Gerson Msigwa: Huwezi kukurupuka kumfukuza mtu, pengine hata wakaguzi wa CAG nao ukaguzi wao una dosari

Gerson Msigwa: Huwezi kukurupuka kumfukuza mtu, pengine hata wakaguzi wa CAG nao ukaguzi wao una dosari

Nilipokaa muda huu Niko na DED aliyetajwa na CAG kuwa ni mwizi ana warembo wanne wanakula bata haijawahi kutokea. Ikitoka 10,000 ya bia moja hataki chenchi. Ana wapambe kama wote japo yeye amelala tu kwenye kiti udenda unamtoka.
 
Wewe unaetukana watu ndiye hujielewi. Yani hadi kufikia CAG kuweka public document km hiyo kwamba hakujiridhisha!!! Unadhani hiyo report ni sawa na makaratasi ya kufungia maandazi.

Km katiba au sheria za nchi zina kipengele Cha kujiridhisha kwa nini serikali isingemzuia kuitoa public kwanza ili ajiridhishe. Sasa wewe mwenye akili nyingi unadhani hadi CAG anaitoa hadharani hakuwasiliana na mamlaka ya serikali.

Watu km nyie ndiyo hamkustahili kuliona jua maana ni hasara kwa taifa. Unajitia ujuaji na kuunga mkono utumbo uliosemwa na mwenzio kwa sababu za mahaba niue. Unaweza kujiona wewe ndiyo fundi kujua kumbe fundi kujiharibia.

Nimemaliza....
Acha chuki mkuu 🤣🤣🤣
 
- Kama sio hukumu ni tuhuma, DPP na TAKUKURU walitakiwa wakafungue Kesi mahakamani, na mahakama ndio itatoa hukumu.
-Au Polisi wafanye Uchunguzi wao nao, halafu wapeleke Police file Kwa DPP halafu DPP atatoa opinion yake kama Kuna haja ya kwenda mahakamani au hakuna haja.
- Ni kweli, CAG hawezi kuhukumu Kwa sababu yeye sio Mamlaka ya utoaji haki, Bali ni mahakama tu ndio yenye kutoa hukumu.
It was an analogy, nikilinganisha mfumo wa utoaji haki nchini na mfumo wa ukaguzi.

PCCB na polisi ni vyombo vya serikali, ripoti ya CAG sio kwa ajili yao ni kwa ajili ya kufanyiwa kazi na Bunge.

Serikali itapewa maazimio na Bunge wakishamaliza kuifanyia kazi ripoti, hatua zitachukuliwa.

Hakuna mtu anatetea ufisadi, ninachokisema ni utaratibu ufuatwe, ukiwa na tabia ya kupuuza sheria za nchi mwisho wake ndio yaleyale ya mtu katumbuliwa leo kesho anarudishwa baada ya kuonekana hana makosa.

Kuna watu wanaweza hata kupoteza maisha kwa presha za kutumbuliwa bila kuwa na makosa, unamkumbuka yule mkurugenzi wa jiji la Dar aliyetumbuliwa hadharani??
 
Msemaji wa Serikali ya Tanzania, Gerson Msigwa amesema kwamba ni vema Wadau wakavuta subira badala ya kutaka kila aliyetajwa kwenye ripoti ya CAG achukuliwe hatua, yapo maeneo ambayo ni lazima yapitiwe upya ili kujiridhisha na kila lililotajwa.

Amedai kwamba unaweza kumchukulia mtu hatua kumbe hana makosa na pengine ripoti ya CAG ndio iliyokosewa.

Toa Maoni yako.
Msigwa ana hara na kutapika
 
Msemaji wa serikali anapaswa kutoa matamko yenye kuzingatia utaalamu na weledi wa fani husika. Kwa kuwa anachokisema huakisi uelewa wa mambo mbalimbali wa watawala. Ni lazima ajitofautishe anapochangia jambo lolote lile akiwa kama mtu binafsi, na pale anapoiwakilisha serikali.
Msemaji wa Serikali ya Tanzania, Gerson Msigwa amesema kwamba ni vema Wadau wakavuta subira badala ya kutaka kila aliyetajwa kwenye ripoti ya CAG achukuliwe hatua, yapo maeneo ambayo ni lazima yapitiwe upya ili kujiridhisha na kila lililotajwa.

Amedai kwamba unaweza kumchukulia mtu hatua kumbe hana makosa na pengine ripoti ya CAG ndio iliyokosewa.

Toa Maoni yako.
Siyo sahihi kwake kusema kuwa ripoti ya ukaguzi wa mahesabu imekosewa, isipokuwa angetoa maelezo kuwa pengine kuna kasoro zilizoainishwa zilitokana na kukosekana kwa ushahidi wa kinyaraka kwa wakati. Wakaguzi hawakurupuki, wala zoezi la ukaguzi haliendeshwi kwa usiri kiasi kwamba wahusika waseme kuwa hawakuwa na taarifa kuhusu mapungufu yaliyotolewa katika ripoti.

Wahusika hushirikishwa katika kila hatua ya ukaguzi, na hutakiwa kuleta ushahidi wa kinyaraka katika maeneo yanayokaguliwa. Siyo kosa la mkaguzi endapo zitatokea "audit queries" ambazo hazitolewi maelezo ya kuridhisha kuendana na kanuni na miongozo iliyowekwa, ama kutokana na mapungufu ya ushahidi wa kinyaraka.

"Audit queries" zinapotolewa maelezo ya kutosha basi huondolewa, la sivyo hubakia na kuripotiwa kuwa ni makosa, na aina ya kosa huangaliwa kuendana na athari yake kama ni kubwa, ya kati, ama ndogo ili hatua stahiki za kiutawala na kisheria zichukuliwe dhidi ya muhusika.

Msemaji wa serikali anapaswa kutambua ripoti ya CAG inatoa "fair view" kuhusu matumizi ya fedha za umma kwa mwaka uliopita wa serikali. Ni lazima pia atachague maneno sahihi pale anapozungumzia masula ya kitaalamu na kiuweledi kutokana na hadhi ya fani husika.
 
It was an analogy, nikilinganisha mfumo wa utoaji haki nchini na mfumo wa ukaguzi.

PCCB na polisi ni vyombo vya serikali, ripoti ya CAG sio kwa ajili yao ni kwa ajili ya kufanyiwa kazi na Bunge.

Serikali itapewa maazimio na Bunge wakishamaliza kuifanyia kazi ripoti, hatua zitachukuliwa.

Hakuna mtu anatetea ufisadi, ninachokisema ni utaratibu ufuatwe, ukiwa na tabia ya kupuuza sheria za nchi mwisho wake ndio yaleyale ya mtu katumbuliwa leo kesho anarudishwa baada ya kuonekana hana makosa.

Kuna watu wanaweza hata kupoteza maisha kwa presha za kutumbuliwa bila kuwa na makosa, unamkumbuka yule mkurugenzi wa jiji la Dar aliyetumbuliwa hadharani??
  • ni lini serikali iliwapeleka mahakamani watuhumiwa wa ufisadi utokanao na Ripoti ya CAG?
  • Serikali imekuwa ikifanyia Kazi mapendekezo ya Bunge Kwa kiwango kidogo Sana,
  • sheria gani ya nchi imepuuzwa hebu tutajie tukaisome.
 
Msemaji wa Serikali ya Tanzania, Gerson Msigwa amesema kwamba ni vema Wadau wakavuta subira badala ya kutaka kila aliyetajwa kwenye ripoti ya CAG achukuliwe hatua, yapo maeneo ambayo ni lazima yapitiwe upya ili kujiridhisha na kila lililotajwa.

Amedai kwamba unaweza kumchukulia mtu hatua kumbe hana makosa na pengine ripoti ya CAG ndio iliyokosewa.

Toa Maoni yako.
Huyo pimbi naye mpuuzi tu
 
Msigwa Hana taaluma ya uhasibu. Ni vema akaongelea Mambo ya Yanga na Simba kupewa vitita vya milioni tano wakifuzu.
Nusu fainali imeongezeka, sasa kila goli mil 10
 
Hapana sijasema hivyo, ofisi ya CAG ni muhimu mno, yeye ndio jicho la bunge. Ninachokisema ni watu waelewe kazi ya CAG, ni jicho la bunge na sio kwamba yeye ndio Bunge.

a ufafanuzi kutoka kwa wahusika, asiporidhishwa na ufafanuzi anaandika kuwa ameona kasoro moja mbili tatu. Sasa kitendo cha CAG kuandika sio hukumu, ni tuhuma.

Kwa hapo nimekuelewa, ingawa position yangu ni kwamba, mtu anapotuhumiwa asimamishwe kazi kwa muda kupisha uchunguzi kuliko sasa unatuhumiwa halafu wewe ndio unaombwa utoe ufafanizi mbele ya kamati ya bunge.
 
Msemaji wa Serikali ya Tanzania, Gerson Msigwa amesema kwamba ni vema Wadau wakavuta subira badala ya kutaka kila aliyetajwa kwenye ripoti ya CAG achukuliwe hatua, yapo maeneo ambayo ni lazima yapitiwe upya ili kujiridhisha na kila lililotajwa.

Amedai kwamba unaweza kumchukulia mtu hatua kumbe hana makosa na pengine ripoti ya CAG ndio iliyokosewa.

Toa Maoni yako.
Uyu Mshamba atafutiwe kazi nyingine!
 
Msemaji wa Serikali ya Tanzania, Gerson Msigwa amesema kwamba ni vema Wadau wakavuta subira badala ya kutaka kila aliyetajwa kwenye ripoti ya CAG achukuliwe hatua, yapo maeneo ambayo ni lazima yapitiwe upya ili kujiridhisha na kila lililotajwa.

Amedai kwamba unaweza kumchukulia mtu hatua kumbe hana makosa na pengine ripoti ya CAG ndio iliyokosewa.

Toa Maoni yako.
Ni kutaka kutengeneza mianya ya kujisafisha...
Pia ni kutaka kumpa kagi mchuzi kidogo awatakatishe.
Aibu
 
  • ni lini serikali iliwapeleka mahakamani watuhumiwa wa ufisadi utokanao na Ripoti ya CAG?
  • Serikali imekuwa ikifanyia Kazi mapendekezo ya Bunge Kwa kiwango kidogo Sana,
  • sheria gani ya nchi imepuuzwa hebu tutajie tukaisome.
Some sheria ya ukaguzi wa umma kuanzia kifungu cha 37 mpaka 40, utaona kuwa ripoti hiyo ni kwa ajili ya Bunge kufanyia kazi, Bunge ndio linatoa mapendekezo serikalini ya hatua gani zichukuliwe.

Lakini pia, kama sehemu kuna wizi unaofanyika, haijalishi kama CAG amendika au la, vyombo husika kama PCCB wanapaswa kuchukua hatua. Kwani yote ambayo PCCB wanafanya CAG huwa anayaona?
 
Watanzania wengi wana mihemko na ni wajinga, ndio maana serikali huwa inapuuza na kungojea mijadala ife yenyewe, kubishana nao ni kupoteza muda.

Msigwa ameongea ukweli mtupu, wenye uzoefu na ripoti za CAG wanayajua hayo, huwa zina makosa mengi tu, na ndio maana baadhi ya hoja zake huwa zinafutwa na kufungwa kabisa.

Wanaofanya ukaguzi ni watumishi wa umma wa kawaida tu, tena wengine wameajiriwa juzi juzi hapa hata uzoefu hawana. Watu huwa wanadhani Kichere mwenyewe ndio anakwenda 'site'.

Hatusemi kuwa ripoti yote imejaa makosa, tunachosema ni kuwa watu wawe watulivu utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa sheria ufuatwe, wenye makosa watachukuliwa hatua na wale wasio na makosa hoja zao zitafutwa.

Kwa umbumbumbu wa watanzania ni bora Msigwa angekaa kimya, sometimes it doesn't matter if you are correct.
Kwani wewe ni lini uliona watumishi wenzako wamechukuliwa hatua kutokana na ripoti ya CAG!
Acha usanii,hiyo ofisi ya CAG si ndiyo huwa inapewa kazi mpaka na taasisi za kimataifa kufanya ukaguzi?sasa leo unatuambiaje kuwa ripoti imekosewa?mbona kimataifa ofisi ya CAG inasifiwa kwa kazi nzuri!
 
We ndiyo mjinga zaidi, watumishi wa CAG huanza ukaguzi baada ya mwaka wa fedha kufungwa June 30 na wao July wanaingia kazini, wanaanza kuomba viambatanisho vyote, ikifika October hutoa hoja zao na kuwapa muda management kuzijibu mpaka January, how huo muda hautoshi na wakati kuna kuwa na exit meeting?
Uyo Kilaza atakuwa na yeye katajwa ndiyo maana anatetea upuuzi.
 
Back
Top Bottom