Gazeti la The Economist: Rais Magufuli na CCM kuendelea kushika madaraka baada ya Uchaguzi Mkuu

Hawa jamaa wanafurahisha sana!

Hili ni tatizo la kukabidhi akili zao kwa mtu ambaye kiuhalisia hawamjui lakini kikubwa zaidi anazichezea akili zao kama atakavyo!

Ikiwa CCM ya 2015 ilikuwa imedhoofika kiasi cha wwnanchama wao kushindwa kuvaa sare mitaani kwa kuogopa kuzomewa, chini ya Magu CCM inabebwa na ukatili, ubabe, vitisho, mauaji, watu kupotea, kulazimisha matokeo kwenye chaguzi, kukandamiza upinzani, kuminya uhuru wa kupeana habari, na utawala usiofuta sheria za nchi kwa lengo la kutekeleza kwa nguvu ilani ya CCM ili kuja kuonyesha baadae kwamba walijaribu.

Hebu ajitokeze mtu aiondelee CCM hivyo vitu vyote vinavyoibeba halafu weka uwanja sawa wa ushindani uone kama kutabaki CCM mahali..

CCM ni dhaifu na imekataliwa na Watanzania toka zamani sana. Ipo madarakani kwa sababu ya hila, na kubebwa na mfumo mzima wa dola.

Hata CCM wenyewe wanalijua hili mioyoni mwao ndio maana ukigusia kurekebisha baadhi ya sheria ili ushindani uwe wa haki, wako tayari tuanze vita kuliko kugusa kisingi inayowabakisha madarakani.

Every Tanzanian knows this FACT. And the whole world know this dirty secret.
 
Post# 16 mtu kasema CCM itayawala milele. Itakuwa hivyo tu kama hapakuwa na siku ilipoanza kama vile MUNGU asiye na mwanzo wala mwisho.

Usahihi ni kusema upo uwezekano mkubwa CCM kutawala muda mrefu. Siyo milele.



Sent using Jamii Forums mobile app
 

Kama ishu ya lowasa katika uchaguzi mkuu hujui basi ww ni mgeni wa siasa au ni kijana mdogo ambae unaleta ubishi usio na msingi
 
Yes, lakini si kwasababu CCM Ni nzuri wala so kwasababu imefana vizuri wenye maendelei ya inchi kwahiyo inapendwa. Lahasha, hii ni kwasababu Ni ukweli kuwa serikali hii ya CCM inafana kila jitihada ya kuua upinzani kwa kutumia nguvu ya Dola, kuwanyima uhuru wa kisiasa na kuhakikisha vyombo vyote vya maamuzi Ni CCM. Hutegemei upinzani ushinde uchanguzi wakati tume ya uchanguzi Ni CCM. The economist wanachosema ndiyo hicho, kwamba kwa Hali ya udictator wa CCM na serikali yake hakuna namna upinzani utashinda madaraka. Huu Ni ukweli.

Nje ya hapo, kuwe na tume ya wananchi, siyo ya CCM, kuwe na uhuru wa kufanya siasa, mtashangaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Kusema kweli hatukuhitaji utafiti wa The Economist kujua hili kuwa kwa jinsi mambo yalivyo ccm itashinda 2020! Kwanza kuna uwezekano mkubwa uchaguzi usifanyike kabisa kama ilivyotokea kwa serikali za mitaa. Na hata ukifanyika hautakuwa tofauti ni zile chaguzi ndogo za kuanzia 2017 au kama ule wa Zanzibar 2015. Tangu umalizike uchaguzi mkuu tumeshuhudia kwa macho yetu nguvu kubwa, uhuni na ujambazi ukitumika kubadilisha ramani ya kisiasa iliyochorwa na uchaguzi huo. Kwenye jimbo moja la jirani nililofuatia kwa karibu, matokeo yalionyesha idadi ya wapiga kura kwenye uchaguzi mdogo ilikuwa kubwa kuliko ile ya uchaguzi mkuu 2015! Haya yanatokea wakati siku ya uchaguzi vyombo vya habari vilionyesha vituo vikiwa havina wapiga kura! Muda mfupi baada ya uchaguzi huo nilihudhuria msiba kwenye jimbo hilo. Kwenye gari nilikuwa na wapiga kura kadhaa wa jimbo hilo. Walikuwa wanaongea wenyewe tu kuhusu uchaguzi. Kati ya wapiga kura 6 au 7 waliokuwepo kwenye gari ikabainika ni mmoja tu au wawili walipiga kura. Mtu mmoja ambaye hskuwepo siku ya uchaguzi akawauliza wenzake swali zuri: kama wote hapa mnasema hamkushiriki zile kura zilipigwa na nani? The Economist wanachosema ni kuwa, kwa mtaji huu na aina ya uongozi tulionao ccm lazima ishinde. Na kusema kweli sababu za ccm kushinda kwa namna yoyote sasa zimeongezeka sana: baadhi ya viongozi wanaamini hawatakuwa salama chini ya chama kingine. Wanayo hata hofu dhidi ya baadhi ya wana-ccm wenzao! Lakini kama huko ndani ya ccm bado kuna waumini wa falsafa ya Nyerere basi swali kubwa la kuwashughulisha ni je, baada ya nchi yetu kupitia mambo magumu na ya kufedhehesha kwa taifa lililokuwa mfano wa kuigwa ccm bado inayo imani kikosi chake kilichoshika hatamu 2015? Nchi yetu iendelee kuwa chini ya KAKISTOCRACY kwa miaka mingine mitano? Tusubiri tuone.
 

Baada ya uchaguzi wa 2015 nchi hii haijaongozwa tena na ccm bali na "kitchen cabinet". Chama kimetumika tu kama hirizi ya kisiasa na kupiga muhuri mawazo binafsi ya baadhi ya watu.
 
Kusema kweli sababu za ccm kushinda kwa namna yoyote sasa zimeongezeka sana: baadhi ya viongozi wanaamini hawatakuwa salama chini ya chama kingine.
Naunga mkono hoja, kitu kama hiki niliwahi kukisema
P
 
Inabidi tu wakubaliane na sera za CCM kwa sababu CCM bado ipo sana!
 
Kuna vitu vya kawaida tu ukiviangalia unaona userious wa vyama ukoje...muundo wa vyama vya upinzani kiuongozi na kamati zake...juzi ccm wanaangalia muuelekeo wa siasa zao mpaka 2030 na ilani ya uchaguzi kuanza kuandaliwa...lakini wenzetu wako tuli...daftari ndio hilo sioni uhimizaji watu...ukweli mchungu ccm wanaweza kuwa na muda mrefu zaidi ya tunavyofikiri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata ningekuwa mimi, yaani nimchague mwenyewe Mwenyekiti wa Tume na Mkurugenzi wake afu eti waniambie sijashinda...weee labda wakatangazie matokeo hayo Pruto!!

Yaani kwa wale wenye akili nzito ni kwamba kama tunaendelea na Tume hii ya uchaguzi utake usitake CCM watashinda watakavyo.
 

..kwani Dr.Slaa baada ya kurudi CCM ameachana na madai yake kwamba alishinda uchaguzi wa 2010?
 
You sound like someone with placebo effect!
 
Unahitaji tu kuwa na akili ya kawaida kujua kuwa CCM haiwezi kutawala milele labda kama mwisho wa dunia unajulikana!
 
Tena nimewahi kusema mara nyingi sana humu jamvini kwamba HAKUNA MTU MNAFIKI KAMA ZITTO KABWE, NI OPPORTUNIST WA HALI YA JUU SANA ! Wamarekani na ujanja wao wasipo kua makini atawapiga hela ndefu japokua wanaweza mtemesha vile vile.
 
Hakuna mwaka utakuwa na wananchi wachache watakaopiga kura kama uchaguzi wa mwaka huu,raia walio wengi hawaoni umuhimu wa zoezi la kupiga kura (kwa mtazamo wangu)

Kwa habari ya majiji na miji kuwa chini ya CCM au UPINZANI haina maana yoyote,kwani kwa kiasi kikubwa watu wanatafuta nafasi kwa malengo yao BINAFSI...

KABLA ya 2015,miaka zaidi ya 50 majiji na miji karibu yote Tanzania ilikuwa ikongozwa na CCM,hata hiyo 2015 Ni fraction ndogo sana ya halmashauri zilizokuwa chini ya UPINZANI,Kama sikosei ni Arusha,DSM, Iringa,Moshi,Mbeya jiji (sijui kama kuna nyingine)

Halmashauri zingine zooote hapa nchini zimeendelea kuwa chini ya CCM,kurudisha hayo majiji na miji inayoongozwa na UPINZANI sidhani kama utakuwa na "any positive expectations" kwetu walala hoi,utakuwa ni mwendelezo wa maisha yetu ya kawaida tu kama ilivyo sasa...

Ni hayo tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…