DOKEZO Gharama mpya ambazo Aga Khan wanataka walipwe kwa wateja wa NHIF ni kuhujumu nchi. Haikubaliki

DOKEZO Gharama mpya ambazo Aga Khan wanataka walipwe kwa wateja wa NHIF ni kuhujumu nchi. Haikubaliki

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Umaskini mbaya sana ndugu yangu
Kabisa, ujue Kuna watu wanalipa cash hawatumii na Wana uwezo wao, hivyo sisi wa Hali ya chini twende hosp za size zetu, kulalamika hakufai Kila 1 anakula urefu wa kamba yake.🤪
 
Mkuu kuna kitu kinaitwa class hata bima za nhif baadhi tu wanaotibiwa pale na wala huwezi kusikia wanalalamika ila wenzangu na mm lazima uone mil 6 nyingi.
 
Dah aisee hatari sana.

Wahindi nao bila shaka wanalipa gharama hizohizo wakienda kutibiwa?
 
View attachment 3069948Hospitali ya Aga Khan wanataka kutoza Shilingi 6,000,000/= kwa huduma za kujifungua kwa njia ya upasuaji wakati Hospitali nyingine zenye hadhi sawa ...
Kwa kifupi mnajipeleka kujichanganya na hawa wahindi lakini hawakutaka muende huko.

Ni hospitali yao na ni kwaajili ya wao matajiri.

Walianza kupokea NHIF majuzi tu lakini wao walikuwa wanpokea Strategies, AAR, VISA BUD na kadi zingine za kimataifa.

Huwezi kuwapangia bei, mnbona hamlalamiki soda pale kempisky inauzwa elfu kumi na tano?

Hospitali ya Aga Khan inamilikiwa na Aga Khan Development Network (AKDN), ambayo ni mtandao wa mashirika yanayoongozwa na Imam Aga Khan, kiongozi wa kiroho wa Waismailia. AKDN inahusisha mashirika kadhaa yanayojihusisha na sekta mbalimbali, ikiwemo afya, elimu, maendeleo ya kiuchumi, na utamaduni, lengo likiwa ni kuboresha hali ya maisha ya watu katika nchi zinazoendelea.

Hospitali ya Aga Khan ni sehemu ya mtandao wa huduma za afya zinazomilikiwa na kuendeshwa na AKDN.
 
View attachment 3069948Hospitali ya Aga Khan wanataka kutoza Shilingi 6,000,000/= kwa huduma za kujifungua kwa njia ya upasuaji wakati Hospitali nyingine zenye hadhi sawa ya rufaa ya Kanda wanatoza kiasi cha Shilingi 230,000/= huku bei ya juu katika baadhi ya Hospitali ikijumlisha na huduma ziada hutoza kiasi cha Shilingi 600,000/=. Aga Khan wanataka kulipwa maradufu kwa asilimia 100 zaidi kuliko Hospitali nyingine.

Huduma ya kulaza wagonjwa mahututi katika Hospitali ya Aga Khan wanataka kulipwa kiasi cha Shilingi 2,278,933, huduma hii kwenye Hospitali nyingine huwa ni kiasi cha shilingi 500,000/= na Shilingi 700,000/= ambayo ni bei ya juu katika baadhi ya Hospitali ukijumuisha na huduma za ziada.

Aga Khan wanataka kutoza kiasi cha Shilingi 334,546 kwa huduma za uchunguzi kwa kupitia CT-Scan huku Hospitali nyingine zinatoza 120,000 hadi 150,000 ikiwa ni bei ya juu katika baadhi ya Hospitali ukijumuisha na huduma za ziada. Kwanini bei iwe juu hivi? CT-Scan hizi hizi ambazo tumeona Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan amezinunua na sasa huduma zinapatikana nchi nzima kwenye Hospitali zote za Rufaa za Mikoa na nyinginezo ngazi za juu. Najiuliza Gharama zote hizo zinakuja kwa msingi upi?
Wasifunge hospital tu, wafunge na shule zao waondoke. Agha Khan ni taasisi ambayo inasamehewa kodi nyingi kuliko taasisi nyingine yoyote hapa nchini. Mwanzoni wakiingia MoU na Serikali waliomba wasamehewe kodi ili watoe huduma nafuu kwa Watanzania walio wengi. Mwisho wa siku huduma zimekuwa ghali kuliko mahala pengine popote. Hawa waondoke wala wasisumbue watu.
 
Kwanza Agakani tofauti na kufanya usafi kwenye tiba wana Madaktari Intern wote yaani hamna kitu pale
Ukienda na Mkeo hata kama hana shida ya kujifungua lazima afanyiwe upasuaji ingawa hili limekua janga la nchi nzima hasa miji mikubwa kila mtu kujifungua ni upasuaji ni aibu sana
Watu wanapiga hela tu 🤣 nchi ya kitu kidogo
 
Hapo kuna wakati fulani mgonjwa wetu alikaa jengo la pavilion
Na alilazwa week 3 huo mkeka ulivyotoka syo poa
Pale waende wenye kibunda,ila all in all mm binafsi napakubali sana muhimbili

Ova
Hahahah Aga Khan tulimpeleka ndugu alipata ajali ya pikipiki mfupa wa paja ukavunjika baada ya week bili ilikuja 25M yani bahati nzuri jamaa ni staff wa absa tena wa kwenye senior position ofisi ikasimamia show.
 
Inaonekana uelewa wako mdogo. Mteja wa NHIF akienda pale Aga khan au hata Saifee huduma kama ni hiyo ya Uzazi kwa njia ya upasuaji yeye atahudumiwa sawa na yule aliyekuwa Saifee au hata Mbeya. Ishu hapa iko kwa NHIF ambaye analipia huduma ambayo mwanachama wake amepata. Huduma hiyo Aga Khan anataka alipwe 6m wengine kama saifee wanachaji 600k. Na hapo kumbuka Aga khan sio wateja wote wa NHIF wanapokelewa. Hatari na nusu.
Wateja gani hawapokelewi Aga Khan?
 
Kwani ni lazima wateja wa NHIF kutibiwa Aga Khan ?
Uko sahihi Kila siku serikali inaimba hospitali za serikali na huduma zake zimeboreshwa waende huko hospital za private waachie wale wa Private sector ndio watumie hizo huduma ambao wengi Wana bima za Afya private sio hizo za NHIF

Wa NHIF serikali iwaambie kabisa kuwa mtatibiwa hospitali za serikali tu

Hizo private hospitals waachane nazo
 
View attachment 3069948
Hospitali ya Aga Khan wanataka kutoza Shilingi 6,000,000/= kwa huduma za kujifungua kwa njia ya upasuaji wakati Hospitali nyingine zenye hadhi sawa ya rufaa ya Kanda wanatoza kiasi cha Shilingi 230,000/= huku bei ya juu katika baadhi ya Hospitali ikijumlisha na huduma ziada hutoza kiasi cha Shilingi 600,000/=. Aga Khan wanataka kulipwa maradufu kwa asilimia 100 zaidi kuliko Hospitali nyingine.

Huduma ya kulaza wagonjwa mahututi katika Hospitali ya Aga Khan wanataka kulipwa kiasi cha Shilingi 2,278,933, huduma hii kwenye Hospitali nyingine huwa ni kiasi cha shilingi 500,000/= na Shilingi 700,000/= ambayo ni bei ya juu katika baadhi ya Hospitali ukijumuisha na huduma za ziada.

Aga Khan wanataka kutoza kiasi cha Shilingi 334,546 kwa huduma za uchunguzi kwa kupitia CT-Scan huku Hospitali nyingine zinatoza 120,000 hadi 150,000 ikiwa ni bei ya juu katika baadhi ya Hospitali ukijumuisha na huduma za ziada. Kwanini bei iwe juu hivi? CT-Scan hizi hizi ambazo tumeona Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan amezinunua na sasa huduma zinapatikana nchi nzima kwenye Hospitali zote za Rufaa za Mikoa na nyinginezo ngazi za juu. Najiuliza Gharama zote hizo zinakuja kwa msingi upi?
aAgha Khani ni wezi miaka mingi walikuwa hawajashtukiwa tu.
 
Back
Top Bottom