Gerald Hando hata Wewe?

Gerald Hando hata Wewe?

Kila Nikiwaza kuandika huu uzi nilikuwa najishauri sana, mwishowe nimeona tu bora niandike ili dukuduku langu liishe.

Hivi karibuni watangazaji wakituo cha Wasafi FM Gerald Handom Maulid Kitenge na Zembwela walienda mpaka ziliko ofisi za DP Word kwenda kufanya mahojiano na wafanyakazi mbalimbali wa kampuni hiyo juu ya utendaji wao katika masuala mbalimbali ya bandari.

Kwangu ziara hiyo haikua na maana sana sababu kinachopingwa na watanzania wengi sio utendaji wa hao jamaa, hakuna anaepinga kua jamaa wako vizuri. Ila kinachopingwa ni aina ya mkataba. Sasa katika watangazaji hawa ningeweza kuelewa kama Maulid Kitenge na Zembwela wakifanya ushabiki wa haya masuala sababu upeo wao wa kuchambua mambo kama haya sio mkubwa kama Gerald.

Maulid Kitenge hua anaropokaga tu anadhani akiongea kwa sauti na ushabiki mkubwa ndio watu wataelewa. Sio mjenga hoja kwenye issues nyeti za msingi. Zembwela anaweza kua anajua kujenga hoja lakin mara nyingi huonekana kwenye vipindi ambavyo sio serious sana hivyo uwezo wake unaweza ukawa unafichwa na hilo.

Lakin Gerald Hando wewe toka ukiwa Clouds FM msimamo wako ulikua ni wa kutetea wanyonge. Wewe ulikua hutetereki kuongea ukweli. Ulikua huogopi kabisa na kipindi hicho uko clouds ulikua hot kweli kaka. Kipindi chako cha Power Breakfast kilikua hot sana kwenye ile segment ambayo ulikua ukizungumzia mambo mbalimbali yanayoihusu jamii. Umejadili mengi sana na kwa weledi sana kwenye hicho kipindi cha PB. Nadhan hata leo hii kama bado ungekua pale ungepinga hili.

Hata ulipoingia EFM bado ulikua hujaacha kuongelea mambo mbalimbali yanayohusu jamii. Nakumbuka ulisimamishwa hata EFM sababu ulikua ukitetea juu ya nchi kukopa kulikopitiliza. EFM yatangaza kumchukulia hatua Hando, yadai maoni yake kuhusu Serikali kukopa si msimamo wa taasisi.

- Hando aungana na Ndugai kupinga Serikali inavyokopa kopa ovyo

Sasa Gerald Hando wa sasa umekuaje? NIni kimekubadilisha msimamo? Ni wewe kweli unaungana na Mtu roporopo kama Maulid Kitenge kutetea kitu ambacho unajua sio sahihi? Najua mtakua mmelipwa ili mtetee ulaji lakini roho yako kweli haikusuti kwa usaliti unaoufanya? Au kuna mahali umebanwa kifedha ukaona ufate msemo wa "mtumikie kafiri upate utajiri"??

Ukweli sijaamini na sintoamini kama kweli eti wewe Gerald Hando unaamini kua ule mkataba wa DP World na Serikali hauna dosari yoyote ile,
Watanzania walio wengi wako wapi?

Jisemee wewe, unapinga nini?

Huna haki ya kumsemea mwengine yeyote bila kumtaja na kumnukuu alichosema, wacha propaganda za kujaza watu ujinga.

Punguani wahed
 
Hii kitu uliyoandika hapa haina maana mbele ya pesa mkuu!! Wee muache tu Gerald ale maisha, hii nchi kwa mfumo uliopo ni vzr uitafune sana pindi ukipata gap!!!
Unamlaumu huyo Hando ila ukweli ni kuwa hata DILI la kutuletea mchungaji ama sheikh wetu mpya ni lazima lifanywe na "mshenga"....

Yaani huyo mshenga asipewe nauli ya pesa kwenda kutuletea tutakacho ?!!!

Yaani huyo mshenga asipewe "kamshiko" ka maji na "soda" akiwa njiani kumfuata tunayemtaka?!!!

Akili hizo za baadhi ya ndugu zetu watanzania sizitaki ziwafikie vitoto vyangu vyenye miaka 6 na miaka 2.....sitaki virithi akili mfu katika du ia hii ya leo [emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Karibu Al Kasus hapa kijiwe cha kahawa karibu na chooni stendi ya mabasi makumbusho[emoji120]
 
Nchi hii kuliko kupambana na serikali kuwatetea wanyonge wasio jitambua bora uungane na serikali kujitumbulia maminofu tu.
 
Watanzania walio wengi wako wapi?

Jisemee wewe, unapinga nini?

Huna haki ya kumsemea mwengine yeyote bila kumtaja na kumnukuu alichosema, wacha propaganda za kujaza watu ujinga.

Punguani wahed
[emoji1787][emoji7][emoji7]
 
Nchi hii kuliko kupambana na serikali kuwatetea wanyonge wasio jitambua bora uungane na serikali kujitumbulia maminofu tu.
"Generalization" hiyo....[emoji1787][emoji1787]

Nchi inajengwa na kila mmoja....

Hivi unataka "mchanga" wa ardhi ya Tanzania ukulaani kwa kutouthamini ilihali uko juu yake kila uchao ?!!!

Tatizo hata imani za DINI hatuzielewi vyema pasi na ukariri utupelekao msambweni...nisikilize....liangalie taifa lako...thamani yake ni kubwa mno zaidi ya "neema" za wachache uwaonao.....

Tunaambiwa usipende kumuangalia sana "aliyeneemeshwa" ila muangalie yule wa chini yako......

Unawahusudu wanywao CIROC kisa tu wewe unaishia ubandani na kachupa kako ka "shengena" ?!!![emoji1787][emoji1787]

Karibu Al Kasus [emoji120]
 
Unamlaumu huyo Hando ila ukweli ni kuwa hata DILI la kutuletea mchungaji ama sheikh wetu mpya ni lazima lifanywe na "mshenga"....

Yaani huyo mshenga asipewe nauli ya pesa kwenda kutuletea tutakacho ?!!!

Yaani huyo mshenga asipewe "kamshiko" ka maji na "soda" akiwa njiani kumfuata tunayemtaka?!!!

Akili hizo za baadhi ya ndugu zetu watanzania sizitaki ziwafikie vitoto vyangu vyenye miaka 6 na miaka 2.....sitaki virithi akili mfu katika du ia hii ya leo [emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Karibu Al Kasus hapa kijiwe cha kahawa karibu na chooni stendi ya mabasi makumbusho[emoji120]
Tatizo ni mfumo!! Hata watoto wetu ikiwa mfumo ni huu huu watapiga madili tu!! Mfumo ubadilike hata raia watakua wazalendo.
 
Ukweli sijaamini na sintoamini kama kweli eti wewe Gerald Hando unaamini kua ule mkataba wa DP World na Serikali hauna dosari yoyote ile,
Kama ni kweli unamwamini Gerald Hando kiasi hicho nawe ni tatizo,
Journalist wengi Bongo ni wachumia tumbo, usiamini kila wanachokisema, huwa hawamaanishi!!
 
Tatizo ni mfumo!! Hata watoto wetu ikiwa mfumo ni huu huu watapiga madili tu!! Mfumo ubadilike hata raia watakua wazalendo.
Mh.Rais Chifu Hangaya amekuja na suluhisho adhimu.....

Karibuni mitaala ya "KUKURU" itai gizwa mashuleni.....

TAKUKURU wameagizwa wakae chini na WIZARA YA ELIMU....

Mh.Rais SSH ana maono makali zaidi ya anavyodogoshwa [emoji120]

#SiempreJMT[emoji120]
 
Mh.Rais Chifu Hangaya amekuja na suluhisho adhimu.....

Karibuni mitaala ya "KUKURU" itai gizwa mashuleni.....

TAKUKURU wameagizwa wakae chini na WIZARA YA ELIMU....

Mh.Rais SSH ana maono makali zaidi ya anavyodogoshwa [emoji120]

#SiempreJMT[emoji120]
Hii ngonjera uliyoandika haisaidii!! Imagine mtoto mdogo mpaka anakua anasikia tu viongoz watu kweny utawala wamepiga B kadhaa mara ufisadi B kadhaa!! Kibaya zaid mtoto mpaka anakua mtu mzm hajawah sikia au kuona wabadhirifu na mafisad wamerudisha pesa zote na kula kifungo. Hapo mtoto anajifunza nn?? Tusijifanganye uzalendo uanzie kwa viongoz kwanza watuonyeshe mfano!! Over
 
Ni neema tupu....

Mkataba wetu na DPW unakwenda kuuondoa urasimu na "status quo" iliyoko bandarini.... haiwezekani bandari za nchi jirani ,Lamu na Mombasa ziwe na ubora wa kupakia na kupakua mizigo ndani ya siku 3 ,zetu ziwachukulie wafanyabiashara siku 7 ,siku 14 hadi mwezi na nusu....AIBU HII ...

Tunapoteza mapato kiasi gani.

Tunawaumiza wafanyabiashara kiasi gani.

Turidhie kukimbiwa na wafanyabiashara wa hizi nchi 8 zinazotuzunguka?!!!

Serikali ya awamu ya 6 inakwenda kuukata huo mzizi wa fitina[emoji120]

Kongole kwake mh.Rais SSH[emoji120]

#SiempreJMT[emoji120]
Vip na jeshi la police nalo mtaliuza kwasababu ya urasimu au
 
Usimlaumu gerald ujue ana ndoa na watoto wanahitaji kwenda chooni, ana suzuki lile linakunywa mafuta kama jini, wenzie akina G habash wanasukuma vw convertible , kipanya ana range rover autobiography kama ya marehemu jasusi mbobezi membe yeye pia anatamani account itune. Kitenge pale DTB ana account inagonga milioni 300. Hando lazima uzalendo umshinde
 
Kama ni kweli unamwamini Gerald Hando kiasi hicho nawe ni tatizo,
Journalist wengi Bongo ni wachumia tumbo, usiamini kila wanachokisema, huwa hawamaanishi!!
Uchumia tumbo usemao ni kama "generalization" hivi....

Duniani kote waandishi wa habari wana "sponsors".....[emoji1787][emoji1787]
 
Ni neema tupu....

Mkataba wetu na DPW unakwenda kuuondoa urasimu na "status quo" iliyoko bandarini.... haiwezekani bandari za nchi jirani ,Lamu na Mombasa ziwe na ubora wa kupakia na kupakua mizigo ndani ya siku 3 ,zetu ziwachukulie wafanyabiashara siku 7 ,siku 14 hadi mwezi na nusu....AIBU HII ...

Tunapoteza mapato kiasi gani.

Tunawaumiza wafanyabiashara kiasi gani.

Turidhie kukimbiwa na wafanyabiashara wa hizi nchi 8 zinazotuzunguka?!!!

Serikali ya awamu ya 6 inakwenda kuukata huo mzizi wa fitina[emoji120]

Kongole kwake mh.Rais SSH[emoji120]

#SiempreJMT[emoji120]
Kwani lamu na Mombasa Kuna muwekezaji?

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
 
Duuuh bas tumuache jamaa, atetee uhai wake.
Hili ndilo wengi hapa mnaomlaumu mlikuwa mmelisahau. Na kuna Mmoja hapo anadhani ni Mtangazaji Mwenzake kumbe yuko Kazini na anamchora tu ili akosee kisha akamripoti na Washughulike nae mazima kama akina Gwanda na Yule wa Chatu Kigamboni.

Naomba niishie hapa tafadhali Mkuu.
 
Watanzania walio wengi wako wapi?

Jisemee wewe, unapinga nini?

Huna haki ya kumsemea mwengine yeyote bila kumtaja na kumnukuu alichosema, wacha propaganda za kujaza watu ujinga.

Punguani wahed
Punguani Mwenyewe,
Vavavayo
 
Haya jibu maswali niliyokuuliza sasa, au ni ufataani tu?
Sawa,
Napinga kua na mkataba usio na ukomo wa muda,
Napinga kua na mkataba usioonyesha mgawanyo wa mapato,
Napinga kua na mkataba ambao ukiingia hutoki,
Napinga Kina Gerald kwenda kuhoji wa DPW wakati kinacholalamikiwa sio utendaji bali mkataba ulivyo,
 
Kila Nikiwaza kuandika huu uzi nilikuwa najishauri sana, mwishowe nimeona tu bora niandike ili dukuduku langu liishe.

Hivi karibuni watangazaji wakituo cha Wasafi FM Gerald Handom Maulid Kitenge na Zembwela walienda mpaka ziliko ofisi za DP Word kwenda kufanya mahojiano na wafanyakazi mbalimbali wa kampuni hiyo juu ya utendaji wao katika masuala mbalimbali ya bandari.

Kwangu ziara hiyo haikua na maana sana sababu kinachopingwa na watanzania wengi sio utendaji wa hao jamaa, hakuna anaepinga kua jamaa wako vizuri. Ila kinachopingwa ni aina ya mkataba. Sasa katika watangazaji hawa ningeweza kuelewa kama Maulid Kitenge na Zembwela wakifanya ushabiki wa haya masuala sababu upeo wao wa kuchambua mambo kama haya sio mkubwa kama Gerald.

Maulid Kitenge hua anaropokaga tu anadhani akiongea kwa sauti na ushabiki mkubwa ndio watu wataelewa. Sio mjenga hoja kwenye issues nyeti za msingi. Zembwela anaweza kua anajua kujenga hoja lakin mara nyingi huonekana kwenye vipindi ambavyo sio serious sana hivyo uwezo wake unaweza ukawa unafichwa na hilo.

Lakin Gerald Hando wewe toka ukiwa Clouds FM msimamo wako ulikua ni wa kutetea wanyonge. Wewe ulikua hutetereki kuongea ukweli. Ulikua huogopi kabisa na kipindi hicho uko clouds ulikua hot kweli kaka. Kipindi chako cha Power Breakfast kilikua hot sana kwenye ile segment ambayo ulikua ukizungumzia mambo mbalimbali yanayoihusu jamii. Umejadili mengi sana na kwa weledi sana kwenye hicho kipindi cha PB. Nadhan hata leo hii kama bado ungekua pale ungepinga hili.

Hata ulipoingia EFM bado ulikua hujaacha kuongelea mambo mbalimbali yanayohusu jamii. Nakumbuka ulisimamishwa hata EFM sababu ulikua ukitetea juu ya nchi kukopa kulikopitiliza. EFM yatangaza kumchukulia hatua Hando, yadai maoni yake kuhusu Serikali kukopa si msimamo wa taasisi.

- Hando aungana na Ndugai kupinga Serikali inavyokopa kopa ovyo

Sasa Gerald Hando wa sasa umekuaje? NIni kimekubadilisha msimamo? Ni wewe kweli unaungana na Mtu roporopo kama Maulid Kitenge kutetea kitu ambacho unajua sio sahihi? Najua mtakua mmelipwa ili mtetee ulaji lakini roho yako kweli haikusuti kwa usaliti unaoufanya? Au kuna mahali umebanwa kifedha ukaona ufate msemo wa "mtumikie kafiri upate utajiri"??

Ukweli sijaamini na sintoamini kama kweli eti wewe Gerald Hando unaamini kua ule mkataba wa DP World na Serikali hauna dosari yoyote ile,
Kitenge na Zembwela hawana elimu yoyote wao wanaishi kwa nguvu za giza, Hando kwa kweli hata mimi nimeshangaa sn
 
TUMBO Baba
TUMBO Baba
TUMBO Baba
TUMBO Baba
TUMBO Baba
TUMBO Baba
 
Back
Top Bottom