Geita: Mwalimu atuhumiwa kumuua mkewe

Geita: Mwalimu atuhumiwa kumuua mkewe

Mohammed wa 5

JF-Expert Member
Joined
Jun 20, 2022
Posts
1,215
Reaction score
3,035
HABARI Polisi mkoani Geita wamelazimika kufukua ndani ya nyumba ya mwalimu Francis Elizeus wa shule ya msingi Lubanga baada ya ndugu wa mke wake kumtuhumu kuwa amemuua mke wake Jenifer Mashimo na kumfukia ndani hali iliyopelekea ndugu hao kumtishia maisha mwalimu huyo. Mke wa Mwalimu huyo inadaiwa alitoweka tangu Machi 2020

Kamanda wa Jeshi la polisi mkoa wa Geita Safia Jongo anasema walipata taarifa ya tukio hilo wakafuatilia kibali cha mahakama ili waweze kujiridhishaa juu ya uwepo wa mwili ndani ya nyumba ya wanandoa hao ambapo hata hivyo hawajaupata

“Tarehe 3, Kibali kilipatikana na zoezi la ufukuaji ulianza kwahiyo siku ya tarehe 3, tulifukua mashimo manne ndani ya nyumba ambapo wale ndugu walikuwa wanahisi hayo maeneo kwamba ndugu yao amefukiwa lakini mpaka ikafika usiku hatukuweza kufanikiwa"

Tarehe 5 zoezi lile pia likaendelea ambapo tulifukua kila eneo ambalo tulitilia mashaka kwamba linaweza likafukiwa mwili lakini hatima yake tulikiridhisha kabisa kila eneo ambalo linastahili kufukuliwa ndani ya ile nyumba na lile eneo ndani ya ule mji tulilifukua na hakuna mwili uliopatikana kwahiyo familia na wenyewe wamethibitisha kwamba hakuna mwili uliofukiwa” alisema Jongo.

Kamanda Jongo anasema kwa sababu za kiuchunguzi na usalama imewalazimu kumshikilia mwalimu huyo ili waweze kumuepusha na watu wanaomtishia Maisha.
 
Ualimu wake unahusikaje kwa kupotea kwa huyo mke?!
Tuheshimu taaluma ya ualimu.

Tunataja taaluma endapo inahusika kwenye tukio...mf. taaluma ya udereva kwenye ajali ya gari.
Hebu tuwaacheni waalimu wapumue kidogo.
 
Ualimu wake unahusikaje kwa kupotea kwa huyo mke?!
Tuheshimu taaluma ya ualimu.

Tunataja taaluma endapo inahusika kwenye tukio...mf. taaluma ya udereva kwenye ajali ya gari.
Hebu tuwaacheni waalimu wapumue kidogo.
Mwalimu tatizo Nini kuitaja ualimu
 
HABARI Polisi mkoani Geita wamelazimika kufukua ndani ya nyumba ya mwalimu Francis Elizeus wa shule ya msingi Lubanga baada ya ndugu wa mke wake kumtuhumu kuwa amemuua mke wake Jenifer Mashimo na kumfukia ndani hali iliyopelekea ndugu hao kumtishia maisha mwalimu huyo. Mke wa Mwalimu huyo inadaiwa alitoweka tangu Machi 2020

Kamanda wa Jeshi la polisi mkoa wa Geita Safia Jongo anasema walipata taarifa ya tukio hilo wakafuatilia kibali cha mahakama ili waweze kujiridhishaa juu ya uwepo wa mwili ndani ya nyumba ya wanandoa hao ambapo hata hivyo hawajaupata

“Tarehe 3, Kibali kilipatikana na zoezi la ufukuaji ulianza kwahiyo siku ya tarehe 3, tulifukua mashimo manne ndani ya nyumba ambapo wale ndugu walikuwa wanahisi hayo maeneo kwamba ndugu yao amefukiwa lakini mpaka ikafika usiku hatukuweza kufanikiwa"

Tarehe 5 zoezi lile pia likaendelea ambapo tulifukua kila eneo ambalo tulitilia mashaka kwamba linaweza likafukiwa mwili lakini hatima yake tulikiridhisha kabisa kila eneo ambalo linastahili kufukuliwa ndani ya ile nyumba na lile eneo ndani ya ule mji tulilifukua na hakuna mwili uliopatikana kwahiyo familia na wenyewe wamethibitisha kwamba hakuna mwili uliofukiwa” alisema Jongo.

Kamanda Jongo anasema kwa sababu za kiuchunguzi na usalama imewalazimu kumshikilia mwalimu huyo ili waweze kumuepusha na watu wanaomtishia Maisha.
Mkuu Jana Si umetuaga humu unaondoka🤓

Nimeulizia tu Kwa nia nzurii....
 
Ualimu wake unahusikaje kwa kupotea kwa huyo mke?!
Tuheshimu taaluma ya ualimu.

Tunataja taaluma endapo inahusika kwenye tukio...mf. taaluma ya udereva kwenye ajali ya gari.
Hebu tuwaacheni waalimu wapumue kidogo.
Kwaio bwana platinum member ulitaka
Aseme bwana mmoja mzilankende amemuua mkewe..

Ukitajwa ualimu watu wanapanic....
 
Back
Top Bottom