Great thinkers wa JF, tuache kujadili viongozi/uongozi badala yake tujadili mstakabali wa taifa letu!

Great thinkers wa JF, tuache kujadili viongozi/uongozi badala yake tujadili mstakabali wa taifa letu!

Kumtupia lawama mtu mmoja ilihali wote mlikuwa jikoni, si sawa.

Ikiwa pesa ni za Rais, Miundo mbinu ni ya Rais, Haki ya kufanya Demokrasia ni hisani ya Rais, Hospitali kajenga Rais ....

Kutokana na hayo lazima rais ataangaziwa sana kuhusu uhusika wake katika maisha ya mtanzania kisiasa, kiuchumi na kijamii kwani amepaishwa kuwa mithili ya Mungu

Toka Maktaba :

Mkapa adai mazungumzo mapana toka kwa wananchi, raia wajadili kwa kina na washirikishwe ktk kila ngazi, wasiachwe nje ya maamuzi ...

 
Hii issue yako ngumu sana kutekelezeka, tatizo halianzii hapo ulipodhani lipo, tatizo linaanzia juu kule.

Pale ambapo kiongozi aliyepo madarakani sasa anapomjadili mtangulizi wake, iwe kwa mema au kwa mabaya yake.

Kumjadili huko husababishwa na mambo kadhaa, mfano miradi aliyoachiwa na mtangulizi wake anayoendeleza utekelezaji wake, au tabia binafsi za kiutendaji alizokuwa nazo mtangulizi wake.

Kwa kifupi hili jambo uliloleta halitekelezeki, kwasababu viongozi ndio wanabeba muelekeo wa taswira ya nchi, mfano kama nchi ikielekea pabaya kutokana na kukiukwa sheria, basi lazima huyo mkiukaji atajwe, kumficha ni sawa na kuendelea kulea tatizo.
 
Mtekelezaji wa mijadala ya maendeleo ya nchi yetu ni nani? Ni kiongozi namba moja wa nchi! kama hawezi kwa nn tusimjadili?
 
Wakati Mungu anataka kuwatoa Wana wa Israel kutoka utumwani (Misri) alilazimika kuandaa kiongozi aitwae Musa.

Musa alipoishia njiani, Joshua alichukua kijiti na kuwafikisha watu wale nchi ya ahadi.

Tanzania ilibahatika kupata kiongozi wa kwanza JKN ambae sio tu alipigania uhuru wa nchi hii, bali alituunganisha kuwa taifa z nchi yanye makabila zaidi ya 120.
Akaja na JKT kuwaunganisha Watanzania.

Shule za sekondari zilichukua watu across the country.

Ili tupate mustakabali bora wa kesho yetu Watanzania, lazima tuwe na kiongozi madhibuti, mwenye maono anaeweza kujenga taasisi ambazo zitasimamiwa na watu (viongozi) ili kufikia matarajio yetu.

Hivyo, lazima tumguse Mkulu wa sasa kuona kama anachokifanya, kina akisi matarajio yetu kuifikia Tanzania tunayoitaka.

Leo tunalia kukosa uhakika wa mafuta ya kula na kupanda kwa bei za bidhaa kama ngano.
Moja ya nchi inayouza ngano na robo ya mafuta ya alizeti duniani ni Ukraine.
Ukraine ni theluthi mbili ya size ya Tanganyika.

Wamekuwa na aina gani ya uongozi wa nchi na kisekta kwenye kilimo-biashara, ili kukumata soko la mauzo ya mafuta ya alizeti duniani.

Kuna msemo unasema 'Proper leadership and management are key factors for a country to take off'

Je tuna aina ya uongozi na viongozi kwenye taifa na sekta chungu mzima ambao wakionesha uongozi na management sahihi, kuwafanya Watanzania wajione wana mchango kwenye kukuza uchumi wao binafsi na kutokuendelea kutembeza 'bakuli' duniani?

Happy Easter Monday!

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Kuna watu wanadai nchi ni yao na chama ni chao hii kauli inatusumbua sana wengine inapaswa walioitamka waifute.

Hii nchi ni ya kila mtanzania wala si mali ya mtu na familia yake na hakuna chama kilichosajiliwa kwa jina la mtu binafsi wala familia ya mtu.
 
Huu ni ushauri wangu kwa wana JF wote ambao wamekuwa wakijadili zaidi watu (viongozi wa kisiasa) zaidi kuliko mambo yanayohusu taifa.

Ukweli ni kwamba, kwa sasa taifa letu limegawanyika kiitikadi/ufuasi pengine kuliko wakati mwingine wowote.

Hii inatokana na kuwepo makundi ya wanaojadili utawala wa kiongozi aliyepo madaraka kwa sasa na yule aliyefariki akiwa bado madarakani.

Hii ndio hasa tofauti kati ya siasa za hapo kabla na hizi za sasa. Kwani, kwa sasa ni vigumu kupata mrejesho toka kwa mmojawao ambaye hayuko tena duniani.

Awamu zilizopita ilikuwa ni rahisi kupata mrejesho hata kwa kuwahoji wahusika. Na ndio maana wengine wametumia fursa ya kuwa kwao hai kwa kuandika vitabu vya historia zao.

Wanajf, hebu tujikite zaidi katika kujadili maendeleo ya taifa letu kisiasa, kiuchumi na hata kijamii.

Madhaifu ya viongozi waliopita yatusaidie kujifunza na kutafuta mbinu za kukabiliana nayo.

Aidha, tusione shaka kuwashauri viongozi waliopo madarakani kwa sasa. Badala ya kuwakosoa au kuwalinganisha na waliopita, tujitahidi kutoa maoni ya namna bora ya kuboresha maslahi ya taifa.

Kuendelea kulumbana kwa kuwapambanisha viongozi waliopo na wasiokuwepo madarakani, haitasaidia kustawisha taifa; na badala yake kutazidi kuligawa taifa!

Mwenyezi Mungu aibariki na kuistawisha Tanzania!
Lanlady nakubaliana na hoja yako ambayo ni ya msingi sana!

Mfano baada ya ripoti ya CAG watu tumejikita kubishana ni awamu ipi imesabibisha ufisadi uliotajwa badala ya kujumuisha nguvu pamoja na kuonesha hasira zetu juu ya huo ufisadi na madhara yake kiuchumi, kijamii na kwa maendeleo ya taifa kwa ujumla.

Watu wanatoa visa fake, wanachana noti, kwenye halimashauri hakuna usimamizi etc sisi tunabaki kubishania awamu kiasi kwamba ufisadi utapita hivi hivi. Ifike mahali tupaze sauti hatua sahihi zichukuliwe kwa manufaa ya taifa letu vinginevyo majambazi yanaendelea kushangilia.
 
Humu wengi wapambe wa viongozi wana posho kabisa hawaandiki tu kwa kujitakia
 
Kiongozi lazima ajadiliwe, maana nchi haitaenda popote kama ina kiongozi wa ngekewa........kiongozi lazima achaguiwe kwa kura za wananchi, katiba mpya ni sasa.......
 
Mstakhabali wenyewe wa taifa letu si ndio huo wa kuwajadili viongozi na uongozi wao kitaifa kwa mapana? hatuwezi kujadili vitu tukaacha watu.
 
Back
Top Bottom