Great thinkers wa JF, tuache kujadili viongozi/uongozi badala yake tujadili mstakabali wa taifa letu!

Great thinkers wa JF, tuache kujadili viongozi/uongozi badala yake tujadili mstakabali wa taifa letu!

Lanlady

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2019
Posts
1,836
Reaction score
6,303
Huu ni ushauri wangu kwa wana JF wote ambao wamekuwa wakijadili zaidi watu (viongozi wa kisiasa) zaidi kuliko mambo yanayohusu taifa.

Ukweli ni kwamba, kwa sasa taifa letu limegawanyika kiitikadi/ufuasi pengine kuliko wakati mwingine wowote.

Hii inatokana na kuwepo makundi ya wanaojadili utawala wa kiongozi aliyepo madaraka kwa sasa na yule aliyefariki akiwa bado madarakani.

Hii ndio hasa tofauti kati ya siasa za hapo kabla na hizi za sasa. Kwani, kwa sasa ni vigumu kupata mrejesho toka kwa mmojawao ambaye hayuko tena duniani.

Awamu zilizopita ilikuwa ni rahisi kupata mrejesho hata kwa kuwahoji wahusika. Na ndio maana wengine wametumia fursa ya kuwa kwao hai kwa kuandika vitabu vya historia zao.

Wanajf, hebu tujikite zaidi katika kujadili maendeleo ya taifa letu kisiasa, kiuchumi na hata kijamii.

Madhaifu ya viongozi waliopita yatusaidie kujifunza na kutafuta mbinu za kukabiliana nayo.

Aidha, tusione shaka kuwashauri viongozi waliopo madarakani kwa sasa. Badala ya kuwakosoa au kuwalinganisha na waliopita, tujitahidi kutoa maoni ya namna bora ya kuboresha maslahi ya taifa.

Kuendelea kulumbana kwa kuwapambanisha viongozi waliopo na wasiokuwepo madarakani, haitasaidia kustawisha taifa; na badala yake kutazidi kuligawa taifa!

Mwenyezi Mungu aibariki na kuistawisha Tanzania!
 
Wapo walioasisi hii mambo, kama Taifa hatukuwahi kua na huu utamaduni wa kuombeana mabaya, mtu wa upande flan akifa au akidhurika wengine wanashangilia!! Kama Taifa tulijengwa kweny misingi ya upendo na kushirikiana. Hao walioasisi hii kitu ndio wa kulaumiwa sasa!!
 
Huwezi kutenganisha mwelekeo wa taifa na kiongozi, uwezo wa kiongozi utadetermine kasi ya maendeleo kwa taifa.

Tuache tu tuwajadili maana ndani ya huo mjadala tutajua tunaenda mbele au tunarudi nyuma kimaendeleo.
 
acha tu wajadiliwe mkuu wangu, kujadiliwa kwao hakuzuii mijadala mingine kuhusu mustakabali wa taifa hili, acha wajadiliwe ili km atatokea mwngne basi aje na staili nyngne ambayo hatuifaham naye akiondoka atajadiliwa vilevile
 
Suala hili halikwepeki, maadamu mtu fulani amefikia kiwango cha juu cha uongozi wa nchi pamoja na mihimili yote ya dola iliyogusa kila kona ya maisha ya raia waliopo ndani ya mipaka ya nchi na nje pia basi legacy yake itajadiliwa na kama ilivyo ada binadamu ana mazuri pia mapungufu hivyo katika mijadala yote, haya mapungufu na weledi yatajitokeza ili tuzidi kujifunza .
 
TOKA MAKTABA:

4 November 2016

Uzuri ni kuwa John Pombe Joseph Magufuli aliwahi kukumbana na maswali kuhusu mwenendo wa serikali yake

Majibu ya Rais Magufuli kwa wanaomsema ni Dikteta: asema critic ni kawaida na pongezi ni kawaida





Mwaka 2016 akijibu maswali toka kwa waandishi wa vyombo tajwa vya habari, Mh. Rais John Magufuli asisitiza kila mmoja ana uhuru wa kufikiria, sasa sisi ni kina nani tujifunge kujadili legacy za Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete, Magufuli na sasa ya Mh. Samia Suluhu Hassan.
 
Huu ni ushauri wangu kwa wana JF wote ambao wamekuwa wakijadili zaidi watu (viongozi wa kisiasa) zaidi kuliko mambo yanayohusu taifa.

Ukweli ni kwamba, kwa sasa taifa letu limegawanyika kiitikadi/ufuasi pengine kuliko wakati mwingine wowote.

Hii inatokana na kuwepo makundi ya wanaojadili utawala wa kiongozi aliyepo madaraka kwa sasa na yule aliyefariki akiwa bado madarakani.

Hii ndio hasa tofauti kati ya siasa za hapo kabla na hizi za sasa. Kwani, kwa sasa ni vigumu kupata mrejesho toka kwa mmojawao ambaye hayuko tena duniani.

Awamu zilizopita ilikuwa ni rahisi kupata mrejesho hata kwa kuwahoji wahusika. Na ndio maana wengine wametumia fursa ya kuwa kwao hai kwa kuandika vitabu vya historia zao.

Wanajf, hebu tujikite zaidi katika kujadili maendeleo ya taifa letu kisiasa, kiuchumi na hata kijamii.

Madhaifu ya viongozi waliopita yatusaidie kujifunza na kutafuta mbinu za kukabiliana nayo.

Aidha, tusione shaka kuwashauri viongozi waliopo madarakani kwa sasa. Badala ya kuwakosoa au kuwalinganisha na waliopita, tujitahidi kutoa maoni ya namna bora ya kuboresha maslahi ya taifa.

Kuendelea kulumbana kwa kuwapambanisha viongozi waliopo na wasiokuwepo madarakani, haitasaidia kustawisha taifa; na badala yake kutazidi kuligawa taifa!

Mwenyezi Mungu aibariki na kuistawisha Tanzania!


Naunga mkono hoja
Tuwe na mijadala yenye suluhu badala ya malalamiko kwa mambo tunayojadili.
 
Huwezi kutenganisha mwelekeo wa taifa na kiongozi, uwezo wa kiongozi utadetermine kasi ya maendeleo kwa taifa.

Tuache tu tuwajadili maana ndani ya huo mjadala tutajua tunaenda mbele au tunarudi nyuma kimaendeleo.
Ni kweli huwezi kumtenganisha mtu na matendo yake.
Lakini jambo la muhimu ni kutoa ushauri wa nini kifanyike kutokana na matendo fulani yasiyofaa.
Hakuna binadamu asiye na mapungufu katika kutenda au kufanya maamuzi.

Ushauri wangu ni kujitahidi zaidi kujadili mstakabali wa taifa kwa sasa badala ya kuwapambanisha/kuwalinganisha viongozi.

Kuwalinganisha viongozi waliopo na waliopita; ni sawa na mtu kupata mke mwingine halafu kila wakati badala ya kumkosoa/kumrekebisha, yeye anamlinganisha matendo yake na yule asiyekuwepo! Haitasaidia! Badala yake inaweza kutengeneza chuki na uhasama zaidi!
 
Huwezi kutenganisha mwelekeo wa taifa na kiongozi, uwezo wa kiongozi utadetermine kasi ya maendeleo kwa taifa.

Tuache tu tuwajadili maana ndani ya huo mjadala tutajua tunaenda mbele au tunarudi nyuma kimaendeleo.
Ni kweli huwezi kumtenganisha mtu na matendo yake.
Lakini jambo la muhimu ni kutoa ushauri wa nini kifanyike kutokana na matendo fulani yasiyofaa.
Hakuna binadamu asiye na mapungufu katika kutenda au kufanya maamuzi.

Ushauri wangu ni kujitahidi zaidi kujadili mstakabali wa taifa kwa sasa badala ya kuwapambanisha/kuwalinganisha viongozi.

Kuwalinganisha viongozi waliopo na waliopita; ni sawa na mtu kupata mke mwingine halafu kila wakati badala ya kumkosoa/kumrekebisha, yeye anamlinganisha matendo yake na yule asiyekuwepo! Haitasaidia! Badala yake inaweza kutengeneza chuki na uhasama zaidi!
 
Hiyo haikubaliki. Uongozi ni historia na historia ni funzo kwa wakati tuliopo na ujao. Magufuli lazima ajadiliwe. Kama hamkutaka ajadiliwe kwa nini alitaka uongozi. Mnafanya mwendelezo wa udikteta,alikataza tusimjadili kwa mkono wa chuma.
 
Good!

Kama nimekuelewa vizuri maana yake ni kwamba yaliyopita si ndwele tugange yajayo?.

Basi kama ni hivyo tupate dira ya taifa itakayomtofautisha kiongozi na matendo yake maana atafuata maelekezo ya dira tofauti na sasa kiongozi akiingia madarakani anafuata yaliyomo kichwani mwake.

Nje ya mada huoni hata viongozi wanachochea huu mjadala? Mfano alichokifanya Samia akiwa marekani.
Ni kweli huwezi kumtenganisha mtu na matendo yake.
Lakini jambo la muhimu ni kutoa ushauri wa nini kifanyike kutokana na matendo fulani yasiyofaa.
Hakuna binadamu asiye na mapungufu katika kutenda au kufanya maamuzi.

Ushauri wangu ni kujitahidi zaidi kujadili mstakabali wa taifa kwa sasa badala ya kuwapambanisha/kuwalinganisha viongozi.

Kuwalinganisha viongozi waliopo na waliopita; ni sawa na mtu kupata mke mwingine halafu kila wakati badala ya kumkosoa/kumrekebisha, yeye anamlinganisha matendo yake na yule asiyekuwepo! Haitasaidia! Badala yake inaweza kutengeneza chuki na uhasama zaidi!
 
Haitawezekana! Sisi wengine tunataka kuingia magogoni mle ndani,Taifa tutalikuta huko mbelee..
 
Huwezi kutenganisha mwelekeo wa taifa na kiongozi, uwezo wa kiongozi utadetermine kasi ya maendeleo kwa taifa.

Tuache tu tuwajadili maana ndani ya huo mjadala tutajua tunaenda mbele au tunarudi nyuma kimaendeleo.
.
 
JF nasi tuna nafasi katika jamii yetu kujadili viongozi wetu, tusiwaachie vijana wenzetu wa buku saba pale mtaa wa Lumumba au wanasiasa na washiriki wa makongamano wanaopewa bahasha za kaki kuwa ndiyo wenye hati miliki ya kuchunguza legacy za viongozi.


TOKA MAKTABA:
30 Juni 2021

SIKU 100 ZA MAMA SAMIA, PROF. LIPUMBA AIBUA MAMBO HAYA MAZITO LEO / KATIBA MPYA BADO NI UGONJWA MKUBWA

 
Huu ni ushauri wangu kwa wana JF wote ambao wamekuwa wakijadili zaidi watu (viongozi wa kisiasa) zaidi kuliko mambo yanayohusu taifa.

Ukweli ni kwamba, kwa sasa taifa letu limegawanyika kiitikadi/ufuasi pengine kuliko wakati mwingine wowote.

Hii inatokana na kuwepo makundi ya wanaojadili utawala wa kiongozi aliyepo madaraka kwa sasa na yule aliyefariki akiwa bado madarakani.

Hii ndio hasa tofauti kati ya siasa za hapo kabla na hizi za sasa. Kwani, kwa sasa ni vigumu kupata mrejesho toka kwa mmojawao ambaye hayuko tena duniani.

Awamu zilizopita ilikuwa ni rahisi kupata mrejesho hata kwa kuwahoji wahusika. Na ndio maana wengine wametumia fursa ya kuwa kwao hai kwa kuandika vitabu vya historia zao.

Wanajf, hebu tujikite zaidi katika kujadili maendeleo ya taifa letu kisiasa, kiuchumi na hata kijamii.

Madhaifu ya viongozi waliopita yatusaidie kujifunza na kutafuta mbinu za kukabiliana nayo.

Aidha, tusione shaka kuwashauri viongozi waliopo madarakani kwa sasa. Badala ya kuwakosoa au kuwalinganisha na waliopita, tujitahidi kutoa maoni ya namna bora ya kuboresha maslahi ya taifa.

Kuendelea kulumbana kwa kuwapambanisha viongozi waliopo na wasiokuwepo madarakani, haitasaidia kustawisha taifa; na badala yake kutazidi kuligawa taifa!

Mwenyezi Mungu aibariki na kuistawisha Tanzania!

Tunaachaje kujadili viongozi wakati wao ndio wanaamua mustakabali wa taifa letu? Ni katika platform gani wananchi tunakutana na kujadili mustakabali wa nchi yetu? Kinachofanyika ni kikundi kidogo cha rais na genge lake wanaamua kama taifa tuende vipi.
 
Good!

Kama nimekuelewa vizuri maana yake ni kwamba yaliyopita si ndwele tugange yajayo?.

Basi kama ni hivyo tupate dira ya taifa itakayomtofautisha kiongozi na matendo yake maana atafuata maelekezo ya dira tofauti na sasa kiongozi akiingia madarakani anafuata yaliyomo kichwani mwake.

Nje ya mada huoni hata viongozi wanachochea huu mjadala? Mfano alichokifanya Samia akiwa marekani.
Tatizo ni kwamba, baadhi ya watu hutumia madhaifu ya watu wengine ili wao waonekane bora. Jambo ambalo si sawa. Kinachotakiwa kufanyika ni kila mtu kutenda kwa nafasi na uweezo wake ili aonekane bora.

Isitoshe, mi huwa nafananisha uongozi sawa na maandalizi ya chakula jikoni. Kinapofika mezani kwa walaji, wapishi wote wanapaswa kupokea sifa au lawama za uzuri au ubaya wa chakula hicho. Kumtupia lawama mtu mmoja ilihali wote mlikuwa jikoni, si sawa.
Inaonesha udhaifu mahali. Kiongozi bora anapaswa kusimamia maono yake pasipo kujali wangapi watamuunga mkono hata kama wako juu yake.
Kusema aliyeweka chumvi nyingi alikataa ushauri, kunaonesha udhaifu!

Na kwa taifa, kama tatizo ni katiba, basi ibadilishwe! Ama sivyo tutaendelea kulaumiana na kukosoana kila kukicha kwa kuwa kila mmoja hutenda kwa matakwa yake!
 
Back
Top Bottom