Tetesi: Habari zaanza kuvuja kuhusu zilikoenda Trilioni 1.5 "zilizopotea"

Tetesi: Habari zaanza kuvuja kuhusu zilikoenda Trilioni 1.5 "zilizopotea"

Tuko Malawi au Tanznania?
Kama ni mtafuta habari, read as widely as possible ili upate uwezo wa kuchuja real news na fake news! Mleta mada kabeba hearsay asizoweza kuzicredit popote isipokuwa watu wasiotaka kujitambilisha!
 
..nina hakika kama hii ni kweli basi bashite atakuwa mmoja wa wanufaika wa pesa hizi....hakuna Mkuu wa mkoa amejenga majumba makubwa dar Na mwanzakwa kipindi kifupi hhivyo kwa mshahara tu tena akiwa madarakani....lazima bashite yumo kwenye ushetani huu....BTW...ilisemekana nae anashiriki kuwaajiri kimagumashi hao wanaojiita Usalama...ama vikosi maalum aka watu wasiojulikana.... Kwenye hili kama ni kweli bashite hakosekani....BTW..hivi ile tume ya maadili ya viongozi ilifia wapi??mbona Hawa wezi hawachunguzwi????
 
Nasikia kila tarehe 15 ya kila mwezi waganga maarufu chini ya Bashite huenda Ikulu kufanya yao... Bashite ndio mtu aliyemtafutia hao waganga JIWE... Ndio maana Bashite na Jiwe ni kama chanda na Pete
Kuna wakati Mkulu hakubali kuandaliwa kiti au chakula akiwa ziara! Huenda pia waganga walisema epuka kupanda ndege!
 
Kama ni mtafuta habari, read as widely as possible ili upate uwezo wa kuchuja real news na fake news! Mleta mada kabeba hearsay asizoweza kuzicredit popote isipokuwa watu wasiotaka kujitambilisha!
Mkuu, unataka tuseme hizi habari nani katoa ndio uamini? Na for as long as hautuweki ushahidi wa kimaandishi hapa basi tunapaswa kuziita tetesi. Kama ungekuwa wewe ndio umetoa hizi habari ungetaka niweke jina lako ili watu waziamini? Kubali kwamba nimesema habari kutoka chanzo cha kuaminika, japo tumezipa kichwa cha tetesi. Uliza wewe kama una ndugu kwenye system labda watakuthibitishia.
 
Huo ni uongo! Ni ajira kiasi gani zimetengenezwa za kugharimu 1.5T Tzs hata kama mmenunua vifaa??? Wafanyakazi wote wa Umma wanalipwa fedha kiasi gani? Hapa mnajaribu kutengeneza mwelekeo mpya wa upepo.
Kuna watu kila mkiandika kitu manadhihirisha ukihiyo wenu. Hivi unajua gharama za operaesheni na intelijensia na usalama wewe? Ni pamoja na kuchoma moto Nissan Patrol mpya ikiwa inaweza kuhatarisha kutambuliwa kwa field agents. Angalau kaangalie picha za James Bond uone mabo ya usalama na intelijensia yanagharama kiasi gani. Wewe unafikiri gharama za intelijensia ni mishahara tu? Kweli unapaswa kuhurumiwa.
 
Kama ni hivyo basi ni vizuri sana maana serikali ilibidi itulize ghasia na ujinga uliokithiri hapa nchini. Sina kinyongo hata kidogo na hizo hela, Mh. rais wakomeshe tu waropokaji.
 
Habari kutoka vyanzo vinavyoaminika zimekuwa zikititirika juu ya ukweli kuhusu zilikoenda zile Trilion 1.5 ambazo zilionekana kama zimeyeyuka hewani, na kutolewa maelezo yasiyoridhisha na serikali.

Habari zilizopo ni kwamba sehemu kubwa ya fedha hizo zilipelekwa katika matumizi ambayo mamlaka toka juu iliamua yasiwekwe wazi, na kikubwa cha matumizi hayo yakiwa ni mambo ya ki intelijensia/usalama. Habari zimezidi kuanisha kwamba kwa mara ya kwanza toka nchi hii ipate uhuru, kumekuwa na matumizi ya kutisha katika idara zote zote za serikali zinazohusiana na mambo ya usalama zaidi sana ya fedha wanazokuwa wakitengewa.

Pia kumekuwa na ajira nyingi zisizofuata utaratibu na kuanzishwa kwa vitengo ndani ya vitengo ambavyo vingi sio rasmi na hivyo matumizi ya fedha za vitengo hivyo hayawezi kuwekwa wazi. Watu wengi wemeajiriwa katika idara hizi zisizo rasmi katika mazingira ya kibinafsi na maagizo kutoka juu badala ya kufuata taratibu rasmi za serikali, na wamekuwa wakitengewa fedha kwa ajili ya "kazi" zao.

Habari zimezidi kudai kwamba hata wakati wa awamu ya Nyerere ambapo kulikuwa na kiwango cha juu cha mambo ya intelijensia na usalama kutokana na Tanzania kuwa kitovu cha mambo ya ukombozi wa nchi za Afrika hatukufikia matumizi ya kiasi hiki. Mbaya zaidi mengi ni matumizi ambayo hayajainishwa na kufuata tarataibu za matumizi ya fedha za serikali, na hayawezi kuhojiwa na mtu yeyote wala kukaguliwa hata na CAG. Habari zimesema kuwa ni kama kwa sasa kuna "obsession" ya mambo ya usalama na intelijensia, na watu wanaotumikia katika sehemu hizi ambazo nyingine sio rasmi wamepewa uhuru wa kutumia fedha wanavyopenda.
vyanzo vipi mkuu !naona ramli chonganishi katika ubora wake
 
Habari kutoka vyanzo vinavyoaminika zimekuwa zikititirika juu ya ukweli kuhusu zilikoenda zile Trilion 1.5 ambazo zilionekana kama zimeyeyuka hewani, na kutolewa maelezo yasiyoridhisha na serikali.

Habari zilizopo ni kwamba sehemu kubwa ya fedha hizo zilipelekwa katika matumizi ambayo mamlaka toka juu iliamua yasiwekwe wazi, na kikubwa cha matumizi hayo yakiwa ni mambo ya ki intelijensia/usalama. Habari zimezidi kuanisha kwamba kwa mara ya kwanza toka nchi hii ipate uhuru, kumekuwa na matumizi ya kutisha katika idara zote zote za serikali zinazohusiana na mambo ya usalama zaidi sana ya fedha wanazokuwa wakitengewa.

Pia kumekuwa na ajira nyingi zisizofuata utaratibu na kuanzishwa kwa vitengo ndani ya vitengo ambavyo vingi sio rasmi na hivyo matumizi ya fedha za vitengo hivyo hayawezi kuwekwa wazi. Watu wengi wemeajiriwa katika idara hizi zisizo rasmi katika mazingira ya kibinafsi na maagizo kutoka juu badala ya kufuata taratibu rasmi za serikali, na wamekuwa wakitengewa fedha kwa ajili ya "kazi" zao.

Habari zimezidi kudai kwamba hata wakati wa awamu ya Nyerere ambapo kulikuwa na kiwango cha juu cha mambo ya intelijensia na usalama kutokana na Tanzania kuwa kitovu cha mambo ya ukombozi wa nchi za Afrika hatukufikia matumizi ya kiasi hiki. Mbaya zaidi mengi ni matumizi ambayo hayajainishwa na kufuata tarataibu za matumizi ya fedha za serikali, na hayawezi kuhojiwa na mtu yeyote wala kukaguliwa hata na CAG. Habari zimesema kuwa ni kama kwa sasa kuna "obsession" ya mambo ya usalama na intelijensia, na watu wanaotumikia katika sehemu hizi ambazo nyingine sio rasmi wamepewa uhuru wa kutumia fedha wanavyopenda.
Swali ni uhalali wa kutawala haujatoka kwa wapigakura
 
Kama ni hivyo basi ni vizuri sana maana serikali ilibidi itulize ghasia na ujinga uliokithiri hapa nchini. Sina kinyongo hata kidogo na hizo hela, Mh. rais wakomeshe tu waropokaji.
Hahaha! Juzi hapa kuna watu walikuwa wanasifia watu wakomeshwee, wakajikuta wamekomeshwa na wao kunyimwa mikopo ya chuo kikuu kwa kuwa walisoma private. Leo wanamlaani Mkulu. Kwa hiyo na wewe zamu yako bado, patakuja tu pa kukukomesha. Tundu alishasema hakuna atakaekwepa kukomeshwa, usidhani wewe uko salama!
 
vyanzo vipi mkuu !naona ramli chonganishi katika ubora wake
Mkuu, hata huko huko ndani ya taasisi nyeti usidhani ni wote wanaofurahia haya mambo. Kina James Mbatia watakuambia wakati wa ule mgomo wa Mwinyi kutukanwa matusi ya nguoni chanzo kikuu cha habari za ndani za Mwinyi likuwa huko huko usalama!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Janga kubwa sana la Taifa huyu dhalimu. Tume iundwe haraka ili kuchunguza hizi pesa ambazo zinaweza kabisa kuwa zimegubikwa na wizi na ufisadi wa kutisha.

Habari kutoka vyanzo vinavyoaminika zimekuwa zikititirika juu ya ukweli kuhusu zilikoenda zile Trilion 1.5 ambazo zilionekana kama zimeyeyuka hewani, na kutolewa maelezo yasiyoridhisha na serikali.

Habari zilizopo ni kwamba sehemu kubwa ya fedha hizo zilipelekwa katika matumizi ambayo mamlaka toka juu iliamua yasiwekwe wazi, na kikubwa cha matumizi hayo yakiwa ni mambo ya ki intelijensia/usalama. Habari zimezidi kuanisha kwamba kwa mara ya kwanza toka nchi hii ipate uhuru, kumekuwa na matumizi ya kutisha katika idara zote zote za serikali zinazohusiana na mambo ya usalama zaidi sana ya fedha wanazokuwa wakitengewa.

Pia kumekuwa na ajira nyingi zisizofuata utaratibu na kuanzishwa kwa vitengo ndani ya vitengo ambavyo vingi sio rasmi na hivyo matumizi ya fedha za vitengo hivyo hayawezi kuwekwa wazi. Watu wengi wemeajiriwa katika idara hizi zisizo rasmi katika mazingira ya kibinafsi na maagizo kutoka juu badala ya kufuata taratibu rasmi za serikali, na wamekuwa wakitengewa fedha kwa ajili ya "kazi" zao.

Habari zimezidi kudai kwamba hata wakati wa awamu ya Nyerere ambapo kulikuwa na kiwango cha juu cha mambo ya intelijensia na usalama kutokana na Tanzania kuwa kitovu cha mambo ya ukombozi wa nchi za Afrika hatukufikia matumizi ya kiasi hiki. Mbaya zaidi mengi ni matumizi ambayo hayajainishwa na kufuata tarataibu za matumizi ya fedha za serikali, na hayawezi kuhojiwa na mtu yeyote wala kukaguliwa hata na CAG. Habari zimesema kuwa ni kama kwa sasa kuna "obsession" ya mambo ya usalama na intelijensia, na watu wanaotumikia katika sehemu hizi ambazo nyingine sio rasmi wamepewa uhuru wa kutumia fedha wanavyopenda.
 
Ha ha haaaaaa,, wizi umehamishiwa JWTZ atakayehoji ajue anahoji kifaru cha jeshi!!
Hahahaha! Nasikia kuna kivuko fulani kibovu kilinunuliwa kwa mabilioni. Kilipokufa kabla ya kufanya kazi jeshi likapewa zawadi ili watu wasihoji😀😀😀
 
Unataka kuniambia nchi yetu ipo hatarini kuliko kipindi chochote kile cha uhuru?
No, ninataka kukuambia nchi yetu kwa mara ya kwanza ina kiongozi ambaye yuko paranoid, haamini mtu, anaogopa kila kitu hata kivuli chake, na ndio maana haachi kuomba aombewe. Yuko tayari hata kusikiliza ramli za waganga wa kienyeji kuhusu usalama wake.

Unakumbuka mtu wa namna hiyo kule Uganda alikuja kuwaje?
 
Kama unashindwa kuona kwamba maelezo yalitengenezwa rasmi ili "uelewe na kuamini", basi wewe na wengine kama wewe ni watu wa kuhurumia sana. Jiulize kwa nini maelezo hayo hakupewa CAG, na kama alipewa kwa nini hakuyaweka kwenye ripoti yake. Licha ya hivyuo, habari zinasema sehemu kubwa ya zile Trilioni 1.5, sio zote.

Na kama ni kweli nchi ya jirani wanasaidia mambo ya usalama, ni rahisi sana kufikisha Trilioni 1.5.
Maelezo yako ya mwanzo yalikuwa yana ingia akilini lakini ulipoanza kuingizia habari za usalama kusaidiwa na nchi jirani umeanza kupunguza uzito wa maelezo yako ya awali.

Hii habari ya kitoto ya kuhusu kuletwa kwa jamaa wa usalama wa nchi jirani inatia shaka sana. Labda kama ni mamluki waliokodiwa na mtu binafsi na sio serikali yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Naona mnawadharau sana watu wa taasisi yetu nyeti, inasikitisha sana zilipofikia siasa za Tanzania.
 
Na hapohapowatu wanapiga sana tu, na kununua midege bilakufuata utaratibu.

Mnashangilia tu mambo, mipewa bill inflated kwa rushwa mnalia.

Tukisema mambo yafuate utaratibu, tunaonekana wapinzani.
 
Back
Top Bottom