GOOD NEWS: Ni Emmanuel OKWI ndani ya YANGA, asaini Miaka Miwili.

GOOD NEWS: Ni Emmanuel OKWI ndani ya YANGA, asaini Miaka Miwili.

Klabu ya Yanga SC imefanikiwa kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa kimataifa kutoka nhcini Uganda
Emmanuel Arnold Okwi ambaye alikua akiichezea klabu ya SC Villa ya Uganda.

Yanga SC imempata mshambuliaji huyo msumbufu kwa mabeki wengi kwa mkataba wa miaka miwili na
nusu ambapo kwa sasa ataitumika klabu yake mpya ya watoto wa jangwani mpaka mwishoni mwa
msimu wa 2015/2016.

Dirisha dogo la usajili nchini Tanzania limefungwa leo usiku Disemba 15, 2013 saa 6 usiku ambapo
mabingwa wa kihistoria klabu ya Yanga wamekalilisha taratibu zote za usajili ikiwa ni pamoja na kupata hati
ya uhamisho wa kimataifa maarufu kama ITC.

Usajili wa Emmanuel Okwi unaifanya timu ya Yanga kufikisha idadi ya wachezaji watano wa kimataifa
wakiwemo mganda mwenzake Hamis Kiiza, Haruna Niyonzima, Mbuyu Twite na Didier Kavumbagu.

Uongozi wa Yanga unawaomba wanachama, wapenzi na washabiki
kuwapa ushirikiano wachezaji wote wa zamani na wapya waliosajiliwa katika dirisha dogo la usajili.

Wachezaji wengine waliosajiliwa hivi karibuni katika kuimarisha kikosi cha Yanga ni mlinda mlango Juma
Kaseja ambaye alikuwa mchezaji huru na Hassan Dilunga aliyesajiliwa kutoka timu ya Ruvu Shooting.

Baraka Kizuguto Afisa Habari – Young Africans SC
Disemba 15, 2013.

Hivi ukishakuwa na Wachezaji wa nje bado inabaki kuwa timu ya Watanzania?
 
Naomba vyuo vikuu vimpe Bin Kleb shahada ya Heshima (Honoris causa) ya Udaktari wa Falsafa (PhD) katika fitina za Simba na Yanga.
 
Naomba vyuo vikuu vimpe Bin Kleb shahada ya Heshima (Honoris causa) ya Udaktari wa Falsafa (PhD) katika fitina za Simba na Yanga.

Bin Kleb anajua nini cha kufanya ndani ya Yanga. Sio huyu Rage mtoto wa kisomali na ujanja janja wake.
 
Hivi ukishakuwa na Wachezaji wa nje bado inabaki kuwa timu ya Watanzania?
Neymar (Brazil), Messi (Argentina), Daniel Alves (Brazil) ni wa Barcelona ya nchi gani?
Khedira (Ujerumani), Bale ((Wales), C Ronaldo, Pepe (Ureno), Marcelo (Brazil) wanachezea Real Madrid ya wapi?
 
Safari ya Rage imeiva. Sidhani kama wana-Simba watamuachia katika hili. Halafu nasikia pesa za Okwi alitia ndani huyu Msomali. Kudadadeki!
 
Bado tunamuwinda Mbwana Samantha na Thomas Ulimwengu..

ka! ka! ka! ka! ka! ka!

Acha ndoto na emotion! kuna timu tanzania inaweza mlipa mshahara mchezaji zaidi ya dola elfu 10,000 na dola 1, 000 kwa kila goli na mwaka mzima kaisha tia njaa ka goli 30. Samata habari nyingine sana wakina okwi saizi ya timu za tanzania kamwe hutasikia samata kaenda timu za afrika ya kaskazini mpunga mwingi tupwisa mazambe
 
Ata wamsajili nani, wakikutana na Azam chupi juu ya kamba tu.
 
Ata wamsajili nani, wakikutana na Azam chupi juu ya kamba tu.

Azam ni kitu gani tena? Ukitaja Yanga timu pinzani ni Simba tu! Wewe unatuletea madudu gani yanayoitwa Azam? Azam tafuteni mtani wenu kama vile Mbeya City, siyo kujilinganisha na wazee kama Yanga na Simba, umesikia Kitoabu? Acha kabisa kujitia kimbelembele na ka Azam kako inapotajwa Yanga au Simba.
 
Last edited by a moderator:
Si nasikia mwezi ujao mnaanza ujenzi wa uwanja kule Bunju au?
Na wa kaunda nao lin cos mwenyekit mwez wa saba mwakan anaachia ngaz au mil 700 za mzee akilmal wataanzia foundation au feasibility study!
 
Ili kuinua career ya vijana sasa inabidi Yanga kuwaachia wachezaji wao chipukizi kutafuta timu nyingine za kuchezea, otherwise watauwa vipaji, namsikitia sana Bahanuzi sijui bado anafanya nini Yanga!
 
Acheni kudanganyana, Okwi si mchezaji wa Sports Club Villa; Okwi bado ni mchezaji halali wa Etoile du Sahel!
Labda kama mnapenda kufurahishana kishabiki!
 
Acheni kudanganyana, Okwi si mchezaji wa Sports Club Villa; Okwi bado ni mchezaji halali wa Etoile du Sahel!
Labda kama mnapenda kufurahishana kishabiki!
Wanaodanganya ni FIFA waliyomruhusu kuchezea Villa, wakIfuatiwa na FUFA iliyotoa ITC, kisha ni wewe unayeongea kishabiki.
 
Klabu ya Yanga SC imefanikiwa kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa kimataifa kutoka nhcini Uganda
Emmanuel Arnold Okwi ambaye alikua akiichezea klabu ya SC Villa ya Uganda.

Yanga SC imempata mshambuliaji huyo msumbufu kwa mabeki wengi kwa mkataba wa miaka miwili na
nusu ambapo kwa sasa ataitumika klabu yake mpya ya watoto wa jangwani mpaka mwishoni mwa
msimu wa 2015/2016.

Dirisha dogo la usajili nchini Tanzania limefungwa leo usiku Disemba 15, 2013 saa 6 usiku ambapo
mabingwa wa kihistoria klabu ya Yanga wamekalilisha taratibu zote za usajili ikiwa ni pamoja na kupata hati
ya uhamisho wa kimataifa maarufu kama ITC.

Usajili wa Emmanuel Okwi unaifanya timu ya Yanga kufikisha idadi ya wachezaji watano wa kimataifa
wakiwemo mganda mwenzake Hamis Kiiza, Haruna Niyonzima, Mbuyu Twite na Didier Kavumbagu.

Uongozi wa Yanga unawaomba wanachama, wapenzi na washabiki
kuwapa ushirikiano wachezaji wote wa zamani na wapya waliosajiliwa katika dirisha dogo la usajili.

Wachezaji wengine waliosajiliwa hivi karibuni katika kuimarisha kikosi cha Yanga ni mlinda mlango Juma
Kaseja ambaye alikuwa mchezaji huru na Hassan Dilunga aliyesajiliwa kutoka timu ya Ruvu Shooting.

Baraka Kizuguto Afisa Habari ? Young Africans SC
Disemba 15, 2013.

watatukoma hawo
 
Azam ni kitu gani tena? Ukitaja Yanga timu pinzani ni Simba tu! Wewe unatuletea madudu gani yanayoitwa Azam? Azam tafuteni mtani wenu kama vile Mbeya City, siyo kujilinganisha na wazee kama Yanga na Simba, umesikia Kitoabu? Acha kabisa kujitia kimbelembele na ka Azam kako inapotajwa Yanga au Simba.

Makoye Matale,

Acha kuwavunjia heshima akina MWANAFYALE (Mbeya City), mtani wa Azam ni Miembeni, KMKM, Makunduchi hao ndo anaweza kuvuana nao upapi
 
Ivi uyu bin kleb ndo nani hapa mjini anatunyima raha?, iki kiburi anakitoa wapi?, mh. Rage umeonyesha udhaifu mkubwa sana kushindwa kupambana na uyu kijana anaejifunza fitna za mpira wa bongo.

Usione vyaelea, vimeundwa.
 
Back
Top Bottom