Godbless Lema: Bora ya Magufuli kuliko Samia

Godbless Lema: Bora ya Magufuli kuliko Samia

Hana nia ya kurudia huyo. Anaona akirudi na matunzo kwishney.
Panatengenezwa uhalali wa kutokurudi ili aendelee kupetiwa petiwa na mabeberu yeye na familia yake.

Hata mimi ningekuwa Lema nisingerudi, watoto wake wanapata elimu bora kwenye mazingira bora kabisa. Watoto wakirudi hapa nchini baada ya elimu bora ya huko wanaweza kupata fursa nyingi kuanzia serikalini, sekta binafsi hadi taasisi za kimataifa. Kuliko arudi hapa kwenye nchi ya majoga, na akifanya siasa aishie kuwekwa lockup na majizi ya kura. Lema abaki hukohuko aendelee kufungua nchi.
 
Yale mambo ya hovyo yote yamerudi awamu hii.
 
Hivi rais gani atakuja kukubalika na Watanzania akiwa madarakani na baada ya kuondoka madarakani tangu turudi kwenye mfumo wa vyama vingi?

Magufuli alipoingia madarakani, watu wakaanza kumkumbuka Kikwete, leo Samia ameingia madarakani, Magufuli anaanza kukumbukwa!!

Itakuwa Tanzania tunahitaji katiba mpya kwakweli, ili kiongozi aliyepo madarakani aifuate hiyo katiba, ili asichukiwe na raia kwa sababu anakuwa anaongoza kwa kufuata katiba iliyotengenezwa na wananchi.

Kwa sasa kila rais anaongoza kwa utashi wake akiingia madarakani, hali inayopelekea huyu anakumbukwa, yule anachukiwa!

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Ukisubiria watanzania wakukubali unajisumbua,watu wanaangalia upande wao wakibaniwa walipotegemea maneno lundo wakipata sifa kwa Kiongozi so Kama wewe Ni Kiongozi focus kwenye ajenda zako.
 
Wanasiasa wa upinzani ni wapumbavu sana.. hasa huyo Lema anaendeshwa na mihemko

Una uhakika haya kasema Lema, au umetengenezewa ajali na huyu muhuni hapa umeingia kichwa kichwa?
 
Analeta propaganda tu huyo, kinachomfanya asirudi ni nini!?
 
Kuna ubaya gani mtu mmoja kumpigia mtu mwingine simu?Kuna mengi kwenye maongezi ya simu.Salamu,kujua mienendo ya nyumbani,kukumbushana jambo na kupeana taarifa.Unadhani alipompigia huyo mstaafu hakumsalimia kwanza?Unadhani hakuwa na jambo lingine ila kumwambia tu anataka kurudi Tanzania?
Mambo ya ubaya yametokea wapi? Au wewe ndie huyo mstaafu aliyepigiwa
 
Jawa wapinzani hawana wanachokisimamia wala kukiamini zaidi ya matumbo yao. No wonder Lissu alipoonana na Rais alizungumzia zaidi hela ya matibabu na kiinua mgongo chake cha ubunge. Mambo ya demokrasia n.k yalikuja nyuma km mazungumzo baada ya habari
 
Ni kweli, kwa kifupi CCM ni majanga - kero kubwa ni kuturusidha kwenye mgawo mkali wa umeme, ni dhahiri shahiri CCM imechakaa - kwisha kabisa.
 
Siwaelewi watanzania wenzangu
  1. Wakati wa wakoloni walisema bora utawala wa Machifu
  2. Wakati wa Mwl. J. K. Nyerere wakasema bora ukoloni
  3. Wakati wa Mzee Mwinyi walisema bora Mwl. J. K. Nyerere
  4. Wakati wa Mzee Mkapa walimsifu sana Mzee Mwinyi
  5. Wakati wa Kikwete walimsifu sana Mzee Mkapa
  6. Wakati wa Magufuli walimponda na kumkumbuka Kikwete
  7. Kaja Samia sasa wanamkumbuka Magufuli
KUna siku niliona baiskeli ya mkodishaji mmoja imeandikwa "...kila asubuhi mpya heri ya jana, siku kdhaa baadaye nikaona nyingine ya mkodishaji huyohuyo imeandikwa "...every new morning is better than yesterday" nilihisi alilenga kutafsiri ile statement ya kiswahili iliyopo kwenye baiskeli nyingine
I hope kuna mtoto atakuwa kachezea simu yake.
 
Back
Top Bottom