FY2021/22 Serikali kutoa Trilioni 11 kulipa madeni ya nyuma

FY2021/22 Serikali kutoa Trilioni 11 kulipa madeni ya nyuma

Samia mwisho wake ni 2015.

Hayo mafeni yameletwa na chama gani? Hata yeye bado ataacha madeni mengi tu, kwa hiyo atakae chukua nchi baada yake na yeye ajisifu, sio? Ama hiyo mikopo atailipa kabla hajaondoka?

Ccm hata wakipewa miaka 1000 ngonjera ni hizi hizi.
Uchaguzi wa 2025 tayari CCM ilishashinda kabla ya Uchaguzi kuanza Pole sana " roho mbaya "
 
Ninafikiri huyu ni Samia mwenyewe anajipigia promo..maana post zake ni kujikweza tuuu mwanzo mwisho.

Fanya kazi mama, ni wajibu wako. Huna sababu ya kujinadi kiasi hicho.
Kibaya kinajitembeza ila kizuri siku zote hujiuza.
niwapi kasifiwa Rais hapa,Chadema mtateseka sana kwa speed ya mama,
 
Chama kinakopa tangu lini wewe CHADEMA,
Madeni ni kwa maendeleo ya nchi,
Hayo madeni hata wewe yamekunufaisha kwa namna moja ama nyingine,

Hongera Sana Rais Samia tuko nawewe sana tu,
CHADEMA kilishakufa kitambo sana,
 
kutokana na Deni la taifa kupaaa, tunaiomba Serikali ihakikishe inadhibiti na kubana matumizi yasiyo ya lazima kwa mfano;

1. Safari za nje zisizo za lazima zizuiwe/zipunguzwe.

2. Vikao vya Bunge vipunguzwe, ratiba ya vikao iangaliwe upya kuanzia mwakani.

3. Matumizi ya magari ya V9/v8 ambayo ni gharama kubwa kuyahudumia,

4. Semina na vikao visivyo vya lazima vipunguzwe.

5. Mishara mikubwa kwa baadhi ya watendaji ipunguzwe, isiwe zaidi ya milioni 10 kwa mtendaji 1.
maana kuna baadhi ya taasisi za serikali watu wanalipwa hadi milioni 15 kwa mwezi.

Kama kweli Serikali yetu pamoja na watendaji wake wana uchungu na watanzania basi lazima wafanye kitu ili kuinisuru nchi na kuelemewa na madeni.

haiwezekani nchi imeandamwa na madeni mpaka puani halafu kuna baadhi ya watu/watendaji wanazidi kunyonya tu bila huruma.
hapana, tunataka kuona hatua zinachukuliwa haraka.
 
Rais Samia Suluhu Hassan kimyakimya analipa madeni mbalimbali aliyoyakuta na kwa kuanza kwa mwaka huu pekee analipa madeni yenye Jumla ya TZS11.17623Trilioni,Mnapoambiwa Rais Samia huyu ni levels zingine muelewe na mumuombee mzigo huu ni mzito sana mabegani mwake na unahitaji neema ya Mungu,

1 . Mama ametoa TZS 111.41BL ili kuwalipa watumishi wa Serikali wanaoidai Serikali,malipo haya yataongeza ari na nguvu za watumishi hawa katika kufanya kazi kwa bidii na maarifa ili kuwatumikia Watanzania ambao ndio waajiri wao,

2. Mama ametoa Jumla ya fedha TZS 264.23BL kwaajili ya kuwalipa wakandarasi mbalimbali wa nje na ndani waliokuwa wanaidai Serikali ili kuongeza imani na uaminifu kwao katika kuendelea kutoa huduma kwa Serikali yetu ya JMT,

3. Mama ametoa Jumla ya fedha TZS 70.49BL kwaajili ya kuwalipa Wazabuni mbalimbali waliotoa bidhaa na huduma kwa Serikal,wote mtakumbuka Wazabuni wengi walikuwa wanalalamika kudaiwa mikopo benki naamini wamefuraha sasa na Wataendelea kutekeleza ilani ya CCM ya 2020-2025 bila kinyongo,

4. Mama ametoa TZS 2.17BL ili kuwalipa watoa huduma mbalimbali waliokuwa wanaidai Serikali kutoka katika Wizara mbalimbali,Hakika mama huyu anajicho la pekee kama hujaelewa unakwenda wapi na Rais Samia basi ni wazi wewe utakuwa hujui unakotaka kwenda,

5. Mama ametoa Jumla ya fedha TZS 67.93BL kwaajili ya hukumu na fidia mbalimbali ambazo Serikali inadaiwa baada ya kushindwa kesi mbalimbali ili kutengeneza imani kwa wawekezaji wa ndani na nje pamoja na watu binafsi,

6. Mama ametoa jumla ya fedha TZS 10.66Trilioni ili kulipia deni la Serikali pamoja na mikopo mingine hakika mzigo ni mkubwa ila kwa uwezo wa Manani kupitia Rais Samia tutafika tena kwa kuwahi,


View attachment 2003891
Wakandarasi vicheko,
Wazabuni vicheko,
Watumishi vicheko,
Watoa huduma vicheko,

Tuacheni utani huyu mama anapiga kazi sana tu,
 
tafuta namna nyingine ya kumpongezq mama,sio inshu ya madeni ,mwal.aliacha madeni,mwinyi aliacha madeni,mkapa aliacha madeni ,jk pia.hakuna ambae ataweza kuyamaliza au kutokukopa.tunachotaka maendeleo basi
 
kutokana na Deni la taifa kupaaa, tinaiomba Serikali ihakikishe inadhibiti na kubana matumizi yasiyo ya lazima kwa mfano;

1. Safari za nje zisizo za lazima zizuiwe/zipunguzwe.

2. Vikao vya Bunge zipunguzwe, ratiba ya vikao iangaliwe upya kuanzia mwakani.

3. Matumizi ya magari ya V9/v8 ambayo ni gharama kubwa kuyahudumia,

4. Semina na vikao visivyo vya lazima vipunguzwe.

5. Mishara mikubwa kwa baadhi ya watendaji ipunguzwe, isiwe zaidi ya milioni 10 kwa mtendaji 1.
maana kuna baadhi ya taasisi za serikali watu wanalipwa hadi milioni 15 kwa mwezi.

Kama kweli Serikali yetu pamoja na watendaji wake wana uchungu na watanzania basi lazima wafanye kitu ili kuinisuru nchi na kuelemewa na madeni.

haiwezekani nchi imeandamwa na madeni mpaka puani halafu kuna baadhi ya watu/watendaji wanazidi kunyonya tu bila huruma.
hapana, tunataka kuona hatua zinachukuliwa haraka.
Naungana na wewe kwa 100% kwenye hili
 
Tulisema tukaonekana wendawazimu, Leo nyie ndio mmethibitisha kuwa MNA matatizo makubwa, niwakumbushe tu kuwa jengeni mifumo na sio mtu, SSH akiondoka mtamsema pia. Samia hatoi pesa na wala haipaswi kutamkwa hivyo ila kwakua ujuaji mwingi hamtakubali

Naungana na wewe mia kwa mia ili nchi iwe na Maendeleo endelevu ni lazima kuwepo na TAASISI IMARA [ STRONG INSTITUTIONS] ambazo zitaleta maendeleo kwa nchi hata kama kutakuwa na mabadiliko ya uongozi!!!

Mnarudia makosa yale yale ya kufikiri Magufuli alikuwa anatoa fedha mifukoni mwake kumbe ni kodi zenu!!
 
tafuta namna nyingine ya kumpongezq mama,sio inshu ya madeni ,mwal.aliacha madeni,mwinyi aliacha madeni,mkapa aliacha madeni ,jk pia.hakuna ambae ataweza kuyamaliza au kutokukopa.tunachotaka maendeleo basi
Daah madeni ya watumishi,
Daah madeni ya wazabuni,
Daah madeni ya wakandarasi
Daah madeni ya watoa huduma

Kweli haya yaliachwa na Mwl, Mwinyi,Mkapa na JK,??!!

KWANINI HAMTAKI KUONA UIMARA WA MAMA?
 
Mama ametoa,mama ametoa.
Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.
 
Naona watu wamejipanga kweli kweli kwenye hili
Siasa ni hatari sana
 
Samia mwisho wake ni 2015.

Hayo mafeni yameletwa na chama gani? Hata yeye bado ataacha madeni mengi tu, kwa hiyo atakae chukua nchi baada yake na yeye ajisifu, sio? Ama hiyo mikopo atailipa kabla hajaondoka?

Ccm hata wakipewa miaka 1000 ngonjera ni hizi hizi.
Madeni mpaka China na USA wanadaiwa. Hawapati madeni kwa nia ya kujifurahisha tu ni katika kutimizamalengo ya muda mfupi na mrefu.
 
kutokana na Deni la taifa kupaaa, tinaiomba Serikali ihakikishe inadhibiti na kubana matumizi yasiyo ya lazima kwa mfano;

1. Safari za nje zisizo za lazima zizuiwe/zipunguzwe.

2. Vikao vya Bunge zipunguzwe, ratiba ya vikao iangaliwe upya kuanzia mwakani.

3. Matumizi ya magari ya V9/v8 ambayo ni gharama kubwa kuyahudumia,

4. Semina na vikao visivyo vya lazima vipunguzwe.

5. Mishara mikubwa kwa baadhi ya watendaji ipunguzwe, isiwe zaidi ya milioni 10 kwa mtendaji 1.
maana kuna baadhi ya taasisi za serikali watu wanalipwa hadi milioni 15 kwa mwezi.

Kama kweli Serikali yetu pamoja na watendaji wake wana uchungu na watanzania basi lazima wafanye kitu ili kuinisuru nchi na kuelemewa na madeni.

haiwezekani nchi imeandamwa na madeni mpaka puani halafu kuna baadhi ya watu/watendaji wanazidi kunyonya tu bila huruma.
hapana, tunataka kuona hatua zinachukuliwa haraka.
Unayohoja hoja mkuu ila usiogope deni ni stahimilivu kwa kipindi kifupi, chakati na kirefu hii ni kimataifa so relax nchi iko salama sana,
 
Back
Top Bottom