Gharama kufuru za matibabu hospitali za umma ni kwa uhalali upi?

Gharama kufuru za matibabu hospitali za umma ni kwa uhalali upi?

Uko sahihi, lakini amezalisha nini?
Sio kila mtu anakuwa front Kuna ma think tank wanalipwa kwa kuwa think tank

Na mnywa pombe ndie analipa Kodi kubwa mno direct kabisa

Alafu mnalia apa Kodi yake ukilipie huduma binafsi
 
Kwanini mmeshindwa Kuweka za halali na zisizo halali ?

Weka huduma kadhaa linganisha na nchi nyingine tuone kwetu zipo juu

Za halali au za haramu siyo namba inayotoka mbinguni.

Uhalali na uharamu unatokana na ghrama za uzalishaji.

Kama gharama ya kuzalisha huduma ni thamani "x" na tunauziwa "10,000x" bei hiyo siyo halali.

Ninyi mnaodhani bei zenu mnazotupa ni halali ziko wapi "x" tujiridhishe?
 
Anaekunywa pombe analipa Kodi kubwa Sana ya VAT kuliko anaeshindwa kununua maharage

Tofauti yake hii hapa:

Fo1QpvoWYAEstsH.jpeg


Uthibitisho huu hapa:

Fnn4deYWYAE-Pmf.jpeg
 
Za halali au za haramu siyo namba inayotoka mbinguni.

Uhalali na ujaramu unatokana na ghrama za uzalishaji.

Kama gharama ya kuzalisha huduma ni thamani "x" na tunauziwa "10,000x" bei hiyo siyo halali.

Ninyi mnaodhani bei zenu mnazotupa ni halali ziko wapi "x" tujiridhishe?
Halali inalinganishwa na haramu ili uwe na haramu lazima uwe na halali

Weka apa haramu na halali
 
Halali inalinganishwa na haramu ili uwe na haramu lazima uwe na halali

Weka apa haramu na halali
Nini usichoelewa? Weka itemized cost ya unachouza tujiridhishe?

Kama MRI ni 350,000/-

1. Umeme shilingi ngapi?
2. Machela shilingi ngapi?
3. Shuka shilingi ngapi?
4. Nk.

Wanaokuuliza hawa hapa:

FpPZ7dKWAAMHQrq.jpeg


Kuweni na aibu japo kidogo kuwaambia ukweli ndugu hawa MRI bei ni afutatu kama ndiyo gharama yake.

Kulikoni kuwaibia watu kama hawa au hata marehemu?

Cc: elmis
 
Sio kila mtu anakuwa front Kuna ma think tank wanalipwa kwa kuwa think tank

Na mnywa pombe ndie analipa Kodi kubwa mno direct kabisa

Alafu mnalia apa Kodi yake ukilipie huduma binafsi
Ingekuwa hivyo, tungekuwa na visima vingi vya kuchimba mafuta na kuuza nje
 
Ila we jamaa bana , ungechimba mafuta unajua mafuta yapo kila sehemu 😂😂😂
Ni wazawa wangapi wapo kwenye utafiti wa kujua hapa kuna mafuta au hapana?Na je, wametoa mapendekezo gani, na hatua zipi zimechukuliwa?
 
Waache blaablaa aisee mimi nimelipishwa 250,000 Moshi kcmc hosptal kubwa kabisa...

Kigezo chao hapo fully private labda wangelipisha 320,000/- hivyo hospitali ya umma ni bei ndogo zaidi ...
 
Cost sharing. Zinahitaji fedha kwa ajili ya kujiendesha bila kutegemea ruzuku kutoka mfuko mkuu wa Hazina. Ruzuku inabaki kama sehemu tu ya mapato ya hospitali.
Hata kama ni cost sharing gharama ni kubwa sana hazina Uwiano ukizingatia hiyo ni serikali
Jana na juzi watu wawili nimewasikia wanalalamika, mmoja mtoto mchanga amelazwa Amana siku 5 bill ikaja laki 3.
Akapewa referral kwenda Muhimbili amkaa wiki bill mil 1 na ushee.
Mimi mwaka juzi mke wangu alifanyiwa operesheni kutoa mtoto aliyefia tumboni akakaa pale siku ICU siku kama 3 na wodini siku 2 bili ikaja mil 2 na ushee nikawaambia kulikoni wakasema hakuna namna kama huna aendelee kukaa wodini siku ukipata unakuja kumkomboa
 
Hata kama ni cost sharing gharama ni kubwa sana hazina Uwiano ukizingatia hiyo ni serikali
Jana na juzi watu wawili nimewasikia wanalalamika, mmoja mtoto mchanga amelazwa Amana siku 5 bill ikaja laki 3.
Akapewa referral kwenda Muhimbili amkaa wiki bill mil 1 na ushee.
Mimi mwaka juzi mke wangu alifanyiwa operesheni kutoa mtoto aliyefia tumboni akakaa pale siku ICU siku kama 3 na wodini siku 2 bili ikaja mil 2 na ushee nikawaambia kulikoni wakasema hakuna namna kama huna aendelee kukaa wodini siku ukipata unakuja kumkomboa

Ungekuwa na bima labda ungelipa kidogo zaidi. Lakini mfuko wa bima ungeweza kutozwa hata mara 2 zaidi ya hapo.

Kichekesho kilichopo ni kuwa mifuko ya bima yenyewe hailalamiki kuhusiana na hizi bei, ila inataka watu wote wawe na bima hasa walio wazima Ili waweze kumudu kulipa hata kama bei hizi zitapandishwa zaidi 🤣🤣.

Kwanini tusiamini kuwa mwenye hospitali ndiye mwenye bima?

Kwamba kumbe sisi umma tunaolipa pia mishahara yote kwenye hospitali hizi kama ni uzuzu, basi na uzezeta pia.
 
Cost sharing. Zinahitaji fedha kwa ajili ya kujiendesha bila kutegemea ruzuku kutoka mfuko mkuu wa Hazina. Ruzuku inabaki kama sehemu tu ya mapato ya hospitali.
Pamoja na hiyo cost sharing lakini wakati mwingine hizo gharama huwa haziendani kabisa na huduma iliyotokewa, nitatoa mfano: mgonjwa wetu alipelekwa Mloganzila baada ya kubainika na matatizo ya Figo. Baada ya kupokewa alikaa bila huduma mpaka siku ya 5 (huduma ya kusafisha damu). Huduma halisi ya kusafisha damu ilianza day 6 na baada ya siku 2 akafariki. Katika kipindi chote hicho waliokuwa wanashughulika na mgonjwa ni wanafunzi, daktari nilimuona only one day. Sasa njoo kwenye bili sasa yaani siku zote alizokuwa pale wameweka mpaka gharama za madaktari, manesi, etc... Yaani unakuta kabisa daktari hajaja kumuona mgonjwa pale wodini, ni wale wanafunzi ndiyo wapo hapo ku attend wagonjwa lakini eti bili inasoma gharama za daktari hii ni uonevu. Unaambiwa gharama za kitanda elfu 50 kwa mfano lakini hapo hapo mpaka gloves na vifaa vingine viko kwenye bili pia. Sasa unajiuliza hicho kitanda ndiyo elfu 50?? Hata hotel ukilipa 50,000 utakuta sabuni, taulo, na breakfast juu...
 
Kila mmoja wetu anatakiwa kuwa na bajeti ya matibabu. Na hapo ndipo inapokuja umuhimu wa Bima ya Afya kwa wote.
Bima tuu ya NHIF inabagua matibabu, mara huduma hii bima haiko covered na bima, sasa ndiyo bima kwa watanzania wote milioni 61 itawezekana kweli?
 
Hili blanket la kusema tu kuhusu bodi haitoshi maana tunaolipa ni sisi iwe moja Kwa moja au kupitia bima.

Ipo hatari kubwa ya kuwa tunapigwa.

Tupewe wazi wazi vigezo hivi maana majengo ni ya umma na wafanyakazi ni wa umma pia.
Exactly mfano hapo Mloganzila au MOI, wanakupa bili ikionyesha kwamba kuna gharama za kila siku za madaktari, manesi etc kumbuka hiyo ni mbali na gharama za kitanda na vifaa mbalimbali na madawa. Huwa najiuliza kwanza unakuta madaktari wenyewe wanakuja mara chache most of the time ni wanafunzi ndo wako wodini, lakini kwa nini kuwe na gharama za madaktari na manesi daily? Hawa si wanalipwa mishahara? Kwa nini kusiwe na consultancy fee inayolipwa just once? Kwani hii ni private hospital? Majengo yamejengwa kwa fedha za umma, vifaa vyote ni vya umma etc etc
 
Back
Top Bottom