Gharama za umeme zimepanda lini? Tsh.10,000 kwa unit 72 badala ya 82 imekuwaje?

Upo mji gani? Kijijin au mjini?
 
Mkuu unatumia mita ipi nami niipambanie kuipata?
 
Iyo elfu 10 kwa tariff 4 ama 0 mbona haiendani na hela iyo,nijuavyo mie ni kuwa Taiff 4 mwisho wa kununua ni elfu 9 na unapata unit 75,sasa izo 82 unapataje mwenzangu.
Ni 72.3 if am not mistaken kama sio 73
 
He!!! Wenzio 10.000 tunapata unit 28!!!! Wewe basi unapata nyingi sana. Inakuwaje?
 
Sahivi unit ni 10 tu afu sio lazima uende Tanesco. Inasemekana kuna automatic verification umeme ule wa mkopo ukitoboa siku zaidi ya 7... Halafu kuna ile tarrif ya 3000 'kama sijasahau kwa mwezi ni ipi? Kuna nyumba nilipanga lol hata kuchemsha maji huwezi, ukiweka tu jagi umeme unazima
 
Inshu sio kuingia, bali kuweza kubakia humo, kwani kwa siku unatakiwa usitumie zaidi ya units 2.5, je kwa matumizi yako una sifa hizo?
Mkuu mimi natumia chini ya hizo kabisa.

Mbona sasa nanunua 10,000 unit 28.
 
Mkuu mimi natumia chini ya hizo kabisa.

Mbona sasa nanunua 10,000 unit 28.
Kwa watumiaji wa tariff 4 pekee ndo wanapata unit 77 kwa 9150.Ila kama hujahamishwa tarrif utapata hzo 28 units kwa 10k
 
Nawezaje kujiunga tariff 4 kutoka hii nilipo?
Unaandika barua kwenda kwa menneja kuhamishiwa hiyo tarif 4 lakini lazima ukidhu masharti watakuja kufatilia nyumbani kwako wakihisi unakidhi ila kama ukiona kimya ujue hauna vigezo kuwekwa kwenye Tarrif 4.
 
Mkuu mimi natumia chini ya hizo kabisa.

Mbona sasa nanunua 10,000 unit 28.
Ni sawa, hilo haliji automatically tu, lazima uende tanesco uandike barua, ndio waangalie, wakiona unastahili watakuhamisha tarrif
 
Ok!hahaaa sasa hizo units 10, utoboe zaidi ya siku saba kweli , ?ni ngumu, hakuna tarrif hiyo ya 3000, umeme unazima kwa kuisha au kuna shoti?
 
Sometimes ukitaka majibu ya uhakika hatua ya kwanza ni kuwauliza wahusika (direct from the horses mouth) na kama una alternative kuliko kuwasubiri wajibu hapa jaribu kupiga simu / kuwatembelea ofisi zao za karibu.
ni kweli umedhurumiwa nenda ofisi husika kuliko kuja na kulalamika bila msaada
 
Inshu sio kuingia, bali kuweza kubakia humo, kwani kwa siku unatakiwa usitumie zaidi ya units 2.5, je kwa matumizi yako una sifa hizo?
Mimi natumia around 2 units per day,
kwa hiyo kuna uwezekano mkubwa wananiibia kwa kuniweka kwenye kundi nisilostahili ?, halafu huo utaratibu ni wa kijinga, kwanini wasiweke standard ?, yaani mtu ukitumia zaidi basi unaonekana fisadi, wangeweka standard ili mtu unapotumia zaidi unalipa kadri ulivyotumia, nasikia hata ukienda kuwaomba wakuhamishe wanasumbua sana ??, natamani tungepata shirika binafsi la ugavi wa umeme ili lishindane na kugawana wateja na hawa wezi tanesco
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…