mtu mmoja alitokea huku Afrika aliyekuwa na kitabu cha Isaya akielekea Jerusalem kuabudu,hiyo ilikuwa ni karne ya kwanza na mapema kabisa kwenye 68 A.D.Ni wakoloni walimpa kitabu cha Isaya huyu mtu?

Hatusikii kuhusu jeshi imara kabisa la Afrika lililotaka kuuangusha utawala wa Roma.Hatusikii kuhusu vyuo walivyovikuita huku AFRIKA wakati wanakuja na kutufanya koloni lao,Hawasemi kuwa walipokuja huku walitukuta tumestaarabika kuliko wao,hawasemi ni kwanini walivunja sanamu za wafuasi wa Yesu zilizojengwa na wanafunzi wa wanafunzi wa Yesu waliokuja huku AFrika na kuna wengine walifia huku....

Luka alikuja hadi Libya wakati huo ikiwa na watu weusi kabisa.Waarabu wakati wanakuja huku walikuta Ukristo upo zamani hata kabla ya ujio wa wakoloni lakini tunaamini wakoloni ndiyo wamekuja kutuletea "akili",inasikitisha sana....

Mkuu huwezi kutegemea adui yako akutengenezee kitu bora kwaajili yako,atakutengenezea kinachomtukuza yeye tu.Sisi Waafrika hatujui tu lakini hakuna anayetupenda hapa duniani kwasababu sisi ndiyo binadamu bora na tuliokamilika kuliko wengine wote....

Siku tukiujua ukweli huu tutarudia enzi zetu ambazo tuliitawala dunia,nadhani hili hulijui lakini tulishaitawala dunia miaka mingi tu.Mfano wa kuliona hili ni Misri,hii ilikuwa ni falme na super power ya watu weusi kabisa na ni mamlaka iliyodumu miaka mingi sana tena miaka ya 3000 B.C huko lakini bado tunajidharau tu na kuamini tulielimishwa na wakoloni....

Mkuu tujisomee sana ili tujiokoe kwenye huu upuuzi wa kuamini kuwa wakoloni ndiyo waliokuja kutuelimisha...
d0ba53b03ea3ca35f807212fe721c1bd.jpg
 
Mkuu Wangu Eiyer naomba nikopy post yako namba 219., naiweka kwa cm na pc for my own references. imenisafisha macho kweri kweri, naisoma mara ya sita saizi,
 
Back
Top Bottom