Get Rich or Die Tryin: Niliyoyapitia katika ukuaji wangu

Get Rich or Die Tryin: Niliyoyapitia katika ukuaji wangu

Mangi shangali

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2023
Posts
533
Reaction score
820
Natumaini wote wazima humu,japo changamoto zipo ila tunatakiwa tukomaye nazo maana haina jinsi:

Hizo changamoto tumeumbiwa sisi binadamu,hata uende wapi zipo pale zinakusubiri.

Nimependezewa niwaletee niliyoyapitia katika ukuaji wangu mpaka nilipofikisha 20s,najua utajifunza moja au lingine.

Mangi shangali..
ARUSHA,TANZANIA.

YAFUATAYO YANAFURAHISHA..

UTANGULIZI:-
NIlizaliwa katika hospital ya mount meru iliyopo katika jiji la arusha.kipindi hicho baba alikuwa anafanya kazi katika benki ya nbc,mama alikuwa mfanya biashara soko kuu arusha kipindi hicho soko lilikuwa linaitwa soko la bondeni kitambo hicho..

Katika ukuaji wangu na story nilizopewa na wazazi wangu pamoja na ndugu zangu waliokuwa nami nilipokuwa mtoto.

Mama anasema nilikuwa mtundu sana tena ujeuri,nilipokuwa na miaka 4 nilikuwa najifungia kwenye friji,kwa watu wanajua yale mafriji ya zamani yalikuwa makubwa sana sasa nilikuwa naingia ndani,nakujifungia humo mama ananitafuta kumbe nipo ndani ilikuwa tafurani sana.

Mama anasema nilikuwa nashika kiwembe najikata mwenyewe mkononi na hata sitoi chozi,nilikuwa na matukio ya hatari kuna siku nilichomeka pasi mkutani nikipigwa na shoti nikazimia kwa masaa 6 watu walijua nimekufa.

Tulikuwa na mtindo wa kudandia gari kwa nyuma, lilechuma lakupanda lilikuwa limeoza kuwa kutu silikakatika bana niliburuzwa mpaka ngozi kwenye tumbo zikatoka.

Aisee ngoja nifupishe maana nilikuwa na matukio ya hatari sana ambayo kama sio kudra za mwenyenzi MUNGU nisingekuwa hai leo hii..

Nilipofikisha umri wa kwenda darasa la kwanza nilijiunga katika shule ya sanawary iliyepo arusha,nilisoma vinzuri mpaka kufika darasa la 4 ndio tatizo lilianza maana nilikuwa ujeuri shuleni na mkorofi,wanafunzi niliyesoma nao kipindi hicho walipata joto ya jiwe maana nilikuwa sionewi ovyo,nilikuwa napigana na walionizidi darasa tena la saba.

Shule tulikuwa na tabia ya kupigana
Tunaenda mtoni huko hakuna watu,natafutiwa mbabe wanaomuona ubabe wao natembeza kichapo heavy nikawa naogopeka shule nzima mpaka vijana wa darasa la Saba waliniwazia maana nishawatandika wababe wao .walimu walipata tabu nilipogoma kusoma hakuna mwalimu alithubutu kunichapa nilipochelewa namba na usafi sikupe ratiba yeyote ya usafi darasani.

Niliingia shule mda walimu wanaingia tena mikono mfukoni,nilikuwa mkorofi ila darasani sikuwahi kushuka chini ya mtu wa 5,matokeo ya mitihani nilifanya vyema.

Itaendeleea...
 
Inaendelea....
Kwetu sisi tupo watoto 8 mimi ni mtoto wa mwisho nina kaka zangu pia na dada zangu,kipindi kile nikiwa darasa la 5 kaka zangu walikuwa wanapolo namaanisha wachimba madini,kipindi kile wanapolo waliogopeka kwa ubabe wao na jeuri ya fedha.
Sasa kuna kipindi mgodi wa tafu goni ulitema na kaka ndo lilikuwa chimbo lao aisee walipiga pesa sana,waliporudi home walijenga nyumba za wapangaji na kununua majumba kwa watu,kwa mkazi wa arusha anaijua barabara ya ilboru wanapolo walikuwa wanaifunga kwa kuweka mTrey yabia tena wanaweka viti katikati ya barabara hakuna gari kupanda wala shuka kibabe na hakuna mtu wakuwagusa.
Walikuwa natabia ya kuosha pikipiki zao na gari kwa bia,kaka walipiga pesa ndefu sana kipindi hicho sema starehe nyingi
 
Yote niliyoyaandika zilikuwa utangulizi sasa story lenyewe niliyokusudia linaanza hivi:...

Sehemu ya kwanza:=...

Tamaa za fedha zilijaa akilini mwangu,kipindi hicho nilikuwa darasa la 7 ndo namaliza ila kiumbo mimi ni mrefu nilijiona nimekuwa tayari hata shule sikupenda sana,ebu fikiria ndugu darasani akili zimo ila shule sitaki kabisa,nawaona kaka wanakula bata na mapikipiki wamependeza na maviatu ya gharama kubwa kipindi kile ukivaa kiatu cha cat,timberland ma makoti ya leather unaonekana wewe mjanja hiyo na zungumzia 2004.

Nilipomaliza darasa la Saba tu niliwaambia wazazi naenda kutafuta pesa mgodini aisee hilo jambo lilikuwa kubwa sana kwa wazazi,ndugu walinishauri sana ila sikuwasikia nilipowaona kaka zangu walioniachia ziwa wanapesa za maana tena wakiwa na miaka 24 bado wadogo nilipatwa na tamaa la ajabu sana..

Wazazi hawakuwa nala kufanya walinipa baraka zote mwanangu nenda kapambane:nikiwa na miaka 15 kwa mara ya kwanza naingia merelani hiyo mgodini dingi na maisha ya kule sio ya kitoto.unaambiwa hivi mgodini na bandarini ndo kazi za hatari zenye kuogopesha,ila siku ogopa chochote.

Kwa mara ya kwanza naingia merelani simanjiro nikiwa juu ya pikipiki cc 250 la brother nikiwa na miaka 15 tuu sio powah arifu


Itaendeleeaaa...
 
Natumaini wote wazima humu,japo changamoto zipo ila tunatakiwa tukomaye nazo maana haina jinsi:

Hizo changamoto tumeumbiwa sisi binadamu,hata uende wapi zipo pale zinakusubiri.

Nimependezewa niwaletee niliyoyapitia katika ukuaji wangu mpaka nilipofikisha 20s,najua utajifunza moja au lingine.

Mangi shangali..
ARUSHA,TANZANIA.

YAFUATAYO YANAFURAHISHA..

UTANGULIZI:-
NIlizaliwa miaka ile ya 90s katika hospital ya mount meru iliyopo katika jiji la arusha.kipindi hicho baba alikuwa anafanya kazi katika benki ya nbc,mama alikuwa mfanya biashara soko kuu arusha kipindi hicho soko lilikuwa linaitwa soko la bondeni kitambo hicho..

Katika ukuaji wangu na story nilizopewa na wazazi wangu pamoja na ndugu zangu waliokuwa nami nilipokuwa mtoto.

Mama anasema nilikuwa mtundu sana tena ujeuri,nilipokuwa na miaka 4 nilikuwa najifungia kwenye friji,kwa watu wanajua yale mafriji ya zamani yalikuwa makubwa sana sasa nilikuwa naingia ndani,nakujifungia humo mama ananitafuta kumbe nipo ndani ilikuwa tafurani sana.

Mama anasema nilikuwa nashika kiwembe najikata mwenyewe mkononi na hata sitoi chozi,nilikuwa na matukio ya hatari kuna siku nilichomeka pasi mkutani nikipigwa na shoti nikazimia kwa masaa 6 watu walijua nimekufa.

Tulikuwa na mtindo wa kudandia gari kwa nyuma, lilechuma lakupanda lilikuwa limeoza kuwa kutu silikakatika bana niliburuzwa mpaka ngozi kwenye tumbo zikatoka.

Aisee ngoja nifupishe maana nilikuwa na matukio ya hatari sana ambayo kama sio kudra za mwenyenzi MUNGU nisingekuwa hai leo hii..

Nilipofikisha umri wa kwenda darasa la kwanza nilijiunga katika shule ya sanawary iliyepo arusha,nilisoma vinzuri mpaka kufika darasa la 4 ndio tatizo lilianza maana nilikuwa ujeuri shuleni na mkorofi,wanafunzi niliyesoma nao kipindi hicho walipata joto ya jiwe maana nilikuwa sionewi ovyo,nilikuwa napigana na walionizidi darasa tena la saba.

Shule tulikuwa na tabia ya kupigana
Tunaenda mtoni huko hakuna watu,natafutiwa mbabe wanaomuona ubabe wao natembeza kichapo heavy nikawa naogopeka shule nzima mpaka vijana wa darasa la Saba waliniwazia maana nishawatandika wababe wao .walimu walipata tabu nilipogoma kusoma hakuna mwalimu alithubutu kunichapa nilipochelewa namba na usafi sikupe ratiba yeyote ya usafi darasani.

Niliingia shule mda walimu wanaingia tena mikono mfukoni,nilikuwa mkorofi ila darasani sikuwahi kushuka chini ya mtu wa 5,matokeo ya mitihani nilifanya vyema.

Itaendeleea...
Acha utoto, eti nilizaliwa miaka ya 90 kitambo hiyo. We bado mdogo ndiyo maana unaandika mambo ya kitoto
 
Back
Top Bottom