Gwajima: Siwezi kujitetea kwa mahubiri yanayotoka kwa Roho Mtakatifu

Gwajima: Siwezi kujitetea kwa mahubiri yanayotoka kwa Roho Mtakatifu

DUH,INABIDI SASA HIYO KAMATI NAO WAKIONGEA NA GWAJIBOY,WAONGE NAYE
KI ROHO MTAKATIFU

ova
 
Huwezi kuyafanya mahubiri ya kanisani kama kichaka cha upotoshaji na wakati mhubiri mwenyewe wakati fulani ndiye pia alikuwa muumini wa kauli hii inayotumiwa mara nyingi na wanasiasa hata out of context: 'Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu' (Warumi 13:1)
Kama Mbowe na ugaidi wake halafu anajifuchia kwenye kichaka cha katiba mpya,mjinga sana ,safari hii kanasa kiulaini sana
 


"Niliitwa na Kamati ya Maadili ya Bunge wiki iliyopita nilipotoka wengi mliniuliza kimejiri nini na nikasema sitosema hadi Kamati iseme kwanza na kwasababu Kamati imeshaongea acha nami nizungumze”

“Sababu ya kuongea ni kwasababu wameniongelea kama Mtu mbaya sana, Jitu baya sana ambalo kama lipo kama lilivyotajwa basi halitakiwi hata kuwa Kiongozi wa Kanisa”

“Mimi Mchungaji wa muda mrefu sana hapa tu Ubungo nipo kwa miaka 25, nilipoitwa kwenye Kamati yale niliyoitiwa ni kuhusu mahubiri ya Kanisani, Mimi nikawaambia sidhani kama Kamati mmefanya vizuri maana yote nimeongea Kanisani na hakuna mwenye Mamlaka ya kuuliza maswali juu ya Ibada ya Kanisani na imani za Watu na nikasema kwenye hili Kamati mmekosea”

“Niliwaambia Kamati mmesema mmesikia nimewaambia Watu wasichanjwe nikasema hiyo haibadiliki milele, nikaweka wazi kwamba sisi Ufufuo na Uzima chanjo ni hiari na sisi tumechagua hatuchanji sikupindisha nilisema hatutowaruhusu Waumini kuchanja na sababu zetu ni hatujapata taarifa za kutosha juu ya madhara ya chanjo ya muda mfupi, siku zijazo na siku nyingi”

“Kwahiyo kama nimeitwa mkorofi ukorofi wangu ni huo na kama huo ndio ukorofi basi ni ukorofi kwelikweli kwenye eneo hilo, wakaniambia jitetee nikasema sina la kujitetea, siwezi kujitetea kwa mahubiri niliyohubiri yanatoka kwa roho mtakatifu, nimefafanua ili mjue Gwajima sio mkorofi ”———-Askofu Gwajima

My Take
Bunge hapa lilichemka. Labda lingempiga pini kwenye chama

Taratibu sasa naanza kuona hata wale mnaokuja na hizi Taarifa za Tapeli wa Kiroho na Kiimani nanyi pia huenda mkawa na Mapepo kama aliyonayo na kwa pamoja mnahitaji Maombi makubwa sana ili mponyeke na msiishie kuwa Wendawazimu.
 
Kama Mbowe na ugaidi wake halafu anajifuchia kwenye kichaka cha katiba mpya,mjinga sana ,safari hii kanasa kiulaini sana
Unapomtaja mtu kwa jina unamshambulia personally. Tujifunze uwasilishaji mzuri usioharibu taswira ya mtu machoni pa jamii. Haya uliyoyataka hapa siku nyingine yanaweza kukupata wewe. Hivyo, usidhani wewe ni salama.
 
Unapomtaja mtu kwa jina unamshambulia personally. Tujifunze uwasilishaji mzuri usioharibu taswira ya mtu machoni pa jamii. Haya uliyoyataka hapa siku nyingine yanaweza kukupata wewe. Hivyo, usidhani wewe ni salama.
Mngetumia ustarabu huu kwa Sabaya ingependeza sana
 
Kuna marehemu alipelekwa hapo kwake kwa siku nne Gwajima ana mfanya vitu vyake tapeli huyu.
Hadi marehemu kaanza kunuka.

Lini mtashituka ninyi kizazi kilicholaaniwa!
Maada iliopo hapa ni kuhusu chanjo sio kwenda kusal kanisan kwake ... Labda waweke wazi kwamba ile hiari ya kuchanja ina ukomo usimwambie mwingine asichanje au sio bwana
 
Mamlaka ndio iliyosema chanjo ni hiari mtu atake kuchanjwa ama la. Kwa ujinga wako unadhani anae kataa anapingana na mamlaka kitu ambacho sio sahii.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Mamlaka pia ndiyo imemwita kwenye kamati kumhoji na akikataa kuhojiwa na kamati na je anakuwa ametii mamlaka?
 
Ccm Sasa huenda wataagiza polisi kuzuia ibada za gwajima Mana ndo tiketi wamebaki mayo Kama sio kumfukuza chama. Hoja jamani ndo tunataka co mabavu nyie wenyewe mmesema chanjo ni hiari Sasa tatizo lenu nni. Ameeleza ukweli kuwa makanisa mengne hutoa nyaraka Ila yeye kaamua kwenda na mahubiri Safi Sana gwajima. Katika nyakati hzi ambazo wanaume halisi na madhibuti wantoweka kwa Kasi gwajima ni wa kupongezwa. Bravo.
 
chanjo zimewadodea ...tupo watu mil 60 waliochanja chini ya laki 4...kuna watu hpa walikuwa wanapiga promo ya chanjo hata wao pia wamegoma kuchanja safi sn

huu uroho wa kuchukua pesa za watu bila kujali usalama wa afya za watu matokeo yake ndio haya ...ni aibu sana kwa mara ya kwanza wananchi wameshinda dhidi ya utapeli
 
Hiyo kamati na wale waliochangia wanalo, wapakwa mafuta si wakuchezea. Asiyefahamu atabeza, tunaofahamu tunaangalia tu
 
Wanafunzi wa Yesu walipo itwa na mamlaka za kidunia na za Kiroho za enzi zao walijitetea kwa kuwahubiria washitaki wao Neno la Mungu la kumkiri Bwana Yesu Mfufuka kwa ujasiri wa hali ya juu na kustaajabisha hasa. Gwajima siku nyengine akiitwa ashuke mistari ya Neno la Mungu inayokaripia rushwa na jinsi viongozi wanavyotakiwa kuwa mfano wa kuwatumikia wananchi kwa uaminifu wote.
 
Kweli yanatoka kwa roho mtakatifu? Huyo roho anaekutuma kuwa unafufua wafu ni nani? Unazidi kunichanganya na maujanja yako. Anyway! Life is a game.
 
Maada iliopo hapa ni kuhusu chanjo sio kwenda kusal kanisan kwake ... Labda waweke wazi kwamba ile hiari ya kuchanja ina ukomo usimwambie mwingine asichanje au sio bwana
Mtu akiwa MUONGO yaani habitual liar, mtu mwenye akili timamu hawezi kuamini chochote anachosema.
Na mtu anaongea uongo ulio wazi kwa sababu maalum-kutapeli watu.
 
Huwezi tii Malamka ya Shetani au yenye mambo ya Kishetani. Usitumie neno vibaya
Hujasoma ukanielewa. Nimesema kuna wakati na yeye alikuwa muumini wa hiyo phrase ya mamlaka dhidi ya viongozi wenzake wa dini waliokuwa wakiikosoa serikali kuhusu demokrasia kipindi cha awamu ya 5. Ndiyo maana nikasema hii phrase inatumiwa vibaya na wanasiasa (out of context) kuhalalisha mambo wanayoyataka, lakini siyo fasili sahihi ya Biblia. Andiko la mamlaka kwenye Biblia halina maana mamlaka yoyote, bali 'mamlaka hahali' au 'mamlaka inayotenda haki' au inayowaunganisha watu au inayotimiza wajibu wake wa uongozi wa nchi kwa masilahi ya wote na siyo kwa masilahi ya kikundi fulani cha watu au eneo fulani la nchi. Yaani hakuna anayekuwa na ulazima wa kutii mamlaka mtu anayoona au anayoamini haitendi haki na kiongozi pekee katika kuamua ni 'certain conscience' (dhamiri yenye uhakika kuhusu jambo fulani). Hii ni aina ya dhamiri ambayo mbele ya jambo fulani na kwa wakati huo wa kuamua mtu anasikia sauti ya ndani mwake ikimwambia tenda au acha. Dhamiri ya aina hii kwa kadiri inavyokushawishi kutenda au kuacha matokeo yake huwa ni furaha (kama ukifuata dhamiri yako inavyokushawishi au huzuni kama ukifanya jambo kinyume na dhamiri yako inavyokushawishi). Baada ya kuamua kutenda au kuacha, mtu anatakiwa kujiridhisha (kujua) kama jambo alililolitenda au acha kutenda ni jema au la. Na kupata habari hapa maana yake ni kuwa na 'well-informed conscience' (dhamiri ya kweli - kuamua kutenda au kuacha kutenda jambo kwa vile unajua bila shaka ukweli au undani wake). Ukiwa na 'doubtful conscience' (dhamiri ya mashaka) hupaswi kufanya uamuzi wowote mpaka hapo utakapokuwa na uhakika wa jambo lenyewe (certain conscience). Na hapa kuwa na uhakika haina maana ya kuwa sahihi maana unaweza kuwa na uhakika wakati uko wrong pia.
 
Back
Top Bottom