Gerson Msigwa: Huwezi kukurupuka kumfukuza mtu, pengine hata wakaguzi wa CAG nao ukaguzi wao una dosari

Kwa maelezo yako ni kwamba Hakuna haja ya kuwa na CAG. Mbona tutaibiwa mpaka tukome.
Hapana sijasema hivyo, ofisi ya CAG ni muhimu mno, yeye ndio jicho la bunge. Ninachokisema ni watu waelewe kazi ya CAG, ni jicho la bunge na sio kwamba yeye ndio Bunge.

Huwezi kutumia ripoti ya CAG kuhukumu watu hapohapo, watu hawatatotendewa haki. Na uzoefu wa miaka ya nyuma unaonesha kuna baadhi ya hoja huwa zinakuwa hazina uzito wa kuitwa 'upigaji', zinafutwa na CAG anaridhia zifutwe kule bungeni.

Pia kuna hoja ambazo zinaibua wizi wa kweli, na huwa zinafuatiliwa vuzuri sana, tena mwaka unaofuata CAG huwa anaanza na hizo kuhakikisha kuwa tatizo halijajirudia.

Kinachotakiwa ni utaratibu kamili ufuatwe, Spika alijaribu kueleza hilo lakini watu wakawa moto kwelikweli, akatumia busara kukaa kimya, japo alikuwa sahihi.

Imagine kama ungekuwa ukikamatwa na polisi unaambiwa toa maelezo, maelezo yako yasipo waridhisha basi unahukimiwa hapohapo na polisi haohao! Unadhani haki inatendeka kwa utaratibu huo?

Likewise CAG anaona mapungufu, anaomba ufafanuzi kutoka kwa wahusika, asiporidhishwa na ufafanuzi anaandika kuwa ameona kasoro moja mbili tatu. Sasa kitendo cha CAG kuandika sio hukumu, ni tuhuma.
 
- hebu tutajie ni Ripoti ya Mwaka gani ilikosewa?
 
- Kama sio hukumu ni tuhuma, DPP na TAKUKURU walitakiwa wakafungue Kesi mahakamani, na mahakama ndio itatoa hukumu.
-Au Polisi wafanye Uchunguzi wao nao, halafu wapeleke Police file Kwa DPP halafu DPP atatoa opinion yake kama Kuna haja ya kwenda mahakamani au hakuna haja.
- Ni kweli, CAG hawezi kuhukumu Kwa sababu yeye sio Mamlaka ya utoaji haki, Bali ni mahakama tu ndio yenye kutoa hukumu.
 
Halafu utasikia kesi imeahirishwa upepelezi bado unaeendelea.
Ndo hapo nashangaa na mie, huyu Msigwa aeleze vizuri umma uelewee., hao waliotajwa wapelekwe mahakamani km ni uongo au ukweli utajulikana huko huko.

Hatutaki kuona double standard, tumechokaaa.
 
Ndo hapo nashangaa na mie, huyu Msigwa aeleze vizuri umma uelewee., hao waliotajwa wapelekwe mahakamani km ni uongo au ukweli utajulikana huko huko.

Hatutaki kuona double standard, tumechokaaa.
Sawasawa mjukuu wa Mshana Jr.
 
Wewe unaetukana watu ndiye hujielewi. Yani hadi kufikia CAG kuweka public document km hiyo kwamba hakujiridhisha!!! Unadhani hiyo report ni sawa na makaratasi ya kufungia maandazi.

Km katiba au sheria za nchi zina kipengele Cha kujiridhisha kwa nini serikali isingemzuia kuitoa public kwanza ili ajiridhishe. Sasa wewe mwenye akili nyingi unadhani hadi CAG anaitoa hadharani hakuwasiliana na mamlaka ya serikali.

Watu km nyie ndiyo hamkustahili kuliona jua maana ni hasara kwa taifa. Unajitia ujuaji na kuunga mkono utumbo uliosemwa na mwenzio kwa sababu za mahaba niue. Unaweza kujiona wewe ndiyo fundi kujua kumbe fundi kujiharibia.

Nimemaliza....
 
Maneno ya kifedhuli kabisa!
 
Kuna watu wanakingiwa kifua kijanja.

Tuna safari ndefu sana
 
Kwa namna hii, Tanzania hata haihitaji kuwa na CAG, ni kupoteza pesa tu kuwalipa watu ambao kazi wanayoifanya inatupwa kwenye dustbin. Ngoja tusubiri iundwe tume ya kuchunguza ripoti.
 
Mh Jakaya Kikwete wakati huo akiwa foreign minister aliwahi kuwaeleza BBC kuhusu ufisadi ulioibuliwa na CAG ktk ubalozi wa Italy kuwa "kazi ya auditor ni kuibua hoja na kazi ya serikali ni kuzijibu". Sasa kusema wanaotajwa na ripoti ya CAG tayari wanastahili adhabu ni ku-miss the point. Ndio maana kuna kamati za mahesabu za bunge. Na kama tayari kama waliotajwa tayari ni wahalifu kusingekuwa na haja ya kujadili ripoti hiyo bungeni. Umewahi kusikia bunge likijadili hukumu iliyotolewa na mahakams?
 
ripoti za CAG wanayajua hayo, huwa zina makosa mengi tu, na ndio naana baadhi ya hoja zake huwa zinafutwa na kufungwa kabisa.

Wakati ripoti za CAG zinatambulika kimataifa kwa ubora, ninyi mnagundua, ni jambo jema kufanya hivyo na msiishie kugundua hayo makosa, muonesheni kabisa ili ajirekebishe kutorudia makosa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…