MADAM PRESIDENT 06
Sasa nilipata picha kuwa wale waliokuja kutuvamia juzi na kupuliza dawa walikua wametumwa na madam kuja kuiba picha na Cheti Cha ndoa, pengine madam alitaka kujiridhisha baada ya kupeleleza na kujua nimeoa Sasa alitaka kupata uthibitisho...
Niliwaza Kisha nikampigia Simu mke wangu kuwa nimekosa pia ..nilibadili nguo Kisha nikaona nitumie Ile piki piki kupigia misele, niliangalia mafuta na kukuta yapo ya kutosha nikaondoka na kwenda mjini kwa Shemeji yangu Aida.
Niliwasili baada ya muda mfupi na kumkuta akiwa nae anarudi
"Haya wewe mzungu vipi Tena za siku "
Alitabasamu baada ya kuniona alifungua akaingia ndani
"Shemeji yake Mimi nimekuja kula njaa inauma Sana"
Nilisema huku nikisogea kwenye friji kuangalia kinywaji....
"Usijisumbue mwenzangu Leo walikuja hao wajomba zako wamekomba friji lote kaa hapo nikuangalizie kinywaji dukani"
Alisema Tena akiingia chumbani,
"Halafu Shemeji yake cheki samaki Basi Nina hamu na ugali samaki leo!"
Nilisema nikikaa kwenye sofa pale sebuleni baada ya dakika kadhaa Shemeji Aida alirudi na kutengeneza chakula Kisha nikamwambia kilichonipeleka..
"Shemeji yake Nina Shida kidogo Kuna kitu unisaidie, nataka nikutoe kidogo hapa mjini ukakae na mdogo wako mpaka atakapojifungua ni zaidi ya miezi miwili kutoka Sasa"
"We mwanaume ! Unaniletea balaa gani Tena, na nyumba yangu namuachia Nani Tena!"
"Hahaha Shemeji yake Sasa hapo unatakiwa ujiongeze, unajua kuwa kila nikija hapa nikikuletea Shida najua unanisaidia 100%, na kila nikija ujue Sina sehemu Nyingine ya kwenda Tena!"
Nilisema kwa upole,
"Shemu unajua kabisa naweza kukusaidia, majukumu yangu yaani na siwez kuacha nyumba bila mtu"
"Yule mdogo wako Aisha vipi kwanini asije kukaa hapa halafu wewe na wajomba muende huko mkakae ,Ni nyumba kubwa tu usijali na itakuwa poa kukiwa na watu wengi wengi, Kama itakuwa Shida pia tutafute mtu alinde nyumba tumlipe!"
Nilisema
"Mh mpaka unasema hivyo kweli umetaitika Shem, sikiliza kesho asubuhi saa 4 nitakupigia kukupa jibu"..
Alisema.
"Shemeji yake, nakutegemea sana Kuna Mambo yakimalizika salama baada ya hiyo miezi miwili utapata zawadi yako nzuri kabisa"
Nilisema.
"Kwahiyo umeshamtoa Mary hapa mjini?"
Aliuliza
"Ndio Tangu Juzi, unajua baada ya wale wezi kutuvamia nikaona hapa mjini hapamfai Tena"
Nilimalizia
******************
Nilirudi mjini na kuzunguuka zunguuka kwenye mitaa huku nikiomba Mungu Aida akubali kwenda mabatini.
Niliamua kwenda kulala nje kidgo ya mji kwa siku hii ya Leo...
"Nitaishi Kama kunguru Hadi lini"
Niliwaza nikiigia kwenye gesti hii ya lala salama.
****************
Kama nilivyowaza Shemeji Aida alikubali kwa masharti kuwa ataondoka na watoto wake kwa bahati amepata shoga yake ambaye atamuachia nyumba ...
Nilimpigia mke wangu kumueleza kuhusu ujio wa Aida na watoto wake,
Kisha nikamtafuta Jose ili jioni ampeleke.
"Sasa kazi inaweza kuanza"
Ilipita wiki moja na nikawa natembelea Ile piki piki kupiga misele tu, mwishowe nikaona siwezi kulala vichochoroni kila siku,
Siku hiyo jioni kwenye majira ya saa 12 niliingia kwenye kibanda Cha kutoa huduma za mtandao nilikua na taarifa fulani ya kutuma Wizarani..
Nilishangaa kuona ujumbe mwingine ambao kwasasa niliweza kujua umetoka kwa Jacob ...
"Wazee wa Ngwasuma"
Uliandikwa hivyo tu...
Kwa haraka nikawaza maana yake na mahali niliposikia Hilo neno
Nilimaliza kutuma taarifa zangu Kisha nikatoka nje..
Baadae nikakumbuka maneno haya anayatamka DJ Mark Yule ambaye atafsiri Filamu lakini kabla ya kusema wazee wa Ngwasuma huwa anaanza na neno "wanakuja, wazee wa Ngwasuma"
Akimaanisha watu katili, wauaji n.k...
"Kwa maana hiyo wamekuja"
Nilijisemea
Nilitembea hatua kadhaa na sikutaka kununua chakula badala yake nilitamani kwenda kupika nilipiga hatua kadhaa kwa kujiamini na tayari Giza lilikua lishaanza nilikua nakaribia mitaa ya kwangu wakati Gari lililokua na vioo vyeusi lilipopaki pembeni yangu
Upande wa dereva alishusha vioo na kuniita...
"Samahani Broo tunauliza kwa afisa Elimu bwana Ruta, "
Alisema.
"Ah hamko mbali Sana nyoosheni na njia hii hii mkifika pale darajani Kuna nyumba kubwa yenye geti jeusi mkono wa kulia ndio hapo hapo"
Nilisema huku nikitaka kuendelea na Safari yangu..
"Sasa Broo si unaelekea huko huko ingia Basi utusaidie sisi Ni wageni kabisa"
Alisema huku akifungua mlango..
Sikujiuliza Mara mbili nikaingia kwenye Gari na Sasa nilijikuta natazamana uso kwa uso na mitutu ya bunduki!
Zaidi ya dereva kulikua na watu wengine watatu ambao walifunika nyuso zao huku wakiwa na bunduki zao
Waliniweka Kati Kati na Gari ikageuzwa kurudi mjini....
"Mnafanya makosa Sana jamaa!"
Nilisema kwa kujiamini..
"Ndio tumefanya makosa maana tulitakiwa tukukamate Tangu siku Nne zilizopita mbwa wewe"
Mmoja alisema huku wenzake wakicheka..
Mmoja alinisachi mfukoni na kutoa waleti pamoja na simu zangu mbili,
Kisha wakanifunga kitambaa usoni wakati nataka kupambana nao nivue kile kitambaa nikahisi kuchomwa na kitu chenye ncha Kali mkononi na taratibu nikajikuta nalegea na Kisha kupoteza fahamu.
*******************
Nilikuja kuzinduka baadae na kujikuta Nikiwa kwenye chumba kimoja kikubwa kulikua na kiti mbele yangu na nilikua nimefungwa kamba mikononi na miguuni na kutupwa sakafuni..
Nilijaribu kufungua macho kijanja kuangalia huko na huko lakini sikuona mtu...
Nilijaribu kujinyoosha nyoosha na sikujisikia maumivu yoyote yale ...
Ni baada ya muda kidogo aliingia jamaa mmoja akaja kunifungua kamba Kisha akaninyanyua nilisimama mwenyewe Kisha akanitanguliza kwenye chumba kingine ambacho kulikua na chakula
"Kula aisee"
Yule jamaa alisema
Nilisogea pale mezani nikapiga ule msosi kwa spidi ya ajabu nilipomaliza nikapewa nguo za kubadili Kisha nikapelekwa kwenye chumba kingine nikaoga nikabadili nguo Kisha nikatolewa kwenye Ile nyumba na kuzunguuka kwenye nyumba iliyokuwa pembeni...
Sasa kulikua na jamaa mmoja mbele mwingine nyuma tukapanda kuelekea kwenye chumba kimoja kilichokua ghorofani,
Tulikaa pale sebuleni kwa dakika kadhaa baadae mngurumo wa Gari ukasikika....
"Kaa Hapo "
Mmoja alise Kisha akatoka nje ya chumba na mmoja akabaki kunilinda akiwa na bunduki mkononi,
Ya muda mfupi mlango ulifunguliwa akaingia madam Janet akiwa na walinzi wake kadhaa
Madam aliwakonyeza wale walinzi wake wakatoka nje ingawa mmoja aligoma kabisa kutoka na badala yake alisogea tu pembeni kidogo pamoja na kumuonyeshea ishara ya mkono atoke nje Yule mlinzi aligoma kabisa na ndio kwanza alikua anajiweka sawa..
"Janet siamini Kama Ni wewe uko behind this"
Nilianza kusema huku nikimtolea macho Janet
"Shut up, Allan, hivi wema wote niliokufanyia wewe ndio wa kunifanya Mimi chizi? Hivi unajua thamani ya penzi langu wewe mjinga wewe! Nakuuliza wewe mjinga wewe!?"
Alisema huku akiachia kibao kimoja kikali Sana,
Nilitulia tuli maana Sasa ningefanya chochote kile ingemaanisha kufa mapema, Hata hivyo pamoja na kumjua Janet kwa miaka yote sijawahi kumuona akiwa amekasirika hivyo..
"Sorry nipe nafasi njieleze Basi"
Nilisema..
"Wewe Mimi sio mtoto mdogo, umeoa na mtoto juu na mke wako Sasa hivi mjamzito kipindi chote kile nakuweka moyoni na kukufanyia wema wote huo unanifanya mchepuko!, Mimi ndio wa kunifanya mchepuko wewe? Nakuuliza Tena mbwa wewe! Mimi Ni mchepukoo?"
Janet Sasa aliporomosha kila Aina ya matusi nilitulia tu
Sasa leo utajua kuwa Mimi Ni Janet ,
"Hivi unajua nguvu ya Raisi wewe mbwa wewe?"
"Nataka nikufanyie kitu ambacho hutaamini Allan "
Alisema Janet.
"Okay Kama umeamua kuniua Janet then kill me with your own hands"
Nilisema huku nikionyesha dalili za kukata tamaa kabisa...
"Nikikuua Nitakuwa nimekupendelea , nataka uteseke ujute kuzaliwa " alisema Janet
"Kulikuwa na haja gani ya kunidanganya yaani Mimi nimekupa mapenzi kwa Moyo wote napata tabu kukuandalia mazingira narisk mpaka kazi yangu nakuingiza mpaka ikulu kumbe huna lolote mbwa wewe!" Alisema Tena kwa ukali akiachia kibao kingine...
"Hebu mtoeni hapa ,
Alisema Janet na wakaingia watu wawili wakaniinua na kunipeleka chumba Cha pili kulikokuwa na minyororo wakanifunga ukutani.
Janet aliingia Kisha akanisogelea..
"Sijaona mwanaume mpumbavu Kama wewe , haya nakupa nafasi ya mwisho..
Kama utakubali kumuacha huyo mke wako kipenzi Mary Dafa, ama ufe huku una jiona"
Alisema janet,
"Sijakuelewa Janet , unamaanisha Nini, unataka kuniua Janet?"
Nilisema nikitetemeka
"Kwanini nikuache hai? Huna faida kwangu, una dakika tano za kufanya maamuzi, kubali kumuacha mkeo kiroho Safi hapa tunaongozana Hadi ikulu kwa Raha zetu, ama uishie huku huku porini"
Nakupa dakika tano za kufikiria....