Google yapigwa faini ya Tsh. 56,076,872,348,484,000,000,000,000,000,000,000,000,000 na Urusi, ni kiasi cha fedha ambacho hakipo duniani

Haahaa!

Dawa ni Google kujiondoa Russia basi
Putin alisema atatunga sheria ngumu sana ili iwe vigumu kwa makampuni ya nje kuondoka Urusi.

Tangu vita yake na Ukraine makampuni ya west na Ulaya mengi yalifunga shughuli na kufunga ofisi na kuondoka.

Alisema atatunga sheria ya kutaifisha mali zao na kuhakikisha hawaondoki bila kuacha mzigo mkubwa, hadi waone ni bora kuendelea kufanya biashara kuliko kufunga virago.

Sasa anatekeleza.
 
In fact huo mzigo wa noti zikichapwa zote dunia itayumba kwenye orbit yake maana haitaweza kuubeba! Wote hatutakuwa salama. Tutajipeleka peponi wote at par!
Nadhani ili orbit isielemewe, itabidi huo mzigo uwekwe bank tofauti tofauti duniani, Tanzania hapa CRDB wataramba mzigo kiasi fulani, mzigo mwingine utatupiwa Brazil, Africa Kusini, Japan, Korea ya kaskani na hata Marekani kwenyewe; hivo yaani
 
Hicho ni kicha cha jumla. Ni KICHAA SHIRIKISHI. Wote nchi nzima mnakuwa mmekuwa vichaa at once. Hapo ni Mahakama ilifungua mdomo wakatamka hayo. Sijui amgeulizwa Rais Putin angeweweseka jambo gani kuhusu Ukraine. Tunashukuru Mungu kichaa shirikishi hutokea only once in global life time.
 
Hizo Hela zimenishinda Hadi kuzisoma asee. Nimemuonyesha mkali wa mathe kasema hiyo Hela haipo na haitakuja kuwepo duniani
URUSI: Mahakama imeitaka kampuni ya Google kuvilipa Vyombo vya Habari vya Serikali faini ya Dola za Marekani takriban Desilioni 20 (takriban Tsh. Undesilioni 56) kiasi ambacho inadaiwa hakipo duniani na faini hiyo inaongezeka kila siku

Uamuzi huo unatokana na kesi ya miaka minne Mahakamani iliyoanza baada ya YouTube kuifungia Chaneli ya Urusi ya Tsargrad mwaka wa 2020 na baadaye kufuatiwa na vikwazo vya Marekani dhidi ya Urusi kutokana na kuivamia Ukraine mwaka 2022 ambapo Chaneli 17 nyingine za Habari zilifungwa na zikatangaza kuishtaki Google

Kwa mujibu wa takwimu za Benki ya Dunia (WB), faini hiyo inazidi Pato la Dunia nzima ambalo linakadiriwa kuwa Dola Trilioni 100, hivyo kama Google yenye thamani ya Dola Bilioni 88 (Tsh. Trilioni 239.49) itaamua kulipa faini hiyo itabidi itafute Fedha zaidi ambazo dunia haina

Soma Google yapigwa faini ya Tsh. 56,076,872,348,484,000,000,000,000,000,000,000,000,000 na Urusi, ni kiasi cha fedha ambacho hakipo duniani
 
Sanctions ambazo Urusi inawabandika hao ni kali mno. Marekani kamwaga mboga, wao wameondoka na ugali.
Hicho ni kituko tu na kisa ni youtube wamefungia account za Warusi wenye mlengo wa kutetea propaganda za Urusi, since Youtube ni US wakafungia hizo channel jamaa wakafungua kesi nchini kwao ndo mahakama ya Urusi imewapiga fine Youtube.. kiasi cha pesa ambaco kinazidi GPA ya dunia nzima.

Sasa si wazimu huo. Wanajua kuwa youtube hatalipa kitachofatia youtube ajitoe Urusi au Urusi iban Youtube itengeneze youtube yake kama china
 
Haipigwi ban ilipe fidia kama ban ijipige yenyewe
 
Pepari linapolazimisha kuungwa mkono hata linapokosea. Na hiyo kajifuraisha tu hakuna mlipaji. Kwahiyo alipovamia Ukraine alitaka apigiwe makofi na kila binadamu? Na vyombo vya habari visapoti kuwa anafanya vizuri. Hahahahahaaa halipwi hata mia kinachofuata watajitoa Russia kwisha.
 
Au nimeelewa vibaya??
Kweli mleta mada upo sahihi! Ulichokosea ni namna ya uwasilishaji!

Russia fines Google more than world's entire GDP for blocking YouTube accounts​


Russia fines Google more money than there is in entire world​


 

Mahakama ya urusi imempiga fine kampuni ya Google kulipa pesa nyingi sana Zenye sifuri 36 kwa kosa la kuzuia vyombo mbalimbali vya habari vya nchini Russia kurusha matangazo kwenye YouTube channel.

Pesa hizo kwa thamani ya dollar ni $20,000,000,000,000,000,000,000,000,000,000,000 Licha ya Google kutambulika kuwa ni Moja ya kampuni tajiri lakini Thamani ya pesa hizo ni zaidi ya dola trilioni 2 za thamani ya Google.

Kwa kweli ni pesa nyingi sana ni kubwa zaidi kuliko jumla ya Pato la taifa la Dunia ambalo linakadiliwa na shirika la fedha kuwa na thamani dollar $110 trilioni.



Chombo cha habari nchini Russia RBC kimeripoti faini hiyo inahusiana na kizuizi cha maudhui ya vituo 17 vya habari vya kirusi kwenye YouTube.

Msemaji wa Kremlin Dmitry Peskov amesema "hawezi hata kutamka nambari hii zilizopo kwenye hiyo fine" lakini aliwahimiza wasimamizi wa Google kuzingatia.

Kampuni ya Google Bado haijatoa maoni yoyote hadharani hivyo watu wengi wanasubiri kusikia Google watasema Nini kuhusu hii tuhuma.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…