Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nimeipenda sana shukrani mkuu , sasa niko najifunza jinsi ya ninavyofuatiliwa huku ninakula keki ya taifa na wanakijiji kwa siri.Story nzuri najua mdau wa story hii utaipenda
Hahaha Jf imepoa haina story nying kama wiki mbili zilizopita😃Nimeipenda sana shukrani mkuu , sasa niko najifunza jinsi ya ninavyofuatiliwa huku ninakula keki ya taifa na wanakijiji kwa siri.
Ilikuwa hatari sanaHahaha Jf imepoa haina story nying kama wiki mbili zilizopita[emoji2]
Nadhani utakuwa ni mwananchiJioni tutaendelea wakuu bado napisha break ya watani!!
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Ila kwa yoyote anayeguswa kutuma bando napokeaaa
Mbona kama tunaanza kupeana arosto mkuuKESI YA MZEE MNYOKA 11
Baada ya kutuma majibu ya sampuli zote Sasa Oscar alishamaliza kazi ya kwanza na hivyo alishajua lazima "Wenye Mali" watajitokeza kufanya kikao Cha dharula,
Alienda kibaruani Kama kawaida na huku akiomba Mungu yule Mlinzi wa Jana usiku asiwepo asubuhi hii, hata hivyo kwa namna alivyojiweka isingekuwa rahisi kutambulika,
Sasa Oscar alifanya kazi huku akiwa ametega masikio yake Kama kuna chochote kumsaidia ...
Ni wakati akiwa anapeleka box moja kule ofisini ndipo akasikia "jamaa" wawili wakipiga story,
"Ndio Ila nasikia order tayari imetoka yule Mzee apotezwe Kuna kila dalili yule Mzee ndio kasababisha huyo jamaa aingie Jana kuiba sampe, unaambiwa huyo jamaa Ni zaidi ya komando, maana kafanya yake halafu kayeyuka, mpaka Carlos mwenyewe unaambiwa kasanda game!"
"Ila mwanangu ujue hii sehemu hatari sana Basi tu"
Oscar aliweka box Kisha akatoka zake,
"Mzee Mnyoka Yuko hatarini" aliwaza ,
Kwa sheria za pale,
Kama Kibarua alikuja na simu Basi alitakiwa kukabidhi kwa Mlinzi , ilikua Ni marufuku kuingia na simu kazini,
Hivyo Oscar aliwaza na kuwazua, alitamani apige simu kwa Kimei au Josephine ili kuwatahadharisha kuhusu Mzee Mnyoka,
'ila niliwaambia wachukue tahadhari" alijisemea,
******
Hospitalini Kiomboi asubuhi saa 2:30,
Nesi Furaha akiwa kazini akiwa zamu ,
Siku hiyo alikua kwenye wodi ya wazazi pamoja na nesi mwenzake Janet,
Simu yake ya mkononi iliita ,
Kwa kuona tu yule mpigaji nesi Furaha akatabasamu na kuiweka Ile simu kifuani,
Janet alitabasamu tu, alimjua rafiki yake vizuri na hivyo akishagundua lazima simu Ile Ni ya mwanaume wake,
Furaha alitoka nje ya wodi na kupokea,
"Hello baby, "
"Hello d, jamani nilikuwa nakuwaza Sasa hivi tu, nawe ukapiga! Nesi Furaha aliongea kwa sauti legevu,
"Mi mwenyewe nimekumisi Sana huwezi Amini, Niko nje hapa mapokezi!"
Ilisikika sauti upande wa pili,
"Jamani honey, umenifuata Hadi kazini?"
Furaha Sasa aliongea huku akipiga hatua kutoka nje, ..
Aliendelea kupiga hatua huku akiongea na simu na mpenzi wake huyo,
Alifika nje na kumuona "mtu wake " akiwa amepaki Gari yake ndogo Nyeusi huku akiwa anazunguusha zunguusha funguo,
Alimfikia na wakaanza kukumbatiana,
Furaha hakujali umati wa watu pale nje,
Hakika walipendeza Sana,
"D Niko bize na kazi jamani, nimefurahi kukuona"
Furaha Sasa alisema huku akijaribu kujinasua mikononi mwa yule jamaa,
Ni wakati huo dokta kimei alikua nae akiingia ndani ya geti la hospitali, alipaki Gari yake Kisha akatoa simu yake na kupiga hatua, kuelekea ndani,
Wakati anakaribia mapokezi Sasa alimuona furaha na mpenzi wake dokta kimei alikua mtu wa utani Sana na alikua mtu mcheshi, manesi wote waliokuwa wanapangwa zamu na Dokta Kimei walifurahia Sana, hakuwa mtu wa kufuatilia Sana mambo,
Dokta Kimei Sasa aliwakaribia akina furaha,
"Oooh kaeni hivyo hivyo, mmependeza Sana, Sasa furaha weka pozi,.....
Ooh Yes, nice photo"
Dokta Kimei aliongea huku akiwa amepiga picha kadhaa kupitia simu yake,
"Nooo nooo! Huwezi kutupiga picha bila ridhaa, lete hiyo simu hapa!"
Mpenzi wake Furaha alibadilika ghafla , Dokta Kimei na Furaha wakaangaliana,
"Easy man, Easy!"
Dokta Kimei aliongea Sasa huku akichukua tahadhari kwa huyu jamaa aliyegeuka mbogo ghafla!
Dokta Kimei hakuwa mtu wa kupenda ugomvi kabisa, kwake yeye alichukulia Kama Jambo "dogo tu"
Hata nesi Furaha alimshangaa Sana mpenzi wake huyo, iweje akubali kukumbatiana hadharani halafu akatae kupigwa picha?
Nesi Furaha Sasa aliingilia Kati,
"Frank No, please usimfanyie fujo huyo Ni mkuu wangu wa kazi nakuomba please"
Furaha aliongea huku akimshika Mkono,
Dokta Kimei aliduwaa tu, baadhi ya watu Sasa walishaanza kunusa harufu ya ngumi na kuanza kuweka mazingira ya kusogea,
Frank Sasa alisita kumsogelea dokta Kimei,
"We mwanaharamu ungenijua, usingenichukulia poa"
Alijisemea mwenyewe halafu akarudi nyuma kwa mpenzi wake,
Dokta Kimei Sasa aliingia ndani kwani ulikua Ni muda wa kumuona mgonjwa wake Mzee Mnyoka kwa ajili ya chai ya asubuhi!
********
"Mimi sipendi kabisa kupigwa picha , ndio maana nikakasirika, ndio maana hunioni Facebook, Wala Twitter au kwenye sijui ma Nini huko, nipo hivi unavyoniona"
Frank aliongea huku akiwa amekaa na Furaha kwenye benchi moja ndani ya hospitali,
"Okay d nimekuelewa, vipi kazi lakini huko Mgodini, na mbona umekuja huku leo wakati kila siku unasema uko bize"
Furaha aliongea
"Yeah, Niko bize siku zote, nimekuja town Mara moja, Kuna karatasi fulani za kutuma huko serikalini, so nikaona nisiishie mjini nikutembelee kidogo," alisema Frank,
"Sasa si tunalala au, nimekumis ujue,"
Furaha aliongea Sasa kwa sauti ambayo kwa wanaume Mara nyingi huwa haiwi ombi tu Bali hugeuka amri,
"Poa, usijali"
Frank alijibu,
"Angalia we nenda Home, utamkuta dada pale, nampigia simu, Ila Sasa ujikaze ntakuja kukupikia mwenyewe chakula Cha mchana"
Alisema Furaha,
"Poa d, halafu , Kabla sijasahau Kuna Mzee wetu pale kijijini aliletwa huku aisee anaendeleaje?"
Frank aliongea huku akijifanya kuondoka kuonyesha kuwa "Hakujali" Sana habari za Mzee Mnyoka
"Mmh anaendelea vizuri kwakweli, yule dokta aliyetupiga picha ndio anamtibia"
Furaha aliongea Sasa bila wasi wasi,
"Yuko wodi namba ngapi aisee nimcheki"
Frank aliuliza,
"Haiko mbali twende"
Frank alitoa miwani yake akavaa! Wakaanza kupiga hatua mdogo kuelekea wodi alipo Mzee Mnyoka,
********
SAA 4:00 asubuh Dar es salaam
"Ni kweli, tumepata taarifa za uwepo wa urenium, Tena kwa kiwango Cha juu Sana, kupita tulivyodhani,"
Alisema Sasa Mr Allan, Mkurugenzi wa Idara ya usalama wa Taifa akiwa Kwenye kikao chake cha Siri na watu wake wa siku zote kwenye Mambo nyeti Kama haya,
Wenzake walikua kimya kabisa wakimsikiliza ..
"Kijana alituma sample usiku wa Jana, amefanya kwa haraka na kwa umakini mkubwa, Sasa nawasikiliza mnasemaje katika hatua hii inayofuata"
Alisema Mr Allan, huku akiwatazama wajumbe wale kwa macho yake makali,
"Kwanza, tuweke ni plan, kutokana na unyeti wa Jambo kwanza Mimi nilikua nashauri ibaki kuwa Siri yetu kwanza,
Halafu tuweke watu standby ili kumsaidia kijana kule,
Lakini pia ni vyema hizi taarifa zifike kwa Raisi moja kwa moja,"
Mr Oresta Sasa aliongea, huku akiweka koti lake vizuri Kama ilivyokuwa kawaida yake,
"Mimi Nina wazo mkuu, Ni wazi kuwa hawa watu wanakimbizana na muda, nao pia wanahofia, hivyo kuzidi kuchelewa Ni kuwapa wao nafasi ya kujipanga zaidi, lakini pia tunaweza kukosa ushahidi "
Sasa Bwana Rashid , aliongea ...
"Nadhani nimewasikia , hebu tupeane task jioni hii kila mmoja aje na plan ya kufanya misheni hii kwa wakati na umakini mkubwa, kesho asubuh tukutane , mahali pa kukutania nitawaambia, Ila muda Ni saa tano kamili, na kode yetu ya muda Ni "Pembe za ndovu"
Sasa Naahirisha kikao Chetu hiki,
Alisema Mr Allan, Kisha akachukua notebook yake na kutangulia,
Ndivyo walivyozoea kukutana, kila kikao na sehemu yake, Leo wangekutana kwenye jengo Hili, kesho wangekutana hoteli hii, kesho kutwa wangekutana kwenye nyumba flani, ili mradi tu vikao vyao vilikua katika Hali ya usiri mkubwa...
@ShunieKESI YA MZEE MNYOKA 11
Baada ya kutuma majibu ya sampuli zote Sasa Oscar alishamaliza kazi ya kwanza na hivyo alishajua lazima "Wenye Mali" watajitokeza kufanya kikao Cha dharula,
Alienda kibaruani Kama kawaida na huku akiomba Mungu yule Mlinzi wa Jana usiku asiwepo asubuhi hii, hata hivyo kwa namna alivyojiweka isingekuwa rahisi kutambulika,
Sasa Oscar alifanya kazi huku akiwa ametega masikio yake Kama kuna chochote kumsaidia ...
Ni wakati akiwa anapeleka box moja kule ofisini ndipo akasikia "jamaa" wawili wakipiga story,
"Ndio Ila nasikia order tayari imetoka yule Mzee apotezwe Kuna kila dalili yule Mzee ndio kasababisha huyo jamaa aingie Jana kuiba sampe, unaambiwa huyo jamaa Ni zaidi ya komando, maana kafanya yake halafu kayeyuka, mpaka Carlos mwenyewe unaambiwa kasanda game!"
"Ila mwanangu ujue hii sehemu hatari sana Basi tu"
Oscar aliweka box Kisha akatoka zake,
"Mzee Mnyoka Yuko hatarini" aliwaza ,
Kwa sheria za pale,
Kama Kibarua alikuja na simu Basi alitakiwa kukabidhi kwa Mlinzi , ilikua Ni marufuku kuingia na simu kazini,
Hivyo Oscar aliwaza na kuwazua, alitamani apige simu kwa Kimei au Josephine ili kuwatahadharisha kuhusu Mzee Mnyoka,
'ila niliwaambia wachukue tahadhari" alijisemea,
******
Hospitalini Kiomboi asubuhi saa 2:30,
Nesi Furaha akiwa kazini akiwa zamu ,
Siku hiyo alikua kwenye wodi ya wazazi pamoja na nesi mwenzake Janet,
Simu yake ya mkononi iliita ,
Kwa kuona tu yule mpigaji nesi Furaha akatabasamu na kuiweka Ile simu kifuani,
Janet alitabasamu tu, alimjua rafiki yake vizuri na hivyo akishagundua lazima simu Ile Ni ya mwanaume wake,
Furaha alitoka nje ya wodi na kupokea,
"Hello baby, "
"Hello d, jamani nilikuwa nakuwaza Sasa hivi tu, nawe ukapiga! Nesi Furaha aliongea kwa sauti legevu,
"Mi mwenyewe nimekumisi Sana huwezi Amini, Niko nje hapa mapokezi!"
Ilisikika sauti upande wa pili,
"Jamani honey, umenifuata Hadi kazini?"
Furaha Sasa aliongea huku akipiga hatua kutoka nje, ..
Aliendelea kupiga hatua huku akiongea na simu na mpenzi wake huyo,
Alifika nje na kumuona "mtu wake " akiwa amepaki Gari yake ndogo Nyeusi huku akiwa anazunguusha zunguusha funguo,
Alimfikia na wakaanza kukumbatiana,
Furaha hakujali umati wa watu pale nje,
Hakika walipendeza Sana,
"D Niko bize na kazi jamani, nimefurahi kukuona"
Furaha Sasa alisema huku akijaribu kujinasua mikononi mwa yule jamaa,
Ni wakati huo dokta kimei alikua nae akiingia ndani ya geti la hospitali, alipaki Gari yake Kisha akatoa simu yake na kupiga hatua, kuelekea ndani,
Wakati anakaribia mapokezi Sasa alimuona furaha na mpenzi wake dokta kimei alikua mtu wa utani Sana na alikua mtu mcheshi, manesi wote waliokuwa wanapangwa zamu na Dokta Kimei walifurahia Sana, hakuwa mtu wa kufuatilia Sana mambo,
Dokta Kimei Sasa aliwakaribia akina furaha,
"Oooh kaeni hivyo hivyo, mmependeza Sana, Sasa furaha weka pozi,.....
Ooh Yes, nice photo"
Dokta Kimei aliongea huku akiwa amepiga picha kadhaa kupitia simu yake,
"Nooo nooo! Huwezi kutupiga picha bila ridhaa, lete hiyo simu hapa!"
Mpenzi wake Furaha alibadilika ghafla , Dokta Kimei na Furaha wakaangaliana,
"Easy man, Easy!"
Dokta Kimei aliongea Sasa huku akichukua tahadhari kwa huyu jamaa aliyegeuka mbogo ghafla!
Dokta Kimei hakuwa mtu wa kupenda ugomvi kabisa, kwake yeye alichukulia Kama Jambo "dogo tu"
Hata nesi Furaha alimshangaa Sana mpenzi wake huyo, iweje akubali kukumbatiana hadharani halafu akatae kupigwa picha?
Nesi Furaha Sasa aliingilia Kati,
"Frank No, please usimfanyie fujo huyo Ni mkuu wangu wa kazi nakuomba please"
Furaha aliongea huku akimshika Mkono,
Dokta Kimei aliduwaa tu, baadhi ya watu Sasa walishaanza kunusa harufu ya ngumi na kuanza kuweka mazingira ya kusogea,
Frank Sasa alisita kumsogelea dokta Kimei,
"We mwanaharamu ungenijua, usingenichukulia poa"
Alijisemea mwenyewe halafu akarudi nyuma kwa mpenzi wake,
Dokta Kimei Sasa aliingia ndani kwani ulikua Ni muda wa kumuona mgonjwa wake Mzee Mnyoka kwa ajili ya chai ya asubuhi!
********
"Mimi sipendi kabisa kupigwa picha , ndio maana nikakasirika, ndio maana hunioni Facebook, Wala Twitter au kwenye sijui ma Nini huko, nipo hivi unavyoniona"
Frank aliongea huku akiwa amekaa na Furaha kwenye benchi moja ndani ya hospitali,
"Okay d nimekuelewa, vipi kazi lakini huko Mgodini, na mbona umekuja huku leo wakati kila siku unasema uko bize"
Furaha aliongea
"Yeah, Niko bize siku zote, nimekuja town Mara moja, Kuna karatasi fulani za kutuma huko serikalini, so nikaona nisiishie mjini nikutembelee kidogo," alisema Frank,
"Sasa si tunalala au, nimekumis ujue,"
Furaha aliongea Sasa kwa sauti ambayo kwa wanaume Mara nyingi huwa haiwi ombi tu Bali hugeuka amri,
"Poa, usijali"
Frank alijibu,
"Angalia we nenda Home, utamkuta dada pale, nampigia simu, Ila Sasa ujikaze ntakuja kukupikia mwenyewe chakula Cha mchana"
Alisema Furaha,
"Poa d, halafu , Kabla sijasahau Kuna Mzee wetu pale kijijini aliletwa huku aisee anaendeleaje?"
Frank aliongea huku akijifanya kuondoka kuonyesha kuwa "Hakujali" Sana habari za Mzee Mnyoka
"Mmh anaendelea vizuri kwakweli, yule dokta aliyetupiga picha ndio anamtibia"
Furaha aliongea Sasa bila wasi wasi,
"Yuko wodi namba ngapi aisee nimcheki"
Frank aliuliza,
"Haiko mbali twende"
Frank alitoa miwani yake akavaa! Wakaanza kupiga hatua mdogo kuelekea wodi alipo Mzee Mnyoka,
********
SAA 4:00 asubuh Dar es salaam
"Ni kweli, tumepata taarifa za uwepo wa urenium, Tena kwa kiwango Cha juu Sana, kupita tulivyodhani,"
Alisema Sasa Mr Allan, Mkurugenzi wa Idara ya usalama wa Taifa akiwa Kwenye kikao chake cha Siri na watu wake wa siku zote kwenye Mambo nyeti Kama haya,
Wenzake walikua kimya kabisa wakimsikiliza ..
"Kijana alituma sample usiku wa Jana, amefanya kwa haraka na kwa umakini mkubwa, Sasa nawasikiliza mnasemaje katika hatua hii inayofuata"
Alisema Mr Allan, huku akiwatazama wajumbe wale kwa macho yake makali,
"Kwanza, tuweke ni plan, kutokana na unyeti wa Jambo kwanza Mimi nilikua nashauri ibaki kuwa Siri yetu kwanza,
Halafu tuweke watu standby ili kumsaidia kijana kule,
Lakini pia ni vyema hizi taarifa zifike kwa Raisi moja kwa moja,"
Mr Oresta Sasa aliongea, huku akiweka koti lake vizuri Kama ilivyokuwa kawaida yake,
"Mimi Nina wazo mkuu, Ni wazi kuwa hawa watu wanakimbizana na muda, nao pia wanahofia, hivyo kuzidi kuchelewa Ni kuwapa wao nafasi ya kujipanga zaidi, lakini pia tunaweza kukosa ushahidi "
Sasa Bwana Rashid , aliongea ...
"Nadhani nimewasikia , hebu tupeane task jioni hii kila mmoja aje na plan ya kufanya misheni hii kwa wakati na umakini mkubwa, kesho asubuh tukutane , mahali pa kukutania nitawaambia, Ila muda Ni saa tano kamili, na kode yetu ya muda Ni "Pembe za ndovu"
Sasa Naahirisha kikao Chetu hiki,
Alisema Mr Allan, Kisha akachukua notebook yake na kutangulia,
Ndivyo walivyozoea kukutana, kila kikao na sehemu yake, Leo wangekutana kwenye jengo Hili, kesho wangekutana hoteli hii, kesho kutwa wangekutana kwenye nyumba flani, ili mradi tu vikao vyao vilikua katika Hali ya usiri mkubwa...
Shukrani dear@Shunie
Jana na leo...nipo mkuuHamuwezi Jutia kusoma hii story wanangu wa faida. Waswahili wanaita Bonge la story na mwandishi anamaliza hajawahi zingua. .
Analyse Half american Watu8 Numbisa Amehlo Depal wao ni wao Shunie Kalpana Dejane leadermoe Antonnia Lovelovie Depal Darlin Nuzulati Synod Binadamu Mtakatifu Johnnie Walker Glenn Mamaya Dahan moneytalk Cee Omar B Salum Dr Restart Numbisa Mo mp5 Santos06 Angel Nylon baby zu shikamkono01
Majukum.ya ndoa yanakuzid sijakuon mdaJana na leo...nipo mkuu