Gari yangu inakimbia sana!

Mlolongo

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2019
Posts
3,483
Reaction score
6,257
Kuna project naisimamia pale Kibaha Mailimoja. Kwahiyo route za kutoka Makongo Juu kwenda Kibaha na kurudi daily hazikatiki. Zile njia sita kutoka Kimara hadi Mailimoja zimenipa nafasi kujua kumbe gari yangu inakimbia mazee.

Gari yenyewe ujue ni gari gani basi?

Ni Passo Racy, 1290CC. Ni ya mwaka 2007.

Kwa data nilizonazo (kwa kipindi cha miezi mitatu), nimegundua yafuatayo:

A: Gari nazozionea road, nawakimbiza nawaachia vumbi:
  • IST zote
  • Sienta, Raum, Runx, Allex, Swift, Nadia, Voltz (tuseme babywoka zote za Toyota)
  • Premio na mwenzie Allion
  • Nissan Dualis na X-trail
  • Rumion
  • RAV4 zote (isipokua lile toleo jipya linatumiwa na gari za serikali na ile Hybrid)

B: Gari ambazo nimeshindwa kufukuzana nazo:
  • Subaru Forester (model karibu zote)
  • Ford Ranger (hii gari noma)
  • Toyota Hilux
  • Landcruiser (VX na jamii yake)
  • ALPHARD (toleo jipya)
  • Toyota Fortune
  • Discovery
  • BMW (japo kuna baadhi navimbiana nao)
  • Toyota Crown
  • Brevis
C: Gari nazokwenda nazo ugoko kwa ugoko:
  • Harrier na Vanguard
  • Range Rover
  • Subaru Impreza

Sasa hivi focus yangu nijipime na kina Audi, Benz, Volkswagen and the like. Tatizo European cars nazokutana nazo barabarani ni chache sana. Halafu huwa nakutana nazo mida ambayo sipo kwenye kuanzisha ligi.

Changamoto nayopata ni gari inachelewa kuchanganya. Hasa pale taa zikiruhusu ndio wengi wanaponipiga bao. Lakini ikishachanganya nawapoteza karibu wote (ukitoa hao wa kwenye kundi B).

 
Weee bwana! Unadai gari yako inakimbia kuzidi nyingine kwa kigezo kipi? Kwani mlikubaliana na wenzako barabarani mshindane? Dash board yako imeandikwa max speed ni ngapi zaidi ya gari ulizozitaja? Zaidi ni 180km/h kama magari mengine. Ikizidi sana kwa magari ninayoyajua ni speed 240km/h. Kijana! Kumbuka usemi usemao: usijisifu unajua kukimbia, msifu unayekimbizana naye!
 
Eti, mtu anaendesha kwa mwendo wake, barabarani, amkipita tayari gari yake inakimbia kuliko zingine.
 
Mkuu umeshawahi kuendesha safari ndefu? Kwasababu kutoka DAR - kibaha hakuna sehemu unaweza kufikia speed 160.
Hiyo ligi unayofanya ni ndogo Sana huwezi kutunisha misuli na premio, rumion,dualis,X trail wala RAV4.....
sidhani kama unaijua vizuri RAV4
 
Nimeshangaa sana, Rav 4 hata zile Old zina mwendo sana.
 
Kifo kinakuita
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…