Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwaajili ya propaganda za wakina lisu na mbowe ndio iwe hasara kwa mzazi wake!Haya yote mnayajua baada ya Lisu kutaka Uenyekiti?
Mlimpa Umakamu akiwa wapi?
Ni hasara sana kwa wazazi waliowazaa na kuwasomesheni.
Wanaweweseka na wanajua huenda yule kibaraka wao asishinde uchaguziMimi hicho ndio sielewi. Kwa vile wameona hastahili kuendelea kuwa Mwenyekiti wafanye kampeni ili wapiga kura wasimchague. Haya ya kumtaka apumzike, oh ni ndugu yangu, oh kabila yangu n.k. halina nafasi hapa. Lema hakuwa na haja ya kuweka press conference kutoa taarifa ya kitu ambacho wote tunakijua. Au anaogopa kuwa Mbowe nae atasema " et tu Lema?"
Mimi ningewashauri kuwa pamoja na kumshauri apumzike wangemwambia pia kuwa apumzike katika kuchangia chama kifedha kupita kiasi. Wanachama watakibeba chama chao.
Amandla...
Huna hojaIli uwe Katibu Mkuu sio!
Wewe ni mkimbizi- Canada( Katibu Mkuu)
TAL ni Mkimbizi - Belgium ( Mwenyekiti)
Heche ni Mjaluo wa Kenya ( Makamu Mwenyekiti)
Ndio utakuwa muundo mpya wa chadema🥺😳😳😳😳😳🥺
Anatamani Mbowe apumzike kwa heshima.Wanaweweseka na wanajua huenda yule kibaraka wao asishinde uchaguzi
Wakuu,
Siku ya jana aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA kanda ya Kaskazini kupitia akaunti yake ya X aliahidi kwamba siku ya leo Tarehe 14 January 2024 atakuwa anazungumza na wanahabari.
Wengi wameshuku kuwa huenda Lema atazungumzia kuhusu Uchaguzi wa CHADEMA na kuainisha ni mgombea gani ya Freeman Mbowe au Tundu Lissu anamuunga mkono.
Kaa karibu na Jamii Forums kupata updates zote
======================================================
"Mimi Mbowe ni kaka yangu, tunajuana. Yeye ni Mchaga na mmachame kama mimi, na familia zetu zinafahamiana, ila kwa uchaguzi ujao wa Mwenyekiti namuomba amuachie Tundu Lissu.
- Godbless Lema amesema kuwa anamuunga mkono Tundu Lissu kwenye nafasi ya Uenyekiti CHADEMA na amemuomba Mwenyekiti wa sasa Freeman Mbowe apumzike
Lissu amekuwa Makamu Mwenyekiti, mnadhimu wa Bunge, Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, wanaosema hawezi kuwa Mwenyekiti wanataka nani awe?
Kuna watu wanasema Lissu asiwe Mwenyekiti kwasababu hana pesa, sasa niwaambie katika wakati ambao chama kinapaswa kupata kiongozi asiye na hela ni sasa ili wajumbe wajue kuwa chama hakipaswi kuendeshwa kwa pesa za mtu mmoja bali mobilization kutoka kwa watu. CHADEMA inabidi kitafute namba ya ku-rise fund. Kuna watu waliingia kwenye uongozi bila kuwa na pesa"
- Aidha Godbless Lema amesema kuwa hatogombea Ubunge wa jimbo la Arusha Mjini kwenye Uchaguzi wa mwaka 2025
View: https://www.youtube.com/live/n4jGmCXtOsc?si=QELvyU3Ewhqvx9gA
Tutashtakiwa MIGA.Wanaweweseka na wanajua huenda yule kibaraka wao asishinde uchaguzi
Hadi damu imtoke masikioni ndio ataelewaMwisho wa mwamba hakutakuwa mzr
Aibu gani?Anatamani Mbowe apumzike kwa heshima.
lakini akishupaza shingo ataondoka kwa aibu.
Wamachame wabinafsi sana,hawawapendi hata wachaga wa jamii zingine,pale njia panda machame,barabara ya arusha,kuna maduka ya vibanda ni wamachame tupu,hadi boda,ukienda mchaga wa jamii nyingine unaibiwa vitu vyako vyote,unaweza usiuze hata 100.Machame oyee, Machame safii, Embu mwangalie jirani yako mwambie mimi ni mmachame.
Duuu. Aisee. Hatari mno.Wamachame wabinafsi sana,hawawapendi hata wachaga wa jamii zingine,pale njia panda machame,barabara ya arusha,kuna maduka ya vibanda ni wamachame tupu,hadi boda,ukienda mchaga wa jamii nyingine unaibiwa vitu vyako vyote,unaweza usiuze hata 100.
ukipeleka daladala yako machame to moshi mjini,hupati hata abiria mmoja kama sio mmachame..
Alitabiri kifo cha mungu wenu wa Chato.NABII WA UONGO KATIKA UBORA WAKE
hata akishinda,heshima kwa watu na wanachama haitakuwepo kama zamani,mengi yamesemwa juu yake,kama anabusara,angejitoa tu.Kadiri Mbowe anakavyokuwa mgumu kuachia kabla ya sanduku la kura...
Matamko yanazidi kuwa mengi....kumsihi aachie ngazi kabla ya uchaguzi, fedheha ya kuachia kabla ni ya muda mfupi kuliko la sanduku la kura, atashindwa hata kumshauri Lissu kwenye mambo ya Msingi
Uchaguzi ukiisha yeye na Lisu wanahama Chadema na makelele hayo
Mbowe bigwa walitaka kumpindua akiwa gerezani sasa kawaibukia sanduku.la kura kuwa njooni tupambane sanduku la kura
Wanapiga miyowe kibao wanajua Mbowe anaenda kuwabwaga sanduku la kura