DOKEZO Gharama mpya ambazo Aga Khan wanataka walipwe kwa wateja wa NHIF ni kuhujumu nchi. Haikubaliki

DOKEZO Gharama mpya ambazo Aga Khan wanataka walipwe kwa wateja wa NHIF ni kuhujumu nchi. Haikubaliki

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Hahahah Aga Khan tulimpeleka ndugu alipata ajali ya pikipiki mfupa wa paja ukavunjika baada ya week bili ilikuja 25M yani bahati nzuri jamaa ni staff wa absa tena wa kwenye senior position ofisi ikasimamia show.
Hospital za private ni Kwa ajili hasa ya private sector

Serikali sjui Kwa Nini wanalazimisha vi NHIF vyao vitambulike hospital za binafsi
Kampuni za private hukatia wafanyakazi wao bima ya Afya kubwa sana wakijua gharama za private hospitals ziko juu sana

Serikali iache uchokozi Kila mwenye NHIF aaambiwe hii kadi ni Kwa ajili tu ya hospitals za serikali full stop

Baada ya hapo hutasikia kelele kutoka hospital yeyote ya private iwe agha Khan nk
 
Inaonekana uelewa wako mdogo. Mteja wa NHIF akienda pale Aga khan au hata Saifee huduma kama ni hiyo ya Uzazi kwa njia ya upasuaji yeye atahudumiwa sawa na yule aliyekuwa Saifee au hata Mbeya. Ishu hapa iko kwa NHIF ambaye analipia huduma ambayo mwanachama wake amepata. Huduma hiyo Aga Khan anataka alipwe 6m wengine kama saifee wanachaji 600k. Na hapo kumbuka Aga khan sio wateja wote wa NHIF wanapokelewa. Hatari na nusu.
Si uende huko Kwa rahisi au umelazimishwa kwenda Aga Khan
Hizo akili za kijinga ndo Zinaua uchumi

Soda MITA 100 KUTOKA mlimani city ni 600 Ila NDANI kule Bei ni tofauti
Na hotel zingine pia
Unajua sababu

Unajua kwanini NDANI ya ndege moja nauli zinatofuatiana zaidi mara tatu
 
Soda kwenye duka la mangi unainywa kwa shilingi 600, soda hiyo hiyo ukitaka kuinywa pale Samaki samaki mlimani City utainywa kwa shilingi 3000, gharama mara tano zaidi. Umeelewa nini?

Kinachoamua bei ya bidhaa au huduma ni Class ya mtoa huduma iliyolenga Class fulani ya wateja.
Kwahiyo mamlaka za udhibiti zote zifutwe ili kila mmoja apange bei ya huduma yake ?
 
Sema kwa ma diaspora pale lazma mpate huduma first classe
Kuna kipindi pale nlikuwa na mgonjwa ulikuja mkeka huo wa mln karibia 50
Shuguli ilikuwa syo ndg
Zile doctor visits 😄 nk balaaa
Watu kwenye kulipa tulitafutanaa

Ova
 
Agha Khan wanachukua Kodi zako kiasi gani ?

Nadhani badala ya kulalamika hawa watu binafsi wanachaji sana unelalamika wale ambao wanatumia pesa zako huduma hazikidhi haja....

 
We umakata kabima ka laki mbili unataka kwenda AG ,Kairuki si kitafuta shida huko,mbao hopeana sanaa
Kabisa kama mfuko wako mdogo agakhan pita napo mbali 😄
Acha twende mwananyamala tu

Ova
 
Shida si kwamba Agakhan wanatoza kiasi gani ,shida ni NHIF ,kwa ambaye anasikiliza yule mwenyekiti wa umoja wa hospitali binafsi juzi akiongelea hili suala akasema issue ni ucheleweshaji wa malipo katika hivyo vituo vya afya vya private , ukizingatia wao hawapati ruzuku ya aina yoyote toka serikalini , hospitali za serikali mishahara , vifaa tiba ,ukarabati ,kodi ndefu nk na vitu vingine vinapata fungu toka wizara wapate hasara au wasipate ,kitu ambacho ni tofauti na private institutions ambapo wanalipa mishahara , ukarabati ,ujenzi ,vifaa tiba nk vyote vinategemea mapato ya huduma zao.
Na alisema vituo vingi bado vitaendelea kukataa hizo bima za NHIF na si Agakhan tu .
NHIF ni scam kama serikali yenyewe tu ilivyo scam
Wewe unalipa 54000 halafu unataka upate huduma ya mtu ambaye analipwa package ya milioni + kwa bima kama AAR ,au strategis nk

Ni mjinga pekee ambaye anaweza tengeneza hoja mfu kama hiyo na kuwalaumu Agakhan .
Kwani NHIF walikuwa wanawapa hizo pesa kama ruzuku ?
Si transaction ilikuwa inafanyika ? ,Kwamba wewe inapeleka makalio yako kutibiwa pale na wenyewe wanaingiza pesa kutokana na dawa na huduma ambazo wamekupatia kulingana na ratings zao ?
Au kwani mnapoendaga kununua vitu madukani huwa bei ni moja hiyo hiyo kwa kila duka na kila sehemu ?
 
Kuna kipindi pale nlikuwa na mgonjwa ulikuja mkeka huo wa mln karibia 50
Shuguli ilikuwa syo ndg
Zile doctor visits 😄 nk balaaa
Watu kwenye kulipa tulitafutanaa

Ova
Hahahahah 50M sio poa mzee
 
Tukirudi kuhusu NHIF wana shida
Kwenye kuwalipa vituo vya huduma ya afya

Ova
 
We umakata kabima ka laki mbili unataka kwenda AG ,Kairuki si kitafuta shida huko,mbao hopeana sanaa
Yaani Agha Khan kumejaa wagonjwa malofa kibao mtu anaharisha mbio Agha Khan

Dunia nzima Kuna hotel za VIP,Shule na vyuo vya VIP , Hospital za VIP nk
Huwezi geuza hospital kama ya Agha Khan iwe kama ya serikali Cha wote kutaua quality na status

Bima ndogo waende hospital serikali

Bima zote za NHIF waende hospital za serikali tunakoambiwa Kila siku kuwa huduma zimeboreshwa kuanzia majengo,madaktari na huduma za Afya
 
Najiuliza Gharama zote hizo zinakuja kwa msingi upi?
Propaganda hizi ujue...hiyo hospitali mliyoiingiza ya Saifee, gharama ya uzazi kwa kisu ni tsh 4,000,000

Sasa hiyo tsh 700,000 ni ya wapi?
 
View attachment 3069948
Hospitali ya Aga Khan wanataka kutoza Shilingi 6,000,000/= kwa huduma za kujifungua kwa njia ya upasuaji wakati Hospitali nyingine zenye hadhi sawa ya rufaa ya Kanda wanatoza kiasi cha Shilingi 230,000/= huku bei ya juu katika baadhi ya Hospitali ikijumlisha na huduma ziada hutoza kiasi cha Shilingi 600,000/=. Aga Khan wanataka kulipwa maradufu kwa asilimia 100 zaidi kuliko Hospitali nyingine.

Huduma ya kulaza wagonjwa mahututi katika Hospitali ya Aga Khan wanataka kulipwa kiasi cha Shilingi 2,278,933, huduma hii kwenye Hospitali nyingine huwa ni kiasi cha shilingi 500,000/= na Shilingi 700,000/= ambayo ni bei ya juu katika baadhi ya Hospitali ukijumuisha na huduma za ziada.

Aga Khan wanataka kutoza kiasi cha Shilingi 334,546 kwa huduma za uchunguzi kwa kupitia CT-Scan huku Hospitali nyingine zinatoza 120,000 hadi 150,000 ikiwa ni bei ya juu katika baadhi ya Hospitali ukijumuisha na huduma za ziada. Kwanini bei iwe juu hivi? CT-Scan hizi hizi ambazo tumeona Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan amezinunua na sasa huduma zinapatikana nchi nzima kwenye Hospitali zote za Rufaa za Mikoa na nyinginezo ngazi za juu. Najiuliza Gharama zote hizo zinakuja kwa msingi upi?
Kwenda Agha khan na hauna hela ni kutafutia watu waonekane wabaya tuu...Si kuna Hizi Kairuki, Kitemgule, Bochi na zipo vizuri tuu
 
Mbona hausemi pia wanatozwa kodi kubwa sa unataka wafanye kitu kisichowanufaisha huku ukionekana wazi kuitetea serikali mara sijui samia kanunua ct scan kwani ametoa hela zake mfukoni eeeh.
Serikali ipunguze kodi za huduma za afya na madawa wananchi tutibiwe vema na pia iwalipe wenye hospital maana watu wa bima huchelewa sn kulipa madeni yao.
 
Kwanza Agakani tofauti na kufanya usafi kwenye tiba wana Madaktari Intern wote yaani hamna kitu pale
Ukienda na Mkeo hata kama hana shida ya kujifungua lazima afanyiwe upasuaji ingawa hili limekua janga la nchi nzima hasa miji mikubwa kila mtu kujifungua ni upasuaji ni aibu sana
Acha fix wewe. Unafikiri wote humu ni watu wasiojitambua kama ww.
 
Back
Top Bottom