TANZIA Gavana mstaafu wa BoT, Profesa Benno Ndulu afariki dunia

TANZIA Gavana mstaafu wa BoT, Profesa Benno Ndulu afariki dunia

... tatizo tumezoea vifo vya mapema hadi tunaona kawaida. Life expectancy (2018) za wengine hizo hapo Mkuu; tunastahili kuishi sio kufa - Sweden - 82.56; Norway - 82.76; Finland - 81.73; Denmark - 80.95; Japan - 84.21; UK - 81.26; US - 78.54; France - 82.72.

Ni wajibu wa serikali inayoongozwa na CCM kutuvusha tufikie level hizo za kuishi/umri. Kuboresha maisha ya wananchi ni jukumu la serikali yoyote inayojali.
Kwa Afrika miaka 71 ni mingi sana iko kwenye range ya vitabu vya dini kabisa
 
Kwani Kichuguu, mna arllegy na Corona ?!. Siwaelewi !!
Hii kitu inaua kinyama tena walipa kodi wazuri . Nawashangaa
Post yangu ya wali ilificha neno moja lililoharibu maana ya post yote; hebu isome tena ndipo tunazie hapo.
 
Kuna watu wanafuraaaaahi kusikia hivi vifo. R.I.P
Inaweza ikawa ni fikra zako, kwa sababu dhamira yako imekufa.

Kila mwenye akili, furaha yake ni kusikia corona imetokomezwa. Aliyefariki hana tofauti na mimi na wewe. Pengine hakuna alichotenda tofauti na tunavyotenda sisi. Huenda alikuwa mwema na mwerevu kuliko sisi.

Tuna nini sisi hata tufurahie kifo cha mmojawetu huku sisi wenyewe hatujui kama tutavuka katikati ya janga hili la kutisha la corona na mengine mengi yatuzungukayo?

Tushirikiane na Ulimwengu nzima kupambana na corona na majanga mengine. Ni juhudi za pamoja ndizo zinazoifanya Dunia kuwa ya matumaini. Ni nani angeweza kuishi bila ya:
Chanjo ya ndui
Tiba ya kipindupindu
Tiba ya malaria
Tiba na chanjo ya kifua kikuu
Chanjo ya surua
Madawa ya magonjwa ya moyo, kisukari
Tiba za typhoid, amoebic dysentery,
Tiba za magonjwa ya zinaa
Na mengine mengi

Ni ushirikiano wa Dunia nzima ndio uliosaidia kupatikana kwa tiba hizimaana hizi dawa zote hazikugunduliwa na nchi moja au mtu mmoja. Hapo ndipo tunapooneshwa maana ya neno lile - viungo Ni vingi lakini mwili Ni mmoja. TUNAISHI KWA KUTEGEMEANA. Tumshukuru Mungu kwa ugawaji wa karama kwaajili ya ukamilifu wetu.
 
Kwa afrika miaka 71 ni mingi sana iko kwenye range ya vitabu vya dini kabisa
...kwa hiyo vitabu vya dini vimetuandikia waafrika kwamba tutakufa mapema (70 yrs max)? Hao waliofika 80+ wako kinyume na dini?
 
... kwa hiyo vitabu vya dini vimetuandikia waafrika kwamba tutakufa mapema (70 yrs max)? Hao waliofika 80+ wako kinyume na dini?
Hata hao wa 80 ni wastani lakini kuna watu wanakufa chini ya hapo na hata hapa kwetu kuna watu kibao tu wana zaidi ya hiyo miaka
 
... tatizo tumezoea vifo vya mapema hadi tunaona kawaida. Life expectancy (2018) za wengine hizo hapo Mkuu; tunastahili kuishi sio kufa - Sweden - 82.56; Norway - 82.76; Finland - 81.73; Denmark - 80.95; Japan - 84.21; UK - 81.26; US - 78.54; France - 82.72.
Kwani alikuwa anaishi Japan au Sweden!?
Weka na life expectancy ya Bongo ndio tujue kaondoka mapema au vipi
 
Pole nyingi kwa familia yake kwa kumpoteza Baba.
Hakika mchango wake kwa taifa letu utakumbukwa daima.
Apumzike kwa amani.
 
Sasa huoni kuwa ni vibaya karne hii kuishi bila kujua chanzo cha kifo...?
Huoni kuwa taarifa za kisayansi zikitoka juu ya chanzo halisi cha kifo jamii inaweza kuwa salama zaidi!!
Ujinga wa kuficha maradhi utatumaliza...
Ugonjwa wa mtu ni siri ya mgonjwa je wewe uko tayari kujitangaza una ukimwi
 
Daah Majabali yanazidi kudondoka aisee[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24] Wazee kama hawa ndo wanaumia sababu ya Upuuzi wa mjuaji mmoja.. Sayansi haidanganyi yanii ni muda sasa wa Viongozi kubadilika yani lasivyo wazee wetu wataisha. Thamani na muda unaotumika kutengeneza Proffesa mmoja ni kubwa sana alafu leo kitoto wanakufa kama kuku.
Mkuu mlikuwa mnataka tamko haya kalitoa jana kanisani je Corona imepungua baada ya kutoa tamko ha ha ha ha ha hata huko ulaya wameamua kuipotezea corona maisha yanaendelea we endelea kusuburi matamko leo nimetoka airport wazungu kibao wameshuka kuja kula bata na barakoa zao so maisha lazima yaendelee mkuu
 
Apumzike kwa amani; alifanya mema wakati wake.

Ila sasa vifo vyote vwa watu maarufu visiwe kete za kisiasa kutumia korona. Watu wengi kwenye madaraka hutokea kuwa overweight na huweza wana matatizo mengine ya kiafya yanayoweza kuathiri uhai wao.
Weka evedence ya overweight
 
Kuna Mtumishi Mmoja hapo Wiki mbili zilizopita tu aliwahi Kuniambia kuwa Floors zao Mbili hapo zimehemewa Wagonjwa wa 'Bupiji Msivae Barakoa' na baada ya Taarifa hii sasa nimemuamini 100%.
 
Back
Top Bottom