G7 yapiga marufuku ununuzi wa mafuta Urusi

G7 yapiga marufuku ununuzi wa mafuta Urusi

Kesho utasikia
"Hatuwezi kususia mafuta na gas kutoka Russia, ili kulinda uchumi wa ujeruman na watu wake" Chancellor wa ujeruman.

"Japan haiwezi kuachana na mradi wake wa bomba la mafuta kutoka urusi, kwasababu ni mradi wenye masilahi mapana kwa uchumi wa taifa letu"

"USA yaendelea kuagiza mafuta Urusi japo imepunguza asilimia kama njia moja wapo ya kutounga uvamizi wa urusi nchini Ukraine" White house.

Hiyo ndo nguvu ya G7 inayopelekwa mputa mputa na Nguvu ya giant mmoja anaejulikana kama G1 A.k.A jeshi la mtu mmoja.
👏👏👏👏🤜
 
Kama wanaweka vikwazo, Ili tuwaone wako sirious wangeweka na vikwazo vya kuagiza mbolea na Gas kutoka Russia. Lakini hicho wanqchofanya ni unafiki kwa UKRAINE, wapeleke na majeshi yao kabisa wamtoe PUTIN Ukraine wamfuate mpaka Russia wamchakaze Ili asirudie kwa nchi nyingine. Tofauti nahapo wanafanya unafiki wakumkopesha silaha Ukraine Ili OP ikiisha waangalie namna gani watalipwa.
Unafahamu chanzo cha mzozo huu? Si Russia hataki Ukraine ijiunge na NATO akihofia military base kujengwa Ukraine hasa military base ya US?

Sasa kwa mfano huohuo uliotoa, wa NATO kwenda kuingia mazima Ukraine na kumtoa Putin, umejiuliza kwanini Putin yeye asimpige US ambae ndie anamshawishi Ukraine?

Putin hakutoa onyo kwa taifa litakalosaidia Ukraine kuwa atayaangamiza? Niambie nchi gani ambayo haifahamiki kama inaisaidia Ukraine. Poland amepeleka vifaru ndani ya siku mbili tatu, na ni jiran tu hapo, bado finland n.k uko UK, US, German ndo kabisaaa sasa kwanini asitekeleze kiapo chake?

Hii ni vita, na mpaka inatokea hivi ujue kuwa kuna intelligence zilifanya kazi kwa kujiandaa na matukio haya, NATO walijua ipo siku moto utawaka dhidi ya Russia, na Russia alishajiandaa ipo siku moto utawaka dhidi ya NATO. Sasa hapo unaposema kwanini wasiweke vikwazo dhidi ya gas na mbolea, ni suala la muda tu. Kumbuka nimekwambia kuna taasisi mbili hapo zinachuana.

Unajua mali za mabosi wa russia zilizoshikwa huko nje? Hasara Russia alopata Ukraine umefatilia? Russia angekuwa yeye anajua ameshika maisha ya NATO hata kwa 80% tayari na yeye angeshatia vikwazo kwa NATO.

Kitendo ch Putin kutoa tamko la kuzima vyombo vya habari kuripot mambo negative kuhusu operation, kumefanya mambo mengi ya ajabu yanayotokea russia yasifahamike moja kwa moja, ila huko pia mambo ni mabaya. Moscow imepoteza ajira 200,000, laki mbiliiiii baada ya mataifa ya NATO kufunga makampuni yao hapo.
 
Urusi inabidi baada ya huu mgogoro aungane na uchina uisaidia afrika isimame kiuchumi na kupata back up ya kutosha maana mataifa yaliyobakia tayari yameanza kupata mbavu mdogo mdogo imebakia tu afrika.

Afrika iache kujitazama kama mataifa madogo madogo bali kama taifa moja kubwa na mataifa madogo kama mikoa au majimbo.

Ni muda muafaka sasa wa kuvimbia mataifa ya kimagharibi wanapokuja na sheria au hoja zao za kulazimishia.

Mataifa ya magharibi yakiongozwa na mnafiki namba moja US yamekuwa kikwazo kikubwa sana cha maendeleo ya kiuchumi kwa mataifa changa kama Tanzania na wengineo kupitia sera zake ambazo huwa na maneno matamu ila matokeo yasiyo na faida siku za mbeleni.
 
Ukiwa na mafuta duniani uwezi ukafa njaa hata siku moja msituongopee kabisa maana wewe ukisusa kununua wenzako wananunua na maisha yanaendelea.
Sasa kipindi hiki si ndiyo Mama aagize Mafuta kutoka Urusi moja kwa moja, maana wanunuzi wengine wamesusa kwa sababu zao binafsi,na soko litakua chini kidogo!!?
 
Sijui watu tatizo ni shule au ni nini, kwani kati ya muuzaji na mnunuzi, anayemhitaji mwenzie zaidi ni nani? Si anayeuza? Tafsir ya kuuza ni kwamba wewe una uhitaji, usipokuwa na uhitaji huwezi kuuza.

Russia ktk hili ndio muathirika zaidi, ni vile tu nchini kwake vyombo vya habari vyote vimezimwa kutoa ripoy negative ktk hii inayoitwa operation.

Hawa vijana wanaojiita mashabiki wa putin wanapaswa kutazama hili sakata kwa mapana.
Tatizo tunabishana na watoto wadogo hawajui maisha bado wanakaa kwa shemeji, Mimi ni mfanyi biashara na siku zote sinaga jeuri mbele ya mteja hata akaja vipi.
Mtu anakuja dukani na stress zake za maisha lakini bado nitamuuzia manake nahitaji pesa zake.
Mteja ndio bosi na bosi hagomewi , urussi anahitaji sana hizo pesa za magharabi zaidi ya wanavyohitaji bidhaa zake na ndio maana akina EU na Marekani wanajeuri kumliko.
Kama kweli yeye dume afunge biashara nao alafu tuone hapo Moscow patakalika.
 
Wakubwa wa dunia hawanunui mafuta kwa sababu wanayo ya kutosha kwann seriakl yetu isende urusi kununua mafuta tena bei rahis tu kuliko kutujazia huku mabei na Tz hatupo upande wowote wa vita 😮
 
Hii ndio opportunity ya mataifa ya afrika kujipanga na kuweka sawa mifumo yao ya kiuchumi na kupunguza western influence.

Western influence kwenye mambo yetu ya ndani ina dhoofisha sana maendeleo yetu.
 
Sijui watu tatizo ni shule au ni nini, kwani kati ya muuzaji na mnunuzi, anayemhitaji mwenzie zaidi ni nani? Si anayeuza? Tafsir ya kuuza ni kwamba wewe una uhitaji, usipokuwa na uhitaji huwezi kuuza.

Russia ktk hili ndio muathirika zaidi, ni vile tu nchini kwake vyombo vya habari vyote vimezimwa kutoa ripoy negative ktk hii inayoitwa operation.

Hawa vijana wanaojiita mashabiki wa putin wanapaswa kutazama hili sakata kwa mapana.
Washabiki wenyewe ni akina bwana utam wanaelewa nini zaidi ya ushabiki?
 
Kesho utasikia
"Hatuwezi kususia mafuta na gas kutoka Russia, ili kulinda uchumi wa ujeruman na watu wake" Chancellor wa ujeruman.

"Japan haiwezi kuachana na mradi wake wa bomba la mafuta kutoka urusi, kwasababu ni mradi wenye masilahi mapana kwa uchumi wa taifa letu"

"USA yaendelea kuagiza mafuta Urusi japo imepunguza asilimia kama njia moja wapo ya kutounga uvamizi wa urusi nchini Ukraine" White house.

Hiyo ndo nguvu ya G7 inayopelekwa mputa mputa na Nguvu ya giant mmoja anaejulikana kama G1 A.k.A jeshi la mtu mmoja.
Siku zote mashabiki huwa wachezaji wazuri kuliko wachezaji wenyewe walioko uwanjani.
Sikushangai hii ni bongo
 
Kesho utasikia
"Hatuwezi kususia mafuta na gas kutoka Russia, ili kulinda uchumi wa ujeruman na watu wake" Chancellor wa ujeruman.

"Japan haiwezi kuachana na mradi wake wa bomba la mafuta kutoka urusi, kwasababu ni mradi wenye masilahi mapana kwa uchumi wa taifa letu"

"USA yaendelea kuagiza mafuta Urusi japo imepunguza asilimia kama njia moja wapo ya kutounga uvamizi wa urusi nchini Ukraine" White house.

Hiyo ndo nguvu ya G7 inayopelekwa mputa mputa na Nguvu ya giant mmoja anaejulikana kama G1 A.k.A jeshi la mtu mmoja.
Tatzo pro rusia wengi Wana uelewa mdogo. Kama rusia ni mbabe si akatae kuwauszia kama. Anajitisheleza. Make NATO na USA wao hua wanakupiga burn. Hawakuuzii kabisa. Rusia anabweka lkn anawauzia. Si akatae ili tuone ubabe wake.

Tambua kua uchumi wa Russia ni mdogo mno. Putin akili yote. Uwezo wote kawekeza kwenye jeshi. Hahangaiki kuimarisha uchum

Sent from my TECNO KG6 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom