Godbless Lema akamatwa Kajiado akitorokea Kenya yeye na familia yake. Kurudishwa nchini kesho Novemba 9, 2020

Binafsi nisichangie chochote kumhusu.

Ila tu. kama nchi yangu Tanzania ip katika hii hali wanasiasa wanayotaka kutuaminisha, tusingeshindwa kuingia mtaani na kuwaunga mkono.

Mbona hapa kitaa barida tu.
We endelea kuimba na kusifu mkuu hakuna shida
 

Mkuu bora na ww utusaidie kupambana na hilo tikiti maji, huwa hajui lolote zaidi ya kupiga propaganda mfu hapa jukwaani.
 
Sasa nimeamini liberal politics and dramas , are two in one.

Chakula kinapotea wanalazimisha kipatikane kwa njia nyingine.

Ukianguka kisiasa unachotakiwa kufanya ni kujipanga kwa ajili ya vita vya kisiasa vya kesho.

Wanaongopa fedheha wakiwa njee ya Bunge? Njooni muwe kama sisi tunavyojenga chama, msiharibu local politics na political parties kwa kutafuta tonge.

Mtapata waungaji mkono ambao wanafikiri maisha ya kisiasa ni tonge na ni leo kama Lema, 1,900,000 Electoral voter needs leadership and to be made
members of Chadema.
 
Hakuna mjadala usio na mifano, hata huko kwenye nyumba za ibada anayejadiliwa ni Mungu, lakini haizuii shetani kuongolewa. Labda useme umekuja na marking scheme humu jukwaani.
Mifano yako haifanani na kinachoongelewa hapa
 
Chadema walitaka wananchi waandamane ila wananchi wakakataaa kuwapa support ndio maana tunasema Chadema hamna popular support mlihamasisha maandamano wananchi hawakuitikia wito huo sababu wanajua hamna dhuluma.

Vita vya Kagera ambavyo vilipivanwa na watanzania walioungana na waganda waliokuwa wanapinga uovu wa Amini vilikuwa na support kubwa kwa wananchi ndio maana nakuambia Museveni alikuwa na support kubwa ya wananchi maana walikuwa wanataka maovu na ubaya wa Amin uondoke. Sawa na wananchi walivyompa Kabila sapoti ya kumg'oa Mobutu.

Hata hapa Tanzania kama kuna uonevu na unyanyasaji kama wa Amin au Mobutu unadhani watanzania wasingeomba msaada toka nje? Jibu ni kuwa hakuna unyanyasaji wala maovu dhidi ya wananchi kiasi cha kufananisha na Zaire ya Mobutuna Uganda ya Amin. Ndio maana watu wanamshangaa Lema kutafuta umaarufu kujifanya anatoroka. Kama kuna uonevu na ukiukwaji wa haki za binadamu Un hawana ofisi hapa mpaka aende Nairobi!

Sijakiri walimu kuchoshwa na mambo wasiolidhika nayo usinukuu vibaya. Mimi nilichomaanisha ni kuwa kama wanadai haki zao sio lazima waandamane. Kudai haki hakuna option moja tu ya kuandamana.
 
Mkuu, kwahiyo unaamini Lema kaangushwa kabisa Arusha na kwamba hana voters wa kutosha? Like for real? Yaani Tz nzima CHADEMA ina madiwani 15 tu!! Na kwako unaona ni realistic?

Kma watu wanadai kuna wizi basi wapeni benefit of doubt, ila kejeli wakati huu hazisaidii. Other factors zikiwa constant alafu CHADEMA ikaangushwa ndio muilaumu ila kuwashauri watafute wanachama million 2 ilihali mfumo wa uchaguzi una shida then ni misleading advice!!

Lissu na Saanane kuna watu walidai ni political stunts ila mwisho wake wote tuliona!
 
Achana na hayo ya Museveni na Kabila huko unazidi kujichanganya tu, maana walitolewa na wageni sio raia kwahiyo achana na huko.

Hoja hapa ni kwamba bila CHADEMA kuandamana ina maana hawana support sababu wananchi wameridhika, ndio nmetoa mfano wa wale wanafunzi waliotishia kuandamana kudai mikopo je walipotishiwa kufukuzwa na baadae wakaacha maandamano je ina maana waliridhika?

Naomba ujibu hili specifically
 
Kama ni hifadhi ya kisiasa, kwanini akina Nyalandu na Lema wasifute ofisi balozi zilizopo Dar kama TL

Kwanini wavuke mpaka?

What if wamezuiwa kwa kukosa Covid 19 Certification na wao wakasingizia kuzuiwa na polisi??

Lema amekamatwa kajiado akionekana kuvuka mpaka kinyume na sheria; kwanini a-paint picha mbaya dhidi ya Tanzania wakati hapa Tanzania angeweza kutafuta asylum bila kuzuiwa Kajiado ambako kavuka bila kuzingatia taratibu za kuvuka mpaka??

Kuna wakati wanasiasa wetu wana-play very cheap politics ili kutafuta public sympathy!

Well, labda kuna mtu kaandika script na hakuchimbua vya kutosha ili sinema hii "iuze"
 
Waliotaka kumuua 2017 alikuwa tishio kivipi hadi wakataka kumuua?
Unajuaje Walitaka kumuua kwa kuwa ni tishio na sio mzulumishi, inaonyesha mshajua sababu ya yeye kutaka kuuliwa.
 
Swali haliendani na mada husika. Maana Chadema walisema wataandamana na wakaomba wananchi waunge mkono. Sasa kuhusu vitisho,sidhani kama vitisho vinaweza kuzuia nguvu ya umma inayodai haki. Nilishudia Misri pamoja na kupiga watu risasi lakini Taharir Square ilikuwa inajaa watu na Mubarak alig'oka.
 
 
Mkuu bora na ww utusaidie kupambana na hilo tikiti maji, huwa hajui lolote zaidi ya kupiga propaganda mfu hapa jukwaani.
tindo hujui kuwa Museveni alishiriki kumg'oa Amini? Hujui kuwa Museveni na wenzake walipata sapoti ya wananchi?

Hujui kuwa Chadema haina sapoti ya wananchi ndio maana hata maandamano hayakufanikiwa?
 
Madeni yamewakimbiza wanadai kuna tishio la kuuwawa,

Hawa jamaa hawawezi survive nje ya politics.

Kiufupi wanasiasa wengi sana hawawezi ishi nje ya mfumo wa siasa, kipato chao kinatokana na siasa, haya ni makosa ya kimfumo.
 
tindo hujui kuwa Museveni alishiriki kumg'oa Amini? Hujui kuwa Museveni na wenzake walipata sapoti ya wananchi?

Hujui kuwa Chadema haina sapoti ya wananchi ndio maana hata maandamano hayakufanikiwa?

Amini alitoka madarakani lini, na Museveni aliingia madarakani lini na vipi, labda tuanzie hapo ili nijue kama unajua unaloongea, au unaandika tu kwakuwa unajua kuandika.
 
Amini alitoka madarakani lini, na Museveni aliingia madarakani lini na vipi, labda tuanzie hapo ili nijue kama unajua unaloongea, au unaandika tu kwakuwa unajua kuandika.
Ahaaaa, Amin alitoka madarakani baada ya vita vya Kagera mwishoni mwa 1979. Museveni aliingia madarakani mwaka 1986, ninaposem alimg'oa Amin sababu alikuwa ni mmoja wa makamanda waliopigana vita vya Kagera ili kumg'oa Amin. Tumia common sense acha hasira,tulia acha papara.
 
Unakimbilia tena Misri? Baada ya DRC na UG kukushinda Haaahaaa.

Ni hvi watu kutoandamana haimaanishi wamefurahi bali hawana namna ndio maana nmetoa mfano Mobutu na Amin hakuna alieandamana licha ya uhuni wao wa wazi kabisa.

Same to walimu na wadai mikopo hawakuandamana licha ya kupanga hivo mara kibao sio sababu waliridhishwa ila hofu ya Dr.Ulimboka n.k

Utaamini hya siku Tz ikipatwa na mabaya utaona tunavyogawanyika. Rejea ndege ilipokamatwa!!
 
Madeni yamewakimbiza wanadai kuna tishio la kuuwawa,

Hawa jamaa hawawezi survive nje ya politics.

Kiufupi wanasiasa wengi sana hawawezi ishi nje ya mfumo wa siasa, kipato chao kinatokana na siasa, haya ni makosa ya kimfumo.
Mwingine huyu hapa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…