Hadithi ya mashimo ya mfalme Sulemani

SURA YA KUMI NA SITA


Giza lilikuwa limekwisha ingia siku ya tatu tulipofika mahali pa kupiga kambi chini ya ‘Vichawi Vitatu’ yaani ile milima mitatu iliyokuwa mwisho wa Njia Kuu ya Sulemani.

Katika safari yetu tulikuwa sisi watatu, na Foulata, na Infadus, na Gagula aliyechukuliwa katika machela, ambaye daima tulimsikia akitukana na kuguna, na askari wachache pamoja na viongozi na watumishi.

Siwezi kusahau milima ile namna ilivyokuwa katika mwangaza wa jua la asubuhi; ilikwenda juu sana hata kufika mawinguni.


Tulipotazama juu tuliona Njia Kuu ya Sulemani inakwenda moja kwa moja mpaka kilele cha katikati, mwendo wa kiasi cha saa mbili.


Afadhali nisijaribu kueleza mambo tuliyokutana nayo katika safari hii, msomaji na akisie mwenyewe.

Lakini sasa tunakaribia mashimo yale ya ajabu ambayo ndiyo sababu aliyofia Yule mzee Mreno zama za miaka mia tatu nyuma, na tena Yule mjukuu wake aliyekuwa rafiki yangu, na tena, labda hata na ndugu yake Bwana Henry.


Je, ajali yetu itakuwa ya namna hiyo hiyo? Wao walipatwa na maovu kama alivyosema Yule kichawi Gagula; na sisi je? Tulipokuwa tukienda katika ile njia nzuri sikuweza kujizuia nisiwe na hofu. Na tena nadhani Bwana Good na Bwana Henry vile vile walikuwa na hofu.


Kwa muda wa saa moja na nusu tulikwenda kwa miguu upesi upesi tukivutwa na tamaa, hata wale waliochukua machela waliona shida kufuatana nasi, na Gagula akatoa kichwa chake katika machela akasema, ‘Nendeni pole pole nyinyi watu weupe, nyinyi mtafutao hazina, mbona mnakwenda mbio kuonana na maovu ?’

Akacheka kicheko cha uhabithi kilichochukiza sana na kufanya mwili kunisisimka, na kwa muda kidogo tulipunguza mwendo wetu.


Basi tuliendelea kwenda mpaka tuliona shimo kubwa lililokwenda chini sana mbele yetu, katikati ya mahali tulipo na kile kilele. Nikamuuliza Bwana Henry, ‘Je, unajua shimo hili ni la nini?’

Yeye na Bwana Good wakatikisa vichwa vyao. Nikawaambia, ‘Ni dhahiri kuwa hamjapata kuona mahali panapochimbwa almasi.


Nadhani shimo hili ni shimo la kuchimba almasi.’
Basi tulifuata njia ili tupate kutazama vitu vitatu tulivyoona kutoka mbali kidogo, na tulipokaribia tuliona kuwa ni Wale Watatu Walio Kimya, wanaoogopwa na Wakukuana. Lakini hatukutambua vema ukubwa wao mpaka tulipofika karibu kabisa.


Hapo tuliona masanamu matatu, na baina ya kila sanamu na mwenzake ilikuwa nafasi ya hatua ishirini, na wote wanatazama uwanda wa Loo. Masanamu mawili yalikuwa ya wanaume na lile la tatu lilikuwa la mwanamke.


Basi tulisimama tukatazama sana masanamu yale, na baadaye kidogo Infadus akatujia, akainua mkuki wake kuyaamkia yale masanamu, akatuuliza kama tunataka kuingia Mahali pa Mauti sasa hivi, au tutangoja mpaka kwisha chakula cha mchana.
 
Ikiwa tunataka kwenda sasa hivi, basi Gagula yu tayari kutuongoza.

Kwa kuwa ilikuwa saa tano tu, nasi tulikuwa na hamu sana kupatazama mahali penyewe, tulisema kwamba tunataka kwenda sasa hivi, nami nikatoa shauri kama afadhali tuchukue chakula pamoja nasi, maana labda tutakawia katika mahali penyewe.
Basi machela ya Gagula ikaletwa, akatoka ndani.


Huko nyuma Foulata aliweka nyama na vibuyu viwili vya maji katika kikapu. Gagula alipotoka katika machela akacheka na akajikongoja kushika njia. Sisi tulimfuata, mpaka kwenye mlango wa pango.


Hapo Gagula akasimama akatungojea, na hata hivi sasa akicheka kicheko cha uhabithi. Akasema, ‘Sasa watu weupe waliotoka katika nyota, mashujaa wenye busara, mtayari?


Tazama mimi nipo hapa kufanya aliyoniamuru bwana wangu mfalme, yaani kuwaonyesheni hazina na mawe meupe yanayong’aa.Ha!Ha!Ha!’
Nikajibu, ‘Sisi tu tayari.’


Akasema, ‘Vema! Vema! Jipeni moyo mpate kuvumilia mtakayo yaona. Nawe Infadus, utakuja, wewe uliye mhaini bwana wako?’


Infadus akakunja uso kwa hasira, akajibu, ‘La, mimi siji, hayanihusu. Lakini wewe, Gagula, utawale ulimi wako, wangalie pia mabwana zangu.


Mimi ninawatia katika mikono yako, na ukiudhuru hata unywele mmoja, wewe Gagula, utakufa, hata ukiwa mchawi wa namna gani! Umisikia?’


Gagula akajibu, ‘Nasikia Infadus. Lakini usiogope, mimi maisha nafuata amri za mfalme tu. Mimi nimefuata amri za wafalme wengi Infadus, lakini mwisho wao walifuata amri zangu mimi.

Ha!Ha! Nakwenda kutazama nyuso zao mara moja tena, na vile vile nitatazama uso wa Twala. Haya twendeni, twendeni.’


Akachukua kibuyu cha mafuta akatia utambi kama taa. Bwana Good akamuuliza Foulata, ‘Unakuja, Foulata?’ Akajibu, ‘Naogopa, bwana wangu.’ Akasema, ‘Basi nipe kikapu.’

Akajibu, ‘La, bwana wangu, uendako nami nitakwenda.’ Basi Gagula hakungoja zaidi, akaingia katika ule mlango, tukaona kuwa ni kinjia cha kutosha watu wawili kwenda pamoja, tena giza tupu.

Tukamfuata Gagula huku tukiogopa na kutetemeka; tukasikia kishindo cha mbawa, na mara Bwana Good akauliza, ‘Je, nini kile, kitu kimenipiga usoni?’ Nikasema, ‘Haya twendeni, alikuwa ni popo tu.’


Basi tukaenda mbele na tulipokuwa tumekwisha kwenda kadiri ya hatua hamsini tuliona kuwa giza linapungua, na halafu tukajiona katika mahali pa ajabu.
 
Tumo katika pango kubwa lililo kwenda juu sana, hata kwa juu lilikuwa kadiri ya hatua mia moja. Kutoka pango hilo mapango madogo yaliingia katika mlima.

Basi tulitaka kutazama kila mahali, lakini Gagula hakutupa nafasi, yeye alikwenda mbele mpaka mwisho wa pango kubwa, tukamfuata.

Tulipofika huko tuliona mlango mwingine na Gagula akatugeukia akauliza, ‘Mko tayari kuingia katika Mahali pa Mauti?’

Tukajibu, ‘Haya tu tayari.’
Bwana Henry akasema, Mambo yanaanza kutisha sasa.’ Basi wakanipa nafasi mimi nitangulie, lakini katika roho yangu niliogopa, mpaka Bwana Good aliposema, ‘Haya, twende rafiki, au kiongozi wetu mzuri atatupoteza.’


Basi kuambiwa haya, nikaanza kuingia katika kinjia, na baada ya hatua ishirini hivi, nilijiona katika pango lingine.

Lilikuwa giza kidogo, lakini nilipozoea giza niliona meza ndefu na mwisho wa meza sanamu jeupe kubwa imekaa, na kuzunguka meza masanamu meupe mengine yenye kimo cha mtu.

Tena nikaona katikati sanamu jingine jeusi kidogo, na macho yangu yalipozoea giza nilitambua masanamu yale ni nini, nikageuka nikakimbia kutoka pango lile kadiri nilivyoweza kwenda mbio.


Kwa kawaida mimi siyo muoga sana, wala siogopi mambo ya kishetani, lakini nakiri kuwa niliyoyaona yalinitisha sana, na Bwana Henry asingalinizuia ningetoka pangoni upesi, na nisingekubali kuingia tena, hata kwa almasi zote zilizopo duniani.


Lakini Bwana Henry alinikamata baraabara, na kwa hivyo nilisimama, Lakini, mara na yeye macho yake yalizoea giza na yeye aliona yale niliyoyaona mimi, mara akaniacha akaanza kujifuta jasho usoni.


Bwana Good akashangaa kabisa, na Foulata akamkumbatia huku akilia tu. Gagula tu ndiye aliyecheka sana.

Mambo tuliyoyaona yakawa ya kutisha mno. Maana mwisho wa meza ile ndefu tuliona mifupa ya mtu mrefu sana, urefu wa futi kumi na tano au zaidi, naye ameshika mkuki mkononi, akawa kama sanamu za hayo Mauti yenyewe.

Nikasema, ‘Je, hi! Ni nini?’ Na Bwana Good akaonyesha wale waliokuwa wamekaa mezani akasema, ‘Na hawa ni nani?’


Na Bwana Henry akaonyesha Yule mweusi kidogo akauliza, ‘Na huyu ni nani?’
Gagula akacheka, ‘Hee!Hee!Hee! Maovu yanawajia wote waingiao Mahali pa Mauti. Hee! Hee!Hee!Ha!Ha! Njoo Ndovu, wewe uliye shujaa katika vita, njoo mtazame Yule uliyemuua.’


Na kizee huyu akamshika kwa vidole vyake vyembamba akamwongoza kwenye meza. Sisi tukafuata. Alipofika akasimama akamwonyesha Yule mweusi kidogo, Bwana Henry akastuka akarudi nyuma.

Maana pale mezani maiti yaTwala ilikuwepo, mfalme wa hivi karibuni wa Wakukuana, alikaa na kichwa chake amekipakata.

Na maiti huyo alifunikwa chumvi; tukasikia matone ya maji yakidondoka, tukafahamu kuwa maiti ya Twala inageuzwa kuwa jiwe, yaani kwa dawa iliyomo katika yale maji yanyodondoka.


Tukatazama masanamu yale mengine na tukafahamu Maiti za wafalme wa zamani zimekaa kuzunguka meza, na maiti ya mfalme Twala imekaa juu ya meza imepakata kuwa wale ni maiti wafalme wa zamani, na sasa wamekwisha geuka kuwa masanamu ya mawe kwa ile dawa.

Tukahesabu masanamu ishirini na saba, na ile ya mwisho ilikuwa sanamu ya baba yake Ignosi, na kila moja limegeuka jiwe.

Tukaona kuwa desturi hii ya kuweka maiti za wafalme hapa ni ya zamani sana. Lakini sanamu ile kubwa iliokaa mwisho wa meza tuliona kuwa ni kazi ya mikono ya watu wale waliochonga Wale Watatu Walio Kimya.
 
Umetisha Mkuu... Umetisha sana
 
Bwana Good alilala masaa 18 [emoji23] [emoji23] [emoji23], noma ssna Makumazahn
 
[emoji39] [emoji119] [emoji119]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…