Gazeti la Uhuru lamalizika sokoni tangu saa 2 asubuhi, Wasomaji walisaka hata kwa dau kubwa

Huo mchongo umesukwa vizuri Sana ndani ya chama ,rais yupo bize na wapinzani kumbe wapinzani wake wapo ndani ya chama chake mwenyewe
Hakuna cha mchongo hapo, CCM tu wameamua kuchezesha watu ngoma zao!!

And trust me, katika hili CCM wapo vizuri sana, sema watu hawajawashtukia!!

Just imagine.... tozo za miamala! Tozo za miamala! Tozo za miamala! Tozo za miamala; mara from nowhere tunasikia Mbowe kafunguliwa mashitaka ya ugaidi; na hivi sasa hakuna tena anayejadili masuala ya tozo!!

Hatujakaa vizuri; mara Kikekee, mara Samia! Mara Kikeke, mara maswali kwa Samia! Hatujakaa vizuri, mara Uhuru wanashuka na habari za Samia kutogombea 2025, na ghafla gazeti lote "limenunuliwa" na kuadimika mtaani, na kifungo kwa Uhuru juu!!!

Simulizi za Samia na intavyuu zinaachwa, watu wanahamia kwenye Gazeti la Uhuru!!
 
Yaani watu wakimbilie kununua gazeti la Uhuru kisa limeandika Samia hatagombea 2025?!

Itakuwa ni CCM wenyewe ndio walinunua nakala zote hili zisisambae!!
Wamesema wanaweka kumbukumbu ili wamkumbushe 2025, Ila keshachomoa
 
Wamesema wanaweka kumbukumbu ili wamkumbushe 2025, Ila keshachomoa
Akina nani hao wanaoweka kumbukumbu ili wamkumbushe?! CCM Insiders, au?!

CCM Insiders hawawezi kufanya hivyo kwa sababu CCM watafanya upumbavu wao wote lakini wakirudi Chimwaga, lao moja!!

Na kama sio Insiders, watakumbushia wapi na kutakuwa na effect ipi?!
 
Kelele za miamala ya simu naamini bado hazijaisha, kila siku wengi bado wanalalamika, kama hii ni mbinu CCM wanayoitumia wamefeli, Samia alituahidi majibu ya ripoti ya tume aliyoiunda, bado yanasubiriwa.

Above all, kuna kesi mahakamani, hata kama mshtaki ameshaanza kuulizwa alizaliwa wapi, tunajua hiyo ni michezo tu ya CCM na idara zake kwenye kulindana, muhimu kesi itasikilizwa na kutolewa maamuzi.

Kuhusu Mbowe, nako kuna kila aina ya ushahidi hiyo kesi ilitengenezwa ili kumfunga mdomo asiendelee na issue ya kudai Katiba Mpya.

Sasa inaonekana wazi kabisa, mbinu zote CCM wanazotumia ili kuwaondoa wengi kwenye reli zinaenda kushindwa.
 
Wa tz ndo tunapenda kutembea na stori 1 ila bado tozo haIkuwa na kipingamizi
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Man,

Unajisahaulisha tu au kujipa matumaini...

Kwanza Watanzania ni watu wa matukio; na ndo hapo hapo wanapotukamatia CCM! Kubali, kataa, la miamala ndo limeshaisha hilo! Kilichobaki hivi sasa ni kelele za kila mtu na lwake... kwamba, ukitaka kutuma pesa, na kuangalia tozo unayotunguliwa; hapo ndo unaanza kulia lia peke yako!!! Ndo kilichobaki hicho!!

Hilo la kesi mahakamani, nalo wala lisikusumbue!! Hivi ni mara ngapi umesikia simulizi za watu kufungulia mashitaka kampuni za simu?! Ni mara yako ya kwanza hii?!

Ushindi wa Mbowe hauna shaka, na ndo maana nikasema, "wakaibuka from nowhere na kumfungulia Mbowe kesi ya ugaidi"! Hawa mafedhuli huwa yanatengeneza matukio makusudi ku-divert attention za watu, na hawajali hata kama matukio yenyewe kuna wengine yanawaathiri!!

Chifu, ukweli mchungu ni mkwamba, CCM knows how to play politics! Mara kadhaa hapa nimepata kusema kuwa, brilliance waliyonayo CCM kwenye siasa ingekuwa ndo kwenye uchumi, Tanzania ingekuwa Uchumi wa Juu hivi sasa!!

Haya mambo ya kusema "wamefeli" tunayaongea sana labda kujipa matumaini lakini hayajafeli, na hatujui tu, yanatuathiri sana! CCM wameshajua udhaifu wa Watanzania... ni watu wa kuchezeshwa ngoma sana!! Mbaya zaidi, hata viongozi wa upinzani na wenyewe huwa wanacheza sana ngoma za CCM; kwa sababu "Watanzania ni watu wa matukio", na hatutaki kujifunza na kuishia kujipa matumaini "wameshajiua wenyewe hao"!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…