Hadi leo najiuliza, ilikuwaje tukajenga SGR kwenda Burundi na kuacha kuboresha TAZARA kuwa SGR ambapo tungefika Congo kirahisi sana

huwa sielewi kagame amewaroga kwa uchawi gani ccm....malori yanayokwenda rwanda ndiyo hayo unayakuta manyoni yamepaki yanasubiri mnada wa kuku walete dar.
Sasa huo ndiyo uchawi wenyewe wa mtz,yaani sisi wafuga kuku unatuona hatuna haki kabisa ya kutumia hayo malori?.
 
Yaani juzi hapa nimetoka Kaliua to Moro hapa,behewa zimefulu mpaka ile njia ya katikati ya behewa haipitiki. Reli ya kati ni muhimu sana kabla hata ya kufikiria nchi jirani.
 
Tazara ni tayari ni SGR ya kiwango kizuri tu.Huko Urusi na Ukraine wanayo na juzi mrusi kaitumia kusafirisha zana za vita.

Sema nashindwa kupandisha video hapa.

Ila hizi picha hapo chini ni Reli ya TAZARA.View attachment 2160677View attachment 2160679
 
Inahisisha kwenda home kirahisi mkuu 😂😂😂
SGR haiendi Uganda!
Inaishia Mwanza!

Kama target ni Congo , kulikuwa na haja gani kuipeleka Burundi na Rwanda tena kwa gharama kubwa sana?

Kwa nini tusingeboresha TAZARA na kufika Congo kirahisi sana?
 
..Matatizo ya Tazara hayapo ktk Gauge.

..Tazara kuwa Cape Gauge Rail naiona ni advantage kuliko disadvantage.
 
Hatujengi reli kwa ajili ya wacongo, warundi wala warwanda, tunajijengea reli kwa ajili yetu ili watanzania wasafiri na kusafirisha mizigo yao kwa gharama nafuu na hii itapelekea pia bidhaa kushuka bei. Sasa fikiria ni pande ipi ya nchi yenye wananchi wengi ya kupewa kipaumbele?
 
Kwa nini sasa haitiliwi mkazo na mkazo ukaenda kuwekwa njia inayoishia Kigoma na haina uhakika wa kufanyiwa Kazi kwa upande wa Burundi hadi Congo?
..Matatizo ya Tazara hayapo ktk Gauge.

..Tazara kuwa Cape Gauge Rail naiona ni advantage kuliko disadvantage.
 
Reli inajengwa kwa mkopo! Kwa pesa za Watanzania si utalipa de I kwa miaka 300?
 
Congo ni kubwa sana,

Tazara inaweza kupokea mizigo ya Lubumbashi, Burundi na Rwanda zinaweza kupokea mizigo ya Bukavu na Kisangani.

Kwahivyo kazi iendelee ya kuifungua nchi
Sasa kwa nini mkazo hauwekwi kwenye Tazara? Mji wa kibiashara ni Lubumbashi kwa nini hatuupi mkazo?

Huko Bukavu na Kisangani hata miundombinu tuna uhakika itafika hivi karibuni? Burundi wana uwezo wa kufikisha reli kwa viwango vya SGR huko Bukavu?
 
Unajua kuwa Reli inajengwa kwa fedha za mkopo? Kwa hela zako za madafu unadhani huo mkopo utaweza kuulipa ndani ya muda?

Tazara ni ya Tanzania na Zambia! Tumeshindwa kutumia uwezo wetu kidiplomasia kuhakikisha tunaboresha Tazara na kukamata soko kusini mwa Congo?
 
Unafahamu kuwa ni almost miezi miwili sasa Reli ya Tazara yaani Treni ya abiria na mizigo hazifanyi kazi kisa kuna sehemu imeharibika hapo Morogoro?
 
Hatuwezi kuboresha Taraza peke yetu bila kuihusisha Zambia ambayo ni mbia.

Isitoshe Zambia kwa sasa hawaitegemei sana Tazara kama miaka ya nyuma na reli ya SGR tumeijenga kwa manufaa yetu wenyewe kwa kuangalia vipaumbele vyetu kwa wananchi wa huko sio nchi jirani.
 
Maswali yako yote mawili hayana msingi; kwani madeni mengine huwa yanalipwaje? Kwa mfano hiz b10 za Uviko zitalipwa kutoka kwa jirani yupi. Watu tunafikiria infrastructure zitakazosaidia uchumi wetu kupanda kwa kuongeza productivity, siyo biashara ya duka hiyo.

Ni kweli TAZARA ni mali ya Tanzania na Zambia, je unaamini kuwa diplomasia ndiyo inayowafanya wafanya biashara wa Zambia watumie Tazara? Ndoto tupu hiyo isiyokuwa na msingi. Wafanya biashara wanatumia bandari yoyote yenye tija kwao. Tatizo la wafanbya biashara wa Zambia kuacha kutumia bandari ya Dar siyo kwa sababu ya TAZARA wala diplomasia, bali ilikuwa ni ucheleweshwaji hapo Dar Bandarini. Unakuta kule Durban mzigo unafika siku hiyo hiyo kesho yake unatoka getini, lakini Dar mzigo unafika unamaliza hadi wiki nzima kabla haujondoka kwenye geti.
 
Na rfk yangu anasukuma hiyo local motive ya makaburu...
 
Kasanga port huwa mnaizungumzia kwa faida ipi hasa? Mnaelewa hata jiografia ya eneo kweli?
 
Ndio hitaji la Kanda ya Ziwa hilo sio? Kwamba sgr itawatoa hapo no.17&18? 😁😁



 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…