Gharama ya kutuma fedha kupitia mitandao kwa sasa ni ghali

Koryo2

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2016
Posts
2,056
Reaction score
2,519
Gharama ya kutuma fedha kupitia mitandao kwa sasa ni ghali mno na inatukatisha tamaa. Kutuma mathalani Tshs.1m/= kwa anayetuma anakatwa Tshs.16,000 na anayepokea anakatwa Tshs.14,000.

Hivi kweli ni haki?. Kwa Mtanzania wa kawaida kiasi hicho anaweza kununua madebe matatu ya mahindi kwa ajili ya familia au kilo 4 za nyama kwa ajili ya familia. Nina imani watu wengi watahamia Benki na kuanzia sasa mimi binafsi nimeacha kutumia mitandao kwa ajili ya kutuma fedha.

Uamuzi uliofanywa na Serikali ulikuwa uamuzi ambao hauna manufaa kwa wananchi.
 
Mbona unaongelea Watanzania wa kawaida halafu unataja MILIONI, unawajua Watanzania wa kawaida wewe?
 
Hilo ndilo suluhu
Kutuma na kupokea pesa kupitia benki
 
Haya makato yanaanza lini? Una uhakika anaepokea anakatwa hela (14,000)?
 

Kwa zamani ilikuaje
 
Jana usiku nimetuma sh milioni moja na elfu themanini, nimekatwa 5,000.00
 
CCM ilishafeli siku nyingi sana,ni matahiri pekee ndiyo wanayoiamini kwa sasa.
Na wanang'ang'ania zile sehemu nyeti kama simba. Simba wakati wa kuwinda akishika winda, anakaba koo kwani anajua windo haliwezi kujitetea kirahisi. Serikali nayo inajua ''wadanganyika'' ni mafukara wa kutupwa, hivyo suala la kuhemea kwa kutumiana visenti haliepukiki. Wanang'ang'ania hapo hapo. Mpaka siku ''mdanganyika'' atakapoamka na kujikomboa tusitegemee mambo kujibadilisha yenyewe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…