Habari hizi za kimataifa kwa manufaa ya nani hapa Tanzania?

Habari hizi za kimataifa kwa manufaa ya nani hapa Tanzania?

AKILI TATU

JF-Expert Member
Joined
Feb 10, 2016
Posts
2,659
Reaction score
2,827
Wakongwe wa tasnia ya habari akiwemo mkuu Pascal Mayalla mtanisaidia kujua ukweli wa hili.

Kwa muda mrefu redio na TV zimekuwa na hizi habari wanazoziita za kimataifa na wakati mwingine wanavuka na kuzichambua kabisa, kiukweli Sina Shaka na hilo, lakini Shaka inakuja wanatuletea habari za kimataifa ambazo hazina impact kwenye jamii yetu, mfano unakuta kuna tukio la ukabaji huko Syrian au labda ajali ya gari wamekufa watu wanne huko China, au magari yamegongana huko Afrika Kusini, sasa najiuliza habari kama.hizi Sisi wasikilizaji au watazamaji zinafaifa gani kwetu au ndio uvivu wa wahariri na upungufu wa mbinu za kutafuta habari za maana?

Lakini pia najiuliza, je huko nje ambalo tunashobokea Sana kuripotiwa habari zao nao wanashoboka kuripoti habari zetu hizi local mfano za kupanda na kushuka kwa tozo au Ile ya Rais Mwinyi kukutana na madaktari wa China juzi hapa?

Tunaambiwa miaka na miaka kuhusu habari za machafuko huko sijui wapi, lakini kila nikisikiliza najiuliza hizi habari kama hizo na zingine impacts zake ni zipi kwetu wasikilizaji, au ni lazima habari inaposomwa au kuandika lazima ziwepo hizo za kimataifa?

Au ni uvivu kwa wandishi wetu wa habari pamoja wahariri kuingia huko ndani ndani ya nchi na kutuletea habari maana akili yangu unakataa kuwa Tanzania hakuna habari mpaka kila ukifunguliwa redio au TV ukute wanatuletea hizo wanazoziita habari za kimataifa tena wakati mwingine hazina impact yeyote Ile Kwa jamii yetu au nchi kwa ujumla?
 
Ukivaa nguo za nje bila ya kuvaa nguo za ndani utajihisi mwili kupwaya.. Ukivaa za ndani peke yake bila za nje utajiwekea mipaka ya kuonekana hadharani

Ndani ya masaa 24 ya siku kuna wakati unahitaji kuvaa nguo za nje tuu na kuna wakati unahitaji kuvaa za ndani tuu na kuna wakati unahitaji kuvaa zote.

Tunazo taarifa za habari za ndani tuu
Tunazo taarifa za habari za nje tuu
Ma tunazo taarifa za habari mchanganyiko za nje na za ndani

Not hizi zina umuhimu wake kama nguo za ndani na nguo za nje
 
Ukivaa nguo za nje bila ya kuvaa nguo za ndani utajihisi mwili kupwaya.. Ukivaa za ndani peke yake bila za nje utajiwekea mipaka ya kuonekana hadharani
Ndani ya masaa 24 ya siku kuna wakati unahitaji kuvaa nguo za nje tuu na kuna wakati unahitaji kuvaa za ndani tuu na kuna wakati unahitaji kuvaa zote.

Tunazo taarifa za habari za ndani tuu
Tunazo taarifa za habari za nje tuu
Ma tunazo taarifa za habari mchanganyiko za nje na za ndani

Not hizi zina umuhimu wake kama nguo za ndani na nguo za nje
Swali je huko nnje hizi local news zetu wanazipa airtime kama ambavyo Sisi kutwa ukifunguliwa hizi redio na TV wanatuhabarisha kuhusu minor issue kwenye jamii za mataifa mengine...elewa habari nazomaanisha na kuhoji hapa NI hizi minor issue , mfano sijui mafuriko kidogo ya maji, sijui ajali za kawaida ambazo hapa pia ziko na zinatokeaga? Simaanishi hizi za kina biden , na harakati zao maana hizi kweli zinamashiko Kwa dunia ya sasa.

Zile za Rais WA Ghana kufungua kiwanda cha dawa za mmbu. Sisi huku zinatuhusu nini?
 
Kimsingi si kila tukio ni habari iwe ndani au nje. Shida ipo kwenye level ya elimu, wanahabari wengi (siyo wote) ni makanjanja. Ata IQ zao ziko chini, fuatilia redio za FM , wanaongea vitu vya kijinga sana, contents za hovyo kabisa na watangazaji ni kama ma bar maid au wauza mitumba wa manzese
 
Kimsingi si kila tukio ni habari iwe ndani au nje. Shida ipo kwenye level ya elimu, wanahabari wengi (siyo wote) ni makanjanja. Ata IQ zao ziko chini, fuatilia redio za FM , wanaongea vitu vya kijinga sana, contents za hovyo kabisa na watangazaji ni kama ma bar maid au wauza mitumba wa manzese
Hakika umeongea vyema Kaka. Haya mambo wanahabari wetu wanatuangusha Sana...hawajui watulishe nin wasikilizaji wao
 
Akili mgando hii, hapa ndipo uwezo wako wa kufikili ulipo ishia?sitak kuamin hili kaa tafakari majib ya unacho uliza yapo kichwani mwako kijana.
 
Swali je huko nnje hizi local news zetu wanazipa airtime kama ambavyo Sisi kutwa ukifunguliwa hizi redio na TV wanatuhabarisha kuhusu minor issue kwenye jamii za mataifa mengine...elewa habari nazomaanisha na kuhoji hapa NI hizi minor issue , mfano sijui mafuriko kidogo ya maji, sijui ajali za kawaida ambazo hapa pia ziko na zinatokeaga ..!? Simaanishi hizi za kina biden , na harakati zao maana hizi kweli zinamashiko Kwa dunia ya sasa...

Zile za Rais WA Ghana kufungua kiwanda cha dawa za mmbu...Sisi huku zinatuhusu nini..!?
Kwakuwa mimi siishi huko nje ni vigumu kulijibu hilo swali lakini kwa muktadha wa nguo nikivaa mimi wengine wakaifanya mjadala mkubwa nguo yangu hiyo kutokana na uzuri ama ubaya wake SI lazima nami nifanye hivyo kwa nguo zao
 
Leo nime sikiliza habari saa moja kamili clouds fm (habari za kimataifa) nimeipenda msomaji wa habari kasema Raisi wa congo DRC kamtuhumu wazi wazi Rwanda kwa kuvamia nchi yake.

Hii ili tokea baada ya Rwanda kuingiza majeshi yake nchini DRC kuwasaidia waasi wa M23 [emoji3] kinyume na makubaliano ya sheria ya kimataifa nime sahau sijui ni ya mwaka gani iliyo tungwa na kujadiliwa ... nimeasahau ali sema msomaji wa habari.

Hapo hapo Rwanda nao wana wa tuhumu serikali ya Tshekedi (Rasi wa DRC) kwa kufadhili kundi la waasi wa EFDL [emoji23][emoji23] ipo siku yaja hawa majirani zetu wata toana roho. [emoji30][emoji2296]

Kwa mtazamo wangu Rwanda ndio muonezi wa Congo nae ni kama ma beberu tu, ana waibia mali DRC ndio maana ana fadhili makundi kama M23 ili vita visiishe aendelee kupiga mali za DRC. Kagame ni boonge la snitch [emoji19]

NB: umbea kama huu kuupata kwenye Tv, Radio stations naona una faida kujua hali za majirani zetu na nini kinacho endelea huko over [emoji23][emoji482]
 
Dunia ni kijiji ndugu yangu kua updated ni jambo jema. Kibaya ni kupewa habari za nje tu na habari za ndani kukosa.
 
Wakisema habari ziwe za ndani tu, kuna muda utawaza hivi haya yanatokea kwetu tu mbona sijawahi kusikia nchi nyngine?

Lakini wakitoa na za nje inabalance habari, inasaidia kujua kumbe kuna nchi nazo ajali zinatokea pia kuna matukio ya kihalifu. Pia inasaidia kujua nchi nyingine wanatumia njia gani kupambana na changamoto zinazowakumba, hii inaweza kutusaidia na sisi kujifunza kutoka kwao.

Mwisho kabisa kuna watanzania wanaishi nje ya nchi (huenda ni kwenye hizo nchi) naye anafuatilia vyanzo vya habari vya nyumbani kwaiyo inamsaidia kupata habari za huko alipo kupitia vyombo vya habari vya Tz. Pia kama ni ajali au majanga mengine itasaidia wale watz wenye ndugu kwenye hiyo nchi husika kuwasiliana na ndugu zake kujua kama wapo salama kwenye hizo nchi.
 
Wakongwe WA tasnia ya habari akiwemo mkuu Pascal Mayalla mtanisaidia kujua ukweli WA hili.
Mkuu AKILI TATU, asante kwa hili tena ni jambo la muhimu sana.
Kwa muda mrefu redio na TV zimekuwa na hizi habari wanazoziita za kimataifa na wakati mwingine wanavuka na kuzichambua kabisa...kiukweli Sina Shaka na hilo, lakini Shaka inakuja wanatuletea habari za kimataifa ambazo hazina impact kwenye jamii yetu..mfano unakuta kuna tukio la ukabaji huko Syrian au labda ajali ya gari wamekufa watu wanne huko China, au magari yamegongana huko afrika kusin ,..sasa najiuliza habari kama.hizi Sisi wasikilizaji au watazamaji zinafaifa gani kwetu au ndio uvivu WA wahariri na upungufu WA mbinu za kutafuta habari za maana!?
Naunga mkono hoja, habari za kimataifa zina lengo zuri la kuwapasha habari Watanzania kile kinachoendelea huko ulimwenguni ila kama tukikijua kina impact kwetu. Ni kweli mara kibao zinaripotiwa taarifa ambazo hazina impact wala relevance yoyote kwetu kwa uvivu na uwezo duni wa baadhi ya wahariri.
Lakini pia najiuliza ..je huko nnje ambalo tunashobokea Sana kuripotiwa habari zao nao wanashoboka kuripoti habari zetu hizi local
Kiukweli hawana kabisa time na habari zetu local, sa maendeleo ila kukitokea majanga, mbio utawaona. Mfano CNN haina correspondents Tanzania ili likotokea la kutokea anatumwa from Nairobi. Wakati wa genocide ya Rwanda CNN walionyesha dilapidated and decomposed bodies za human being ikielea Ziwa Victoria na kupelekea kupigwa marufuku minofu ya samaki. Wakati vita vya Iraq na Libya pia walionyesha miili ya watu dead bodies lakini kwenye September 11, hakuna mwili wowote ulioonyeshwa!. Kwetu wanaona mabaya tuu!. https://www.jamiiforums.com/threads...hakuna-mazuri-yotote-ya-kuyaangazia.1471986/l
mfano za kupanda na kushuka Kwa tozo au Ile ya Rais Mwinyi kukutana na madaktari WA China juzi hapa..!?
Hili sio habari kabisa kwao ila China wanaturipoti vizur
Tunaambiwa miaka na Miaka.kuhusu habari za machafuko huko sijui wapi...lakini kila nikisikiliza najiuliza hizi habari kama hizo na zingine impacts zake NI zipi kwetu WA sikilizaji..au ni lazima habari inaposomwa au kuandika lazima ziwepo hizo za kimataifa..!?
Si lazima ila kuna habari za machafuko huko kwao zina impact kwetu kama vita vya Russia na Ukraine.
Au ni uvivu Kwa wandishli wetu WA habari pamoja wahariri kuingia huko Ndani ndani ya nchi na kutuletea habari..maana akili yangu unakataa kuwa Tanzania hakuna habari mpaka Kila ukifunguliwa redio au TV ukute wanatuletea hizo wanazoziita habari za kimataifa TENA wakati mwingine hazina impact yeyote Ile Kwa jamii yetu au nchi Kwa ujumla!?
Sio uvivu ni resources, kuna habari nyingi tuu za maendeleo vijijini lakini media zetu haziripoti due to lack of resources kuzifikia wakati international news zinapatikana bure
P.
 
Ulimwengu upo viganjani, habari ni kupata habari jinsi ulimwengu unavyokwenda, yakiwemo na matukio yake.

Mfano, mi nikiamka mpaka jioni huwa napenda kujua matukio mbalimbali yaliyotokea duniani; nisipofanikisha hilo najiona kama nipo kijijini sana.

Kiufupi, wapo wanaozifuatilia; hata ukifatilia zingine za ndani, zinakuwa hazina impact, ila kwa sababu ni habari, inabidi kusikiliza tu.​
 
Kwani Hauna Choice ?!!! Kama haya wanafanya TBC inayoendeshwa na Tozo zetu basi hapo una haki ya kulalamika ila kama ni hao wengine hata kama wanaonyesha (Paint Drying on a Wall) its their prerogative, wewe unao uwezo wa kuchukua remote na kwenda pengine (na wengi tukifanya hivyo basi watakufa kifo cha kawaida)
 
Mkuu AKILI TATU, asante kwa hili tena ni jambo la muhimu sana.

Naunga mkono hoja, habari za kimataifa zina lengo zuri la kuwapasha habari Watanzania kile kinachoendelea huko ulimwenguni ila kama tukikijua kina impact kwetu. Ni kweli mara kibao zinaripotiwa taarifa ambazo hazina impact wala relevance yoyote kwetu kwa uvivu na uwezo duni wa baadhi ya wahariri.

Kiukweli hawana kabisa time na habari zetu local, sa maendeleo ila kukitokea majanga, mbio utawaona. Mfano CNN haina correspondents Tanzania ili likotokea la kutokea anatumwa from Nairobi. Wakati wa genocide ya Rwanda CNN walionyesha dilapidated and decomposed bodies za human being ikielea Ziwa Victoria na kupelekea kupigwa marufuku minofu ya samaki. Wakati vita vya Iraq na Libya pia walionyesha miili ya watu dead bodies lakini kwenye September 11, hakuna mwili wowote ulioonyeshwa!. Kwetu wanaona mabaya tuu!. https://www.jamiiforums.com/threads...hakuna-mazuri-yotote-ya-kuyaangazia.1471986/l

Hili sio habari kabisa kwao ila China wanaturipoti vizur

Si lazima ila kuna habari za machafuko huko kwao zina impact kwetu kama vita vya Russia na Ukraine.

Sio uvivu ni resources, kuna habari nyingi tuu za maendeleo vijijini lakini media zetu haziripoti due to lack of resources kuzifikia wakati international news zinapatikana bure
P.
Mkuu unafikiri kuna siku kutakuwa na changes kwenye haya...Kwa sababu now uwepo WA teknolojia umerahisisha ukusanywaji WA taarifa...why iwe shida Kwa waandishi wetu kuingia front line kutupa kinachotokea ndanda huko nk.!? Basi hata hapo jirani Kenya, uganda na Rwanda kweli tunashindwaje kuwa na corresponding journalists . Kwenye haya maeneo..au ni uthubutu hatuna!?
 
Back
Top Bottom