Gaudensia Kabaka Mwenyekiti wa UWT?

Barbara! Wamama was Pwani walikiona kidume Cha kwenfa UNO niJulius😅
 
Kwa maswali uliyomaalizia hapo chini mjadala huu utakuacha!
 
Hilo la kuwa mlipigania Uhuru hatuna mashaka nalo...Sasa mlitaka mpewe zawadi gani zaidi ya hii kiwa no wapigania Uhuru!
Au mlikuwa mnapigania Dini!?
 
Kwa maswali uliyomaalizia hapo chini mjadala huu utakuacha!
Sawa ila time factor ni muhimu ila Lombo unakataa tu, binafsi bado nasubiri majibu na ufafanuzi wa hili suala; vinginevyo nitabaki na dhana yangu kuwa SI KWELI NA NI UZUSHI TU.
 
Huyo unaemtukana anatuzo zaidi ya 10 za heshima
 
Kama hawakwenda basi ujue hawakufaulu,inamaana hawana akili kama ulivyosema.

Sent using Jamii Forums mobile app
Saint...
Mimi nilipompelekea huyu mtaalamu hii data nikamwambia tu-assume kuwa hawa vijana wa Kiislam hawana uwezo na ndiyo maana wakashindwa kupasi.

Yeye akaniuliza maswali mengi lakini akaniambia kuwa akifanya analysisi katika law of probability inakataa hili haliwezi kuwa.

Akaendelea kuniambia kuwa mfano wake ni kama pyramid katika matokea ya mitihani kuwa juu wanakuwa wachache na chini wengi.

Mimi sikushindwa nikawa namuuliza maswali mengi na yeye aknipa majibu kitaalamu.
Alinichekesha aliponiambia kuwa hayo matokeo ya Tanzania ingekuwa ni kweli hakuna ''foul play,'' ingekuwa imeanzisha '' unique law,'' natungeingia katika vitabu vya dunia kwa uvumbuzi mpya.

Mwisho nikamuonyesha utafiti ambao ulifanywa na Warsha mwaka wa 1981 kuhusu elimu Tanzania.

Jibu aliloniletea nilicheka.

''Foul play.
Mohamed you have all the answers and yet you want to waste my time!''

Huyu sahib yangu yeye ni ''educationist,'' akaniambia kuwa ananishukuru kwa kumpa topic ambayo ataitumia kwa wanafunzi wake.
 
Hilo la kuwa mlipigania Uhuru hatuna mashaka nalo...Sasa mlitaka mpewe zawadi gani zaidi ya hii kiwa no wapigania Uhuru!
Au mlikuwa mnapigania Dini!?
Lombo,
Tatizo ni kuwa historia ilipotoshwa ndiyo maana nikaamua kuandika kitabu cha Abdul Sykes.
 
Hizo analysis za probability kama vijana hawasomi lazima zikatae mzee.

Ujanja ni kusoma.


Mtihani hauna dini ule mzee(ukitoa Bible knowledge na Islamic knowledge)

Vijana wasiposoma,haijalishi wapo wengi au wachache kiasi Gani,watafeli tu.
Una miaka mingapi mzee?
Naona kichwa chako kishavurugika..



Kuishi kwingi ni kuona mengi,ila wewe naona akili ishaanza kuzeeka .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Barbara! Wamama was Pwani walikiona kidume Cha kwenfa UNO niJulius😅
Lombo,
Uwezo wa Julius Nyerere ni wazi na akina mama ndiyo wanachama wa mwanzo wa TANU kuunga mkono harakati za ukombozi.

Chiku bint Said Kisusa mjukuu wake ndiye aliyemvisha shada la maua Nyerere aliporejea UNO.

Mumewe ni Shariff Abdallah Omar Attas.

Shariff Attas alikuwa Mkusanyaji Ushuru wa nafaka Kariakoo Market ambako Abdul Sykes alikuwa Market Master.

Shariff Abdallah Attas wakati ule Nyerere kaacha kazi yuko kwa Abdul Sykes ilikuwa Mwalimu akisha kunywa chai anakuja Kariakoo Market ofisini kwa Abdul Sykes.

Pale kulikuwa na chumba ambacho kulikuwa na magazeti na vitabu Mwalimu alikuwa akikaa pale kujisomea na kukutana na watu.

Mchana anaongozana na Shariff Attas kwenda nyumbani kwa Mama Daisy, mkewe Abdul Sykes kwa chakula cha mchana.

Baada ya kula wanapumzika kidogo kisha pamoja wanarudi ofisini kwa Abdul Sykes.

Bi. Chiku akafahamiana na Mama Maria na wakawa mashoga wakubwa.

Kuna historia kubwa sana.

Kadi za TANU za kwanza ziliuzwa hapo Kariakoo Market.

Laiti kama nisingeandika kitabu cha Abdul Sykes haya yote yangepotea.


Kariakoo Market na ofisi ya Abdul Sykes ni hiyo nyumba ndogo kulia.
 
Hizo analysis za probability kama vijana hawasomi lazima zikatae mzee.

Ujanja ni kusoma...
Saint...
Ahsante hii ni data nitamrushia sahib yangu nisikilize atasema nini.
Hakika kuishi kwingi ni kuona mengi.

Nina miaka 69 nakimbilia 70 In Sha Allah February 2022

Mimi ni mzee sasa na uzee unajenga ustahamilivu ndiyo maana unanikejeli katika jambo la kisomi sighadhibiki naendelea kujadiliana na wewe.

Hizi data nilizokupa wewe vijana kama wewe waliniuliza maswali mengi sana kufikia kutaka niwapatie script za mitihani.

Hili nililifikisha kwa wenzangu wao jibu lao lilikuwa hapana haja tusitafute makubwa mradi jambo hili lishazungumzwa Bungeni na Hansard imerekodi inatosha.

Nadhani umeona tofauti kati yako na vijana wenzio.

Wewe unakejeli tena unamkejeli mzee wenzako wanaona nimewaletea topic ya research wanataka kujua nini kimetokea kiasi papatikane matokeo kama yale.

NB
Sahib yangu kaniletea majibu comment zako kwangu.
Kaniuliza kiwango cha elimu ya ''subject.''

Subject anakukusudia wewe.
Mimi nimemjibu kuwa sijui na siwezi kukuuliza.

Nasubiri jibu lake nitakutaarifu.
Angalia vichwa vya wenzetu vinavyofanya kazi.

Keshakufungulia jalada na kalipa jina ''Subject''
 
Basi yaishe Moderators futa hii makitu inaleta uchonganishi tu wa kidini
 
Unachanganya elimu na dini mzee wangu.
Watoto wafeli usingizie eti dini Yao!
Hizi ni porojo mzee wangu.


Ukilaza hauhusiani na dini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unachanganya elimu na dini mzee wangu.
Watoto wafeli usingizie eti dini Yao!
Hizi ni porojo mzee wangu.


Ukilaza hauhusiani na dini.

Sent using Jamii Forums mobile app
Saint...
Sahib wangu ananiuliza ikiwa watendaji wa serikali huwa wana majibu kama yako wanapokabiliwa na matatizo kama haya?

Jibu langu nimemwambia kuwa hili ni jambo nyeti sana na serikali wana msimamo wa kunyamaza kimya.
 
Saint...
Sahib wangu ananiuliza ikiwa watendaji wa serikali huwa wana majibu kama yako wanapokabiliwa na matatizo kama haya?

Jibu langu nimemwambia kuwa hili ni jambo nyeti sana na serikali wana msimamo wa kunyamaza kimya.
Endeleeni kuota.
Watoto wenu wa kiislam wasiposoma wataendelea kushika mikia na kuwa vilaza.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Basi yaishe Moderators futa hii makitu inaleta uchonganishi tu wa kidini
Mwana...
Uzi huu umevutia watu wengi sana.
Wanakuja kusikiliza.

Itakuwa si busara kuufuta kwa haraka.
Mimi nina mengi sana ya kueleza kwa faida ya taifa letu.

Mimi ningekuomba uwaombe wachangiaji wachangie kwa heshima na adabu ili mjadala ustawi.
 
Endeleeni kuota.
Watoto wenu wa kiislam wasiposoma wataendelea kushika mikia na kuwa vilaza.

Sent using Jamii Forums mobile app
Saint...
Hapana hatuoti.

Tulikuwa na mipango mizuri sana ya elimu chini ya EAMWS na tukafikia kutaka kujenga Chuo Kikuu lakini EAMWS ikapigwa marufuku na serikali na kuundwa BAKWATA.

Huu ukawa mwisho wa mipango yetu ya elimu.

Juu ya haya hatukukata tamaa tukajenga shule kila mtu pale alipo na hizi ndizo shule zilizohujumiwa na NECTA na tukaandamana.

Nimekieleza kisa hiki hapa.
Ushahidi wa mandamano hayo na hisia za Waislam ni hizo hapo chini kwenye picha:



Moja ya bango katika maandamano ya kupinga NECTA.
Unachanganya elimu na dini mzee wangu.
Watoto wafeli usingizie eti dini Yao!
Hizi ni porojo mzee wangu.


Ukilaza hauhusiani na dini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jones...
Mimi hapa niko darasani nasomesha yale ambayo wengi hamkuwa mkiyajua
Sijawawahi kuona mwalimu anayefundisha mambo kwa bias. Usifundishe kinachokufurahisha wewe fundisha kinachofanya jamii ielewe kwa mapana yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…