CM 1774858
JF-Expert Member
- May 29, 2021
- 5,621
- 5,029
||FY2021|22 Rais Samia kutoa Jumla ya Trilioni 11 kulipa madeni ya nyuma yaliyoaachwa na mtangulizi wale,
===Rais Samia Suluhu Hassan kimyakimya ameendelea kulipa madeni mbalimbali kwa makampuni binafsi au taasisi.
Kwakuanzia tu mwaka huu pekee Rais Samia analipa madeni yenye thamani ya Jumla ya zaidi ya TZS11.17623Trilioni.
Watanzania mnapoambiwa Rais Samia ni levels zingine muelewe pamoja na kulipa madeni yote haya miradi yote ya maendeleo Mipya na yazamani inaendelea kwa speed, Pitia hii listi ya malipo
1 . Mama ametoa Jumla ya fedha kiasi cha TZS 111.41BL ili kuwalipa watumishi wa Serikali wanaoidai Serikali,
Tunafahamu malipo haya yataongeza ari na nguvu zaidi kwa watumishi hawa wa Serikali kufanya kazi kwa bidii na maarifa ili kuwatumikia Watanzania ambao ndio waajiri wao, Je! hili si jambo jema?
2. Mama ametoa Jumla ya fedha kiasi cha TZS 264.23BL kwaajili ya kuwalipa wakandarasi wetu mbalimbali wa nje na ndani waliokuwa wanaidai Serikali.
Hii itaongeza imani na uaminifu kwao katika kuendelea kutoa huduma kwa Serikali yetu ya JMT, Je! hili si jambo jema?
3. Mama ametoa Jumla ya fedha kiasi cha TZS 70.49BL kwaajili ya kuwalipa Wazabuni wetu mbalimbali waliotoa bidhaa na huduma kwa Serikali yetu.
Sote ni mashahidi Wazabuni wengi walikuwa wakilalamika kudaiwa mikopo benki naamini wamefuraha sasa na Wataendelea kutekeleza ilani ya CCM ya 2020-2025 bila kinyongo, Je! hili si jambo jema?
4. Mama ametoa Jumla ya fedha kiasi cha TZS 2.17BL ili kuwalipa watoa huduma mbalimbali waliokuwa wanaidai Serikali kutoka katika Wizara mbalimbali.
Hakika mama huyu anajicho la pekee kama hujaelewa unakwenda wapi na Rais Samia basi ni wazi wewe hujui unakotaka kwenda-Je! hili si jambo jema?
5. Mama ametoa Jumla ya fedha kiasi cha TZS 67.93BL kwaajili ya hukumu na fidia mbalimbali ambazo Serikali inadaiwa baada ya kushindwa kesi mbalimbali ili kutengeneza imani kwa wawekezaji wa ndani na nje pamoja na watu binafsi,Je! hili si jambo jema?
6. Mama ametoa Jumla ya fedha kiasi cha TZS 10.66Trilioni ili kulipia deni la Serikali pamoja na mikopo mingine kwa uwezo wa Manani kupitia Rais Samia na timu yake tutafika tena kwa kuwahi sana.
Je, hili si jambo jema?