Pre GE2025 Geita: Viongozi wa dini Chato wachangisha Tsh. Mil 1.4 kwaajili ya Rais Samia kuchukua fomu ya kugombe Urais

Pre GE2025 Geita: Viongozi wa dini Chato wachangisha Tsh. Mil 1.4 kwaajili ya Rais Samia kuchukua fomu ya kugombe Urais

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hizi fomu zipo ngapi maana Kila siku nakutana na Uzi watu wamechanga


Afu ccm si walishapitisha wagombea? Au mimi Kuna kitu sielewi hapa
Toa 1800 upatiwe ng'ombe 2 na kilo 500 za mchele mjini shule
 
Wakuu,


Mchango huo umefanyika katika hafla maalum iliyoandaliwa na Kamati ya Amani ya Wilaya ya Chato inayoundwa na viongozi wa dini mbalimbali kwa ajili ya kuliombea taifa dhidi ya ugonjwa wa Marburg.

Soma: Pre GE2025 - Geita: Matukio yanayojiri kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Katika mchango hao ambao wananchi pia walishiriki umefanikisha kupatikana kiasi cha Tsh. milioni 1.4 kwa ajili ya Rais Samia kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu mwaka 2025.

Ikumbukwe kuwa hivi karibuni serikali ya Tanzania ilithibitisha kuwepo kwa ugonjwa wa Murburg wilayani Biharamulo mkoani Kagera ambapo ni jirani na Chato Na mgonjwa mmoja kuthibitika kufa.

Soma: Pre GE2025 - Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Wajinga na ujinga ndiyo mtaji wa tapeli. Unachanga pesa huku una maisha magumu. 1.4m kulipa jitu ambalo limekuibia kwa kufuru. Limepitishwa na wapuuzi wewe unakuja kulichangia tena. Mimi nikikutana na Hawa waliochanga nafyeka viboko wote na kuwatia ndani
 
Nyerere aliwahi kusema maadui wakubwa wa 3 wa taifa hili ni

1.Ujinga
2. Maradhi
3. Umaskini

Na bado mpaka Leo hii Hawa maadui wa 3 bado hatujaweza kuwatokomeza
Ht Trump alikuwa anachangiwa tena na watu wenye akili km Elon, wamarekani ni adui yupi anawaandama? We ndio jinga lisiloelimika
 
Back
Top Bottom